aaah! mods naomba mic niwakilishe.
oh! baby!
nimekaa na kutulia, mengi nimefikiri
Mawazo yamenijia, tangu tulipoanzia
shairi nakutungia , nielewe my dia
mwenzio ninaumia, please say wewe pia
Kila nikikuangalia, kweli umekamilika
nguvu zinaniishia, nikuite malaika?
moyoni ninaumia, mwenzio nasononeka
Penzi lako nalilia, usije wakakuteka
Natamani kuwa nawe, sekunde kila dakika
Liwalo acha na liwe, moyoni nimekuweka
Mola acha asifiwe, alokuumba ukaumbika
Daima mimi na wewe, wazi wazi natamka
Napenda sauti yako, ukitaja jina langu
Hufichi hisia zako, ukiwa pembeni yangu
Kukusaliti ni mwiko, umetosha kiu yangu
Milele mimi ni wako, kwavile wewe ni wangu.
Nasifu zako tabia, Wazazi nawapa sifa
Mtoto umetulia, akili na maarifa
"Honey! nimekupikia", unanipa taarifa
Darling nimekuzimia, nakupa zote nyadhifa.
Usiku ukiingia, mapema wajitayarisha
Visa wanisimulia, vyengine vya kuchekesha
Uchokozi waishia, na kuanzisha tamasha
Nami nalimalizia, na koja nimekuvisha.
Macho ukiniangalia , taabani sijiwezi
mwendo u kitembea, laniuwa lako pozi
Nyumbani nakungojea, fanya hima laazizi
Zawadi mekuletea , za kukupa usingizi.
Nina mengi ya kusema, lakini muda hautoshi
Nakuombea uzima, Uzidi wako ucheshi
Unithamini daima, kwa harusi na mazishi
Ewe changu chema, Unukiae marashi.
Ni malenga wenu klorokwini a.k.a ileile "bukta la jeshi"
Yaaani Kloro kaanzisha sredi???
Tena li-Songi la Awilo Longomba??
Kudadadadadadadada deki zake, kweli sasa amepona.
heheh na huyu ndio mjukuu mtiifu. Kumbe na mistari ipo? aiseee!Breaking News: Klorokwin In Love lol
Hakika amesikia, kiliocho kakipata
Anatikisa mkia, moyoni kakupakata
Raha anaisikia, mawingu umeyakata
Sema baba usikike, usijekufa kwa kihoro............................
hehehe Lokassa ya mbongo! Hizi anga za Klorokwini a.k.a director wa Titanic wewe unatafta nini? wewe acha nikuwekee wimbo unaokuhusu hapa chini. Uskilize kwa makini halaf ulipe hela yangu haraka.
klorokwini unatishia mzee hii mistari ni balaa, du ngoja nami niandike nitarudi....
Shairi limetulia, kwa vina kupangilia
mtoto wamsifia, moyoni washangilia
malaika wamdhania, na penzi walilia
mapenzi yana hadaa, ndugu yangu klorokwini
mapenzi yana ghiliba, ndugu yangu tahadhari
yasije geuka mwiba, na mengi yenye shari
wengine wakaja iba, waile yako sukari
mapenzi yana hadaa, ndugu yangu klorokwini
Nyadhifa zote wampa, eti umedhamiria
siku akija kutupa, wapi utakimbilia
je akigeuka papa, ni vipi utatwambia
mapenzi yana hadaa, ndugu yangu klorokwini
Tabia zabadilika, kama upepo masika
leo yu malaika,namba wani ameshika
vipi akija kuchoka, na mapenzi kuyazika
mapenzi yana hadaa, ndugu yangu klorokwini
Hapa natamatia, namini umesikia
ni vyema kuzingatia,yaweza kusaidia
mola akupe na nia, usipatwe na kadhia
mapenzi yana hadaa, ndugu yangu klorokwini
Hahaha.....namimi naweza nikawa malenga
khaaaa!Kloro ntakupeleka studio. Safisha hilo bukta lako na mabuti.
khaaaa!
heehehe mkuu post lako mikwala miiingi, halaf uskute studio lenyewe linarekodi kiduku.Njo kwenye studio yangu urecord bureeeeee, ila usije kuimba kwa staili ya kubana pua.
nilikuwa naishi jirani na shaban robert lakini nyumba yangu ikabomolewa na CCM.Kloro limetulia kweli shairi..kumbe uko 'talented' eeh!!...Bravo
unajaribu mic?kheee! Khiíi! Khooo! Khuuu!
unajaribu mic?
ndio maana unaleta usanii mpaka kwenye PM, haya njoo haraka huku na usanii wako, kabla Inbox langu halijajaa.mi msanii kloro ila sipendi umaarufu.
ndio maana unaleta usanii mpaka kwenye PM, haya njoo haraka huku na usanii wako, kabla Inbox langu halijajaa.
PM=Panga Mapema. haya njoo tupange halaka kabla uporoto hajavamia jukwaa.PM ndio Prime minister eeh?