Huko kusini hususani Mtwara ndio ufisadi ulikojaa, kwa hiyo magamba mmewakamata kweli kweli k.m Newala ndiko kuna magodowm ya korosho alishauziwa Kalamagi siku nyingi, viwanda vidogovidogo vya kubangua korosho vilivyopo Mtwara mjini waliisha wahi wajanja nashindwa hata kuwataja na mashine wamehamishia sehemu nyingine, wakati Murji akiwa mbunge Newala na mwenzie Dr Alex Khalid walijaribu kulizungumzia hili la kuhujumu miundo mbinu ya korosho matokeo yake Murji akapigwa ban na magamba wenzie amesota weeee ndio mwisho akahamia kugombea Mtwara mjini nako amehonga karibu miaka miwili. Mbaya zaidi bandari ambayo ilikuwa imeajiri wamakonde wengi nayo imeuzwa kwa hio huko magamba hawana ujanja mmewakamata pabaya. Kielelezo cha umaskini wa Mtwara wambieni waende Mtwara maeneo ya magalani kuna kiwanda cha kubangua korosho cha wahindi lile jingo lilikuwa la mamlaka ya korosho ndani yake akina mama kama 2000 wameajiriwa wanabangua korosho kwa kutumia mikono na vimashine Fulani vya miguu sasa kawaangalie mikono ilivyoliwa na mafuta makali ya korosho lazima yeyote mwenye huruma atawahurumia sana kwa sababu risk ni kubwa malipo ni kichekesho niliacha wanapewa elfu 4000 kwa siku na wanalipwa jumamosi sh 28,000 elfu Kazi hiyo akina mama a Mtwara mjini hawaitaki kabisa wanachofanya wale wahindi wameweka mawakala kuwatafutia nguvu kazi toka vijiji jirani kama Ziwani, Msangamkuu, Naliendele , Moma nk kwa hakika mpaka uwe maskini wa kutupwa ndo kazi ile utafanya. Ninachowaombeni makamanda wakati mnawajuza wananchi au mnapowafungua macho msiseme kwa ukali na kuonyesha hali ya jazba kwani kufanya hivyo magamba wataogopa kwa hiyo hata mkishinda hawatawapeni nchi maana wataogopa mtawakamata watasema tu wacha liwe litakavyokuwa inaweza kuishia kama ya BAGBO wa Ivory Coast, punguzeni ile hali ya munkali. Ushauri wangu ndio huo. CHADEMA KAMATA MWIZI MEEEEN.