nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
04 APRIL 2012
SEKRETARIETI ya Tanzania Labour Party (TLP) imemchagua Bw. Micah Mrindoko, kuwa mgombea ubunge wa Afrika Masharika.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juzi , Mwenyekiti wa TLP, Bw. Agustino Mrema, alisema kuwa chama chao kisimamisha wagombea watatu na kura zao kwenye Bw. Enock Mugae (0), Bw. Mutamwega (1) na Bw. Micah Mrindoko (4).
Alisema watu hao walichaguliwa na Sekretarieti ya watu sita na ambayo iliona Bw. Mrindoko ndiye anafaa kugombea nafasi hiyo.
"Ni vizuri kumchagua mtu anayefaa hata kwa jamii ndiyo maana sekretarieti ya chama chetu imeamua kumchagua, Bw. Mrindoko kuwa mgombea ubunge wa Afrika Mashariki,"alisema, Bw. Mrema.
Aliongeza kuwa nafasi hiyo ni muhimu hivyo ni vizuri kumuomba Mungu mgombea wa chama hicho apite kwenye kinyang'anyiro hicho.
Vyama vya upinzani vinatakiwa kuwa na mbunge mmoja wa bunge hilo, huku CCM ikiwa na nafasi 8.