TIGOSMS mbona wanajishembendua...

Watu8

Platinum Member
Feb 19, 2010
70,499
92,317
Zifuatazo ni baadhi tu ya SMS zinazokera kweli kutoka TIGO, hivi ni lazima kutumiana SMS kama hizi, binafsi huwa nakereka kwa kuwa unaweza fikiria imeingia SMS ya maana....

"Jipatie dondoo za jinsi ya kupunguza uzito wa mwili na kubaki mwenye afya njema, tuma UZITO kwenda 15519, Pata dondoo hizi siku 5 BURE kisha Sh 125/SMS"

"Kucheka ni dawa isiyo na gharama yoyote,tuma KICHEKESHO kwenda 15519 na upokee vichekesho murua kwenye simu yako kila siku. BURE siku 5 kisha Sh 95/SMS"

"Pata dondoo za afya njema na epukana na magonjwa yatokanayo na afya dhoofu, tuma AFYA kwenda 15519.Utapokea kila siku dondoo za afya bora kwa TZS 125/SMS"
 
si uzifute ukishaziapta?

SI tatizo lake si kuzifuta , shida hapo hua wote hututokea!
Mf. Mie ninaetumia Mob. Hua nakatwa pesa mara tu nikingia ktk Internet, ukitoka ukirejea unaliwa tena.
Sasa while umo mtandaoni unaona msg ime'deliver unajua huenda msg ya issue ya haraka! Inakutoa online unakuta ndiyo "huo upumbavu wa msg za kampuni "
inaudhi si haba !
 
si uzifute ukishaziapta?

mkuu ishu sio kuendelea kuka kwenye simu...ila ni kwa nini tutumiane meseji ambazo mimi sijaomba hiyo hutuma, wakati mwingi unaweza ukadhani ni ujumbe muhimu umeingia kwa kuwa ulikuwa unasubiria sms ya biashara n.k...
Binafsi nimeshawahi kuishi nje ya Tanzania, nakumbuka hizi huduma mtu kama unazihitaji huwa unaomba wakati unanua kadi ya simu. Kampuni huwa inakupa menu ya vitu unahitaji na ambavyo huitaji...hizi huwa zinaitwa Huduma za ziada
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom