Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Tangu kuibuka kwa wimbi la mkaguzi wa mahesabu ya serikali kuanika hadharani uvujaji wa pesa za umma serikalini, hali iliyosababisha wabunge kuivimbishia mishipa serikali wakiongozwa na wabunge wa upinzani kinara akiwa Zito kabwe, ambaye amezua mtafaruku mkubwa ndani ya CCM kwa kuanzisha mchakacho wa kukusanya sahihi za wabunge wasiopungua sabini ikiwa ni asilimia 20 ya wabunge kujenga hoja ya kupiga kura ya siri ya kutokuwa na imani na Waziri mkuu, kwa lengo la kushinikiza mabadiliko ya baraza la mawaziri kumechafuka vibaya ndani ya CCM.
Pamoja na ajenda ya kujadili na kuridhia mabadiliko ya baraza la mawaziri, CCM imeonja joto la jiwe kwa wimbi kubwa ambalo limetikisa si umoja wa vijana tu, ila hata vikongwe ambao walikuwa damudamu na CCM kuanza kuikimbia Jembe na nyumba na kujiunga na Chadema.
Ajenda kuu ya Kamati Kuu ya CCM ilikuwa kujadili hali ya kukimbiwa na wanachama ambayo imekuwa ni ajenda ya siri, na hii ya kuridhia hoja ya wabunge kushinikiza mabadiliko ya baraza la mawasili ni kuridhia kwa ajili ya kujinasua na mtego wa kukimbiwa na wanachama wake.