To make quick money, start your own church

Prodigal Son

JF-Expert Member
Dec 9, 2009
1,067
697
To make quick money, start your own church

By Arusha Times Reporter

Monotonous high pitched voices, unintelligible prayers and corrupted gospel songs that disturb your neighbourhood daily could be a scam designed by imposters who are all out to make money in the name of the Lord. Watch out.
Church leaders from about 20 Christendom denominations in Arusha region have expressed concern that their faith was being misused by some imposters who reap money 'in the name of the lord!'
Speaking during Good-Friday-cum-Easter mass last weekend, Archbishop Josaphat Louis Lebulu of the Catholic Archdiocese in Arusha adds that many gullible people were falling prey to daily mushrooming 'money hungry' prayer groups and congregations whose leaders charge premium for imaginary miracles.
"And these fake preachers have been doing good business getting wealthier even as their victims continue to suffer in poverty," he said.
The Archbishop was speaking on behalf of other clerics while delivering a sermon at a communal mass involving all the mainstream Christendom denominations in Arusha to mark this year's Easter season.
Evangelical Lutheran Church Bishop Thomas Laizer added that it was abominable to charge fees in order to pray for somebody or set specific amount of money for people to bring as offering as many new-age preachers are currently doing.
The Chairman for the Union of Christian denominations in Arusha, Pastor Mathias Mushi warned that the church and Christianity have become extremely commercialized and focused on materialism such that the related 'faith-based' money making schemes seem normal.
The clergy here are also not quite sure of the recent trend of 'Choir' or 'Gospel' concerts whose organizers are enriching themselves by charging high entrance fees camouflaged as 'contributions to the work of 'God!'
In a separate interview Pastor Andrew Mollel of Philadelphia church in Sekei area said it was clearly indicated in the Bible that during 'end times' many fake preachers will emerge.
"Right now in Arusha there are some 'priests' who peddle 'miracle water' which they claim can cure all ailments under the sun including bad marriages," he said.

Source Arusha times
 
Makanisa yamevamiwa na kibaya kondoo wanaokamuliwa wengi wao ni masikini na wenye matatizo kibao....Ni kweli ukitaka kutoka kimbilia ubunge ama anzisha kanisa.
 
nabaki kujisemea kila siku huyu Yesu siku hiz kageuzwa biashara

kweli Mungu anahuruma na siku yaja anyway.......

Msama anatudanganya ati ''njoni watoto wa Mungu tukamwimbie bwana'.
....................my foot!!
 
Nakumbuka Mzee wa Upako kwenye channel Ten alikuwa anatangaza bila aibu kwamba weka fedha kwenye account yake binafsi ili akuombee.
 
Nakumbuka Mzee wa Upako kwenye channel Ten alikuwa anatangaza bila aibu kwamba weka fedha kwenye account yake binafsi ili akuombee.
mi mtu kama mzee wa upako hawezi kuniibia!wasio na macho ya kiroho ndio wataibiwa,biblia imeshasema MTAWAJUA KWA MATENDO YAO sasa kipi kigumu kugundua jinsi yule baba alivyo muongo,mi namwitaga mzee wa riwaya na tungo,yaani ana hadithi za uongoo,mara utasikia nilienda salon kinyozi kushika kichwa changu akapigwa shoti akadondoka,mara utasikia lete fungu la kumi ktk bahasha unikabithi mwenyewe halafu nikutizame machoni ili upako ukuingie,mara aah ..acheni tu jamani,nilikuwa nasali pale basi kila akijaribu kunidondosha sidondoki.
halafu na yeye kaja na strategy ya kudai eti kafufua misukule 70 ili kujiongezea customerz.mi nakwambieni kuliko kugawa pesa zangu kwa wajasiriamali wenzagu hawa nitachanga pesa zangu nisomeshe mtoto yatima na mungu wa mbinguni atapokea dhaka na sadaka yangu.lkn hawa ni noooo.ila mzee wa upako anajua kweli biblia na kufundisha neno,tatizo lake ni urongo mwingiiii.msanii tu.
 
na chakusikitisha sikuhizi hata mtu ambaye hajaisomea Bible anaweza kuwa na wanayoita ministry yake, na kujikusanyia waumini kibao, wengi wanatumia khali ngumu ya maisha inayokabili watu wengi kama advantage olewenu kwani yoote mnayofanya lazima mtaenda kuyajibu mbele ya haki.

kuna wanaowambia waumini kama wnataka kuombewa mpaka watoe kiasi fulani cha pesa, mbona Yesu hakuwahi wambia watu watoe pesa kama kigezo cha kuwaombea???????? umefika wakati muafaka sasa haya makanisa yawe yanafanyiwa ukaguzi na kodi hata Yesu alilipa kodi
 
Siku zote mtanaswa:
1. Nyie msiosoma biblia na kuelewa mapenzi ya Mungu ni nini kwenu.
2. Msioenenda kwa Roho. Maana kila upepo wa elimu uwateka nyara na msione muujiza hapo fahamu zenu za kiroho upeperuka kabisa.

Walio na masikio ya kiroho hao watapona.
Na wale wanaoliangalia neno na kulishika hao watapona na mitego hii. Mwenye masikio na asikie.
 
mi mtu kama mzee wa upako hawezi kuniibia!wasio na macho ya kiroho ndio wataibiwa,biblia imeshasema MTAWAJUA KWA MATENDO YAO sasa kipi kigumu kugundua jinsi yule baba alivyo muongo,mi namwitaga mzee wa riwaya na tungo,yaani ana hadithi za uongoo,mara utasikia nilienda salon kinyozi kushika kichwa changu akapigwa shoti akadondoka,mara utasikia lete fungu la kumi ktk bahasha unikabithi mwenyewe halafu nikutizame machoni ili upako ukuingie,mara aah ..acheni tu jamani,nilikuwa nasali pale basi kila akijaribu kunidondosha sidondoki.
halafu na yeye kaja na strategy ya kudai eti kafufua misukule 70 ili kujiongezea customerz.mi nakwambieni kuliko kugawa pesa zangu kwa wajasiriamali wenzagu hawa nitachanga pesa zangu nisomeshe mtoto yatima na mungu wa mbinguni atapokea dhaka na sadaka yangu.lkn hawa ni noooo.ila mzee wa upako anajua kweli biblia na kufundisha neno,tatizo lake ni urongo mwingiiii.msanii tu.

Cha kusikitisha pia licha ya kuwaibia kondoo waom kama anavyofanya Mzee wa Upako. Pia huwatongoza wa kina mama wanaoabudu kwenye makanisa yao tena wake za watu gia ya kujifanya kuwa wanajua matatizo yaliomo kwenye ndoa zao. Utakuta anamfuata mke wa mtu na kumwabia kuwa nimefunuliwa na BWANA kuwa una matatizo kwenye ndoa yako. Mama akikataa anamwambia kuwa mimi najua una matatizo, jifikirie uniambie ili nikuombee. Na mama akishasikia hivyo anaamini kabisa na kumwona huyo Mchungaji kama Mwokozi wake. Mwisho wa siku ni kuanza kumegana. Makanis haya feki mkeo akijiunga tu umeliwa.
 
Manabii wa uongo katika siku za mwisho ni kweli watakuwepo na hilo halikwepeki kwani roho ya mpinga kristo (ant-christ) inafanya kazi hivi sasa. Lakini jamani huwezi kuabudu bila kutoa sadaka na zaka - kwani utoaji ni sehemu ya ibada.
Michango mingine ni kuujenga ufalme wa Mungu - michango lazima itumike kufanya mambo mbali mbali - e.g. kupanua kanisa; au kusaidia yatima; au kusaidia wenye shida kanisani; etc. Pia katika jengo la ibada kuna expenses - kama kulipia umeme, maji, na huyu mtumishi aweze kuishi - asomeshe watoto etc.
Tunapokuja kwenye issue ya maombi - Mungu amesema MMEPEWA BURE TOENI BURE - hapo hakuna malipo otherwise ndio utajua huyo anayekuombea ana agenda ingine.
- Hivi tunajua kuwa unapotoa kiingilio kwenye jumba la starehe (dansi, ulevi...) unaujenga ufalme wa shetani?? unaweza kuona kuwa unakwenda kujipa starehe ila ukweli ni kuujenga ufalme wa shetani.
- Heri mtu anayemhubiri YESU ale hela yako kuliko mtu anaye mwinua SHETANI
Great Thinkers - Think Deeply
 
Jamani Efatha waumini walitangaziwa wapeleke sadaka mshahara wao wote...na pale efatha kama wewe ni mtoaji mzuri wa sadaka unatangazwa utoke mbele ya waumini uombewe zaidi! hii ilinisikitisha sana tuwe makini na upcoming church tunapotea na kutekwa akili...
 
Prodigal Son,,

Je ni kweli bado we ni mtoto mpotevu? Unahitaji ukweli...

Kwanza Maaskofu Josephat Lebulu ( Roman Catholic ) + Thomas Laizer ( KKKT), wazi walikuwa wanachangia mada kwenye mkutano wa ndani...

Je huyu mwandishi aliyefanya kuwa news kubwa .. je yeye na mhariri wake waliona hiyo ni news... Waongo wapo, wenye dhambi wapo kila mahala... Hata Yesu alikuwa na Yuda ambaye ni msaliti na alikuwa anakwapua kwenye kapu la sadaka.. Je Yuda aliweza kuzuia huduma ya Yesu isiendelee? Hakuna.

Kuwepo na manabii wa uongo na wenye kupenda fedha , Yesu mwenyewe alishaliongelea na kuliweka bayana na alitoa njia ya kupambana nayo.. kwa hiyo hilo si tatizo hata kidogo.

Tatizo lililopo si la wachungaji au manabii wa uongo, bali ni utitiri wa wauumini wasiotaka kujifunza na kuijua kweli, Neno la Mungu katika Yoh. 8:32- Mtaijua kweli na kweli itawaweka huru.... ( Wauumini) wengi ni wachanga kiroho na wasiopenda kujifunza lolote, hivyo ni wepesi kudanganywa, endapo hutaki kudanganyika inabidi uujue ukweli, na ukweli upo kwenye kujifunza neno la Mungu.

Sasa basi endapo mtu anakubali kudanganywa kirahisi kwa sababu ya uvivu wa kutotaka kujua neno hilo ni shauri lake mwenyewe... Lakini hata hivyo ukumbuke Yesu atakuuliza maswali magumu na hukumu yake ipo ya kutotembea na ukweli... Kuna gharama ya kulipia hapa duniani na hata kwenye kiti cha hukumu.

Prodigal son, wewe naye unashiriki katika kusambaza habari ambayo si ukweli kwa ujumla wake..... Si kweli kwamba kuanzisha kanisa ni mradi wa kupata hela!!! Huduma za watumishi wa kweli walioitwa na Mungu wapo.. Kama Bw. Yesu alisema mtawatambua kwa matendo yao , ya nini kuanzisha thread ambayo haina kipya ??? Je umeshindwa kuwatambua ?? Usiungane na hao maaskofu ambao nia yao kubwa ni kupinga uanzishwaji wa makanisa mapya kwani yanachangia kupunguza idadi wa wauumini katika hayo makanisa kongwe. Bila ya haya makanisa mapya mimi na wengine wengi tusingejua kweli tunazojua hivi sasa, ambazo ni nyingi tu. Nilidumu katika makanisa hayo na ukweli huo sikuupata, ashurukiriwe Mungu ambaye aliahidi kwa neno lake injili ya kweli itahubiriwa kwa kila kiumbe. Kaa tayari upokee na utafute injili ya kweli. Ngoja nitoe baadhi ya kweli chache , kuwa na nguvu juu ya magonjwa, kushinda nguvu za uchawi na ushirikina, hakikisho la kuwa na uzao wa tumbo na mali ... haleluya zipo nyingi...

Makanisa mapya yataanzishwa na kama yanaweza kuvuta watu basi ni dhahiri kuna ukweli unaoelezwa. Kashfa za mchungaji mmoja mmoja haziamaanishi makanisa yote mapya hayafai, mbona hiyo Roman ( wana matatizo ya makasisi kuwafanyia watoto vitendo vibaya?) Hata hapa Tanzania Padri Kimaro .... KKKT wana matatizo ya kuunga ndoa za kishoga huko Ulaya na hata imekuwa tatizo Uganda ? Hadi Dr. Malasusa kutoa tamko hapa Tanzania... Je tuyakatae makanisa ya Roman na KKKT kwa ajili ya mifano hiyo michache???
 
Haya, nimesoma na mimi nimeona ni-comment kidogo.
Biashara: Kama kweli lenngo ni kumtolea Mungu, basi wasiweke Account No. zao kwenye screen wakati wa vipindi vyao hapo Chaneel Ten, ATN na kwingineko, pili, Account hizo ziwe accessible na waumini wote wepewe mchanganuo wa mapato, matumiz na makadirio na kuwepo na Auditing kama CCT-Chaplaincy ya Chuo fulani.

Uzinzi na wake za watu; Kama utaangalia fasta fasta kwenye HOLY BIBLE ambayo ndiyo ninayoiamini, utanona kuwa mara zote MUNGU aliadhibu dunia, Taifa, Utawala au ukoo na kabila fulani kwa dhambi ya UZINZI, mfano wa wazi na unaojulikana na wengi ni ule wa SODOMA NA GOMORA pale wanaume walipogeuzana lakini pia kamwangalie HOSEA aliyeambia akoe KAHABA na kafanyiwa vituko na huyo kahaba lengo likiwa ni kuonyesha ni kwa kiasi gani MUNGU anachukizwa na mambo haya.

UKIONA CHUKIZO LA UHARIBU limesimama patakatifu ujue ule mwisho....
Hawa wanaotumia madhabahu ili kuwanasa wake na mabinti za watu watakuaje mbele za MUNGU?

USHAURI kwa mama na dada zangu ambao siku zote wamekua mstari wa mbele kutaka kuombewa wakijifanya wana matatizo mengi kuliko wengine ni Kwamba; WAKATAFAKARI MAANA NA IMPLICATION YA PAZIA LA HEKALU KUCHANIKA MARA MBILI au kwa kuwasaidia ni kwamba, Wewe sasa waweza kuongea na kueleza matatizo na shida zako kwa MUNGU na si lazima hata mambo yako ya sirini umwambia huyo unayemwamini kuwa na UPAKO na ...

Ni kweli, ukitaka kuwa tajiri fasta anzisha kanisa lakin ujue si la ROHONI bali ni HEKALU la Wanyang'anyi na ole wako, kanisa gani mmenunua malefu ya ekari, benki, television, na mnataka na viwanda...mtu akiipenda pesa pesa basi ujue kumpenda MUNGU khakupo ndani yake. Na ma-HAMMER yenu hayo na Ma-Benzi yatawaangamiza tu.

Shemdodo original
 
Nasali kwenye Kanisa la Mchungaji TiTO, divai ni safari larger kwa wakubwa na watoto
 
kanisa gani mmenunua malefu ya ekari, benki, television, na mnataka na viwanda...mtu akiipenda pesa pesa basi ujue kumpenda MUNGU khakupo ndani yake.

Shemdodo original

Shemdodo

Hakuna ubaya wowote wa kanisa kumiliki ardhi...... Je wajua kwa taarifa yako. Roman Catholic is a richest estate owner in the world???? Kuwa na television, radio, benki ni mambo ya kawaida. Huduma nyingi zilizo na waaumini wengi wanahitaji kuwa na masuala ya benki ili kuweza kumiliki na kusimamia mambo yao vizuri.

Makanisa ni huduma na inabidi iendeshwe kibiashara kabisa , kwani ipo mistaari ya biblia kuzungumzia hilo. Kwani Mungu si wa hasara... Endapo yote hayo yamelenga kuhubiri injili ya Kikristo.

Utaona huduma zinahitaji television, radio na hata viwanda mfano vya uchapaji kwa ajili ya kuendeleza injili na mwisho ukumbuke kuwa uchumi wa dunia unahitaji kumilikiwa na kanisa la wanaomuabudu Mungu kwa roho na kweli . Chochote kinachojiinua iwe huduma feki au watu kitashushwa tu.
 
Ukisikia watu wanapigia kelele makanisa kumiliki ardhi, benki, tv, radio, majengo makubwa, na kadhalika wakati dhehebu lake wanamiliki na haulizi unaweza kujua jinsi watoa hoja wengine hapa wanavyotakiwa kufunga mdomo na kunyamaza kimya kwa hoja zao dhaifu.
Newazz asante sana kwa maelezo yako mazuri. Nimeshindwa kukuwekea thanks bila kuisema kwa kinywa changu. lol
Kama nilivyotangulia kusema, kamwe mtego uko kwa wasiolijua neno la Mungu maana hapa mmeshikwa, mtadanganywa kwa kila elimu hata shetani atawadanganya kama Prodigal son anavyotumika kusambaza habari za shetani.
Someni biblia na tembeeni katika Roho mtashinda kila mtego. Si hivyo mtapigwa chini.
 
for sure wewe umetumwa na ibilisi. Not only kumiliki ardhi and utajiri, the church has all the economic, politica and social rights to control the state
 
Back
Top Bottom