Tofauti kati ya NYERERE na KIKWETE

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,739
155,436
2.jpg

1.jpg

3.jpg


4.jpg


5.jpg
 
mbona hatuku endelea wakati mkulu yupo ikulu ? ila haya ndio yalikuwepo:
  • kulima kwa jembe kama anavolima yeye hapo kwenye picha , hatimae chakula hakuna badala yake tukila sembe ya njano ya ngome kutoka marekani
  • raia hawakua na uhuru wowote , walingizwa vijijini kumuimbia mkulu..kama ile hekaya ya animal farm
  • uzalishaji ulipungua kutoka kilimo mpaka viwandani
  • kukawa hakuna kitu madukani
  • ujanja ukaanza..kila mwaka akawa anabadilisha noti ili walokua nazo wakiambiwa walanguzi na kunyanganywa
  • alichukua kwa nguvu nyumba za raia ati kazitaifisha.....hapa naona aliigwa na Iddi Amin...kwani yeye alizichukua nyumba zote za nchi hii alijua kuwa wahindi na wengineo wataona Tanzania pagumu watahama.......
  • mashamba ya raia aliyachukua bila ya fidia..naona comrade Mugabe hayupo pekee
  • Mabanks na makampuni ya Bima aliyataifisha yote bila ya fidia
  • kuagiza gari mpaka upate kibali na ueleze umepata wapi hela....rushwa ilitumika kupata ka- Peugeot
  • HATIMAE TUKAFUNGA MPAKA NA MALAWI...ALIKUA HAIVI NA BANDA
  • TUKAKOROFISHANA NA MABUTU....MPAKA NAO UKAFUNGWA ..KWA KUWASAPOTI KINA KABILA MKUBWA
  • MKULU AKAPELEKA JESHI UGANDA ILI KUMREJESHA RAFIKIYE...OBOTE....HATIMAYE WANAJESHI WAKAULIWA BURE
  • CHOKO CHOKO ZIKATAWALA JUMUIYA YA AFRICA MASHARIKI IKAVUNJIKA...MKULU AKATUTAKA TUFUNGE MKANDA HALI MBAYA
  • AKAFUNGA MPAKA NA KENYA ...NA KUWATUKANA JIRANI HAWA KWA KUWAITA MANYANGAU...
  • KUFUNGWA MPAKA HUU NI SISI NDIO TULIO PATA TABU..MAANA HATUKUWA NA KITU..TUKITEGEMEA MAHITAJI MENGI KUTOKA KENYA...MPAKA HUU ALIKUJA KUUFUNGUA MZEE WETU MWINYI
  • HATIMAYE AKAWAKARIBISHA WAPINZANI WA AMIN KINA TITO , OBOTE NA MUSEVENI...WAKAPEWA MAFUNZO NA UGANDA IKAVAMIWA..
  • VITA ILE ILIMGOA AMIN LAKINI MADENI YAKE MPAKA KESHO..ROHO ZA WATU ZIKAPOTEA KWA YASIO TUHUSU
  • HAPO MKULU AKASEMA HELA HAMNA TUFUNGE MKANDA TUNDU YA MWISHO.
  • KILA ULIEMUONA TAABAN
  • HUMU NDANI HAKUSIKILZA MAWAZO YA WENGINE
  • IKAWA FIKRA ZA MWENYEKITI ZIDUMU WEWE KAMA UNA FIKRA ZAKO UTAPOTEA
  • MKULU ALIKUA NA TV PEKEE YAKE
  • WATU WALIINGIZA TV KWA MAGENDO ZIKAJA KUCHUKULIWA WAKATI WA KUWAIBIA WATU ATI ULANGUZI
  • TV ZENYEWE WABONGO TULIKUA TUNAANGALIA VEDIO TUU......HAKUKUWA NA KITUO CHA TELEVISION
  • GAZETI NI UHURU NA DAILY NEWS TUUU
  • RADIO NI RTD TU
  • ULIZA RTC NI NINI WAKATI WA MKULU
  • WATU WALIKUA NA CARD ZA CHAKULA KWA WIKI UNAPATA KILO YAKO MOJA YA SEMBE
  • PETROL ILIKUA KWA CARD UNAPEWA LITA ZAKO 10 KWA WIKI....UKIWA NA SAFARI SHAURI YAKO
  • MARAFIKI WETU WALIKUA NI MA DICTORS DUNIANI...KINA CHAUSESCU WA ROMANIA, MAO WA CHINA, MANGISTU WA ETHIOPIA, BREZGNEV WA URUSI....SIASA ZA WAUWAJI WA KUBWA NA MAWAZO YAO KINA LENIN NA STALIN NDIO SIASA ZETU...
  • JEE UNAJUA HUYU STALIN ALIUUWA WARUSI WENGI ZAIDI KULIKO WARUSI WALOKUFA VITA VYA PILI ? SASA SIASA ZA HAW NDIO ILIKUA MAWAZO YETU MASHULENI.
  • JEE WAJUA KUHUSU VITA VYA BIAFRA , HUKO NIGERIA ? MKULU ALIPELEKA JESHI LETU KUWASAIDIA BIAFRA IJITENGE NA NOGERIA.
  • JEE UNAFAHAMU KWA ZAIDI YA MARA 5 VIJANA WA BONGO WALITAKA KUMWEKA KANDO MKULU? ALITAKA KUPINDULIWA NA KINA KAMBONA 1968
  • NA KINA BIBI TITI NA WENZAKE...AKAWAFUNGA.....HAYA YOTE NI KWASABU NCHI ILIKUA INAENDA ARIJOJO
  • NA MIAKA YA 80 KINA UNCLE TOM , HANSPOPE NA WENZAKE WALITAKA PIA KUMWEKA MKULU KANDO AKASALIMIKA....ALIKIMBIA ZANZIBAR...MPAKA HALI ILIPOTULIA...
  • KUONESHA MFUMO WAKE ULIKUA UMEWACHOSHA WATU...WALIPOKAMATWA KINA UNCLE TOM WALIWEZA KUTOROSHWA KUTOKA MIXIMUM SECURITY PRISON .....HATIMAE WAZIRI WA MAMBO YA NDANI ALIJIUZULU...
  • JEE UNAJUAA MWAKA 1968 ALIWASIMAMISHA JANGWANI KWENYE MKUTANO WA HADHARA ALIYEKUWA BALOZI WA TANZANIA MAREKANI..OTHMAN SHARIF PAMOJA NA MAKAMO WA RAIS WA ZANZIBAR KASSIM HANGA ATI WAMETAKA KUPINDUA SERIKALI YA ZANZIBAR !!! WAKATI BALOZI HUYU ALIMWITA ARUDI KUNA KAZI ?
  • BAADA YA MKUTANO ULE ALIWAREJESHA ZANZIBAR NA HAWAKUONEKENA TENA MPAKA LEO...
  • JEE WAJUA VIJAA WA LOCHOKA KULA SEMBE LA NJANO WALITELKA NDEGE YA ATC WAKATI WA MKULU.. NA KUIPELEKA HADI LONDON WAKA DEMAND MKULU AWACHIE WAFUNGWA WA KISIASA NA KUJIUZULU URAIS UMEMSHINDA ?
  • JEE WA JUA MIAKA MIWILI BAADAE WA BONGO KWA MARA NYENGINE WALIICHUKUA ATC IKIWA ANGANI WAKIWA NA LENGO KAMA LA WENZAO WA MWANZO.....INGAWA HAWA HAWAKUFANIKIWA ATC ILIRUDI DSM NA KUTUA
  • HAYA YOTE NI KWA SABABU WATU WALICHOKA.....
  • SASA KUMLINGANISHA MKULU NA KIKWETE ....KWELI NI TOFAUTI.....JAPO ALIKUA BOSI WAKE LAKINI WAKO TOFAUTI..KIKWETE ANATAWALA KUFATA SHERIA NA HAKI ZA WATU......NA ANALIMA KWA KUBOTA NA MATREKTA......NA FEDHA ZA MIKOPO KWA WAKULIMA...NDIO MAAANA CHAKULA KIPO HAKUNA SHIDA....LAKINI JEMBE LA MKONO LA MKULU ILIKUA KAMA ALIVO SEMA MWENYEWE 'KILIMO NI SIASA'
 
Uwe unalinganisha... ukitaja baya la Nyerere utaje na la Kikwete pia.
Ukitaja wema wa Kikwete, utaje na wa Nyerere pia.
hapo mizani ita balance.
 
Tuna umasikini wa kujitakia kwa sababu jm analea mafisadi.
 
Mmoja mgalatia na mwingine mujahidina,hiyo ndiyo tofauti yao kubwa!
 
Acha Porojom hizo za Mwaka 47777777777777777777777777777777777777777777777777777777777 Wewe hukumbuki Dunia kwa kipindi kile tuylikuwa nyuma sasa malizetu zote zinauzwa eti unalinganisha na miaka ile linganisha na enzi ya Ukapa na Ukiwete wasasa alaaaaaaaaaaaa
 
hajakuwa ataacha awezi kufananisha sindano na pembe ya ng'ombe enzi hizo wengi walikuwa hawajasoma sasa wizi ulikuwa ni wa mtu mmoja sasa akili kichwani kwako
Conquest-paka ni paka hata akiwa kama tembo
 
Back
Top Bottom