TID Atoka Kifungoni kwa Msamaha wa Rais

Mlalahoi

JF-Expert Member
Aug 31, 2006
2,182
883
Tanzania Daima,Jumatano 10,2008
MSANII wa muziki wa kizazi nchini Khalid Mohammed ‘maarufu kama TID' aliyekuwa akitumikia kifungo cha mwaka mmoja katika gereza la Segerea, jana aliachiwa huru kupitia msamaha kwa wafungwa uliotolewa na Rais Kikwete katika maadhimisho ya miaka 47 ya Uhuru.

TID ambaye Julai 23, mwaka huu alihukumiwa katika mahakama ya Kinondoni kutokana na kujeruhi, alikuwa ni mmoja ya wafungwa 4,306, walionufaika na msamaha huo ambao ni kwa mujibu wa Ibara ya 45 (1) (d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrance Masha, ana imani wafungwa watakaoachiliwa watarejea tena katika jamii kushirikiana na wenzao katika ujenzi wa taifa na watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani.

Kutokana na kuachiwa huru huko kwa TID, mashabiki wa msanii huyo jana walikuwa katika furaha za aina yake kwa kupita katika maeneo ya Kinondoni yalipo makazi ya msanii kuyo na kushangilia huku baadhi yao wakiwa wamevua mashati.

TID alirejea nyumbani kwake akiwa ndani ya gari aina ya Pajero, akisindikizwa na magari kadhaa alionekana ni mpole na mtulivu tofauti na alivyozoeleka kabla ya kukumbwa na kifungo hicho.
Ni matumizi mazuri ya msamaha wa Rais kwa wafungwa wenye tabia nzuri au Masha kapata kitu cha kumpa ujiko?
 
Ni matumizi mazuri ya msamaha wa Rais kwa wafungwa wenye tabia nzuri au Masha kapata kitu cha kumpa ujiko?

Kwani Masha ni member wa Parole Board? May be it is just a mere coincidence...I give him(Masha) a benefit of doubt on this matter unless proved otherwise.

Shadow
 
At least atakuwa na adabu kwa kila raia, kama tulivyofundishwa tangu utotoni!

karibu mzee, wa kukupigia zeze sijui bado yupo, au kaota mbawa!
 
Haya TID uache kutishia wazee na vijana wenzako kuwa utawavutia bangi.Hope kifungo hicho kimekufundisha. Nasubiri utoke na single ukielezea kwa masikitiko maisha ya jela
 
Karibu tenaa uraiani kama ambavyo nilitabiri kuwa atatoka kwa msamaha wa rais dec.....ni kwelii....
 
Karibu tena uraiani TID we hope umapata fundisho la kutosha....... Kaza buti sasa zingatia mziki kama umeamua kuwa ndio ajira yako.
 
Wafungwa kupata msamaha wa JK
Wafungwa wapatao 4,306 waliweza kupatiwa msamaha kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete, kwenye maadhimisho ya miaka 4 ya uhuru wa Tanganyika.

JK aliweza kutoa msahama huo kwa kutumia madaraka aliyopewa kikatiba, ya katika ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Msamaha huo ulitolewa kwa wale wafungwa wenye kifungo kisichozidi miaka mitano, ambao mpaka jana walikuwa wametumikia robo ya vifungo vyao.

Wengine walioangukiwa na msamaha huo ni wale wenye ugonjwa wa Ukimwi, Kifua Kikuu na Saratani, waliokuwa kwenye hatua ya mwisho.

Pia msamaha huo uliweza kupita kwa wale wafungwa waliokuwa na umri wa miaka 70 na zaidi, wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani na wale walioingia na watoto wachanga wanaonyonya, pamoja na wenye ulemavu wa mwili na akili.

Kwani wafungwa wote hao waliobahatika kupata msamaha wa JK ni wale wenye matatizo ya kiafya, waliweza kuthibitishwa afya zao na jopo zima la waganga.
 
hope kapunguza kuvuta mibangi yake iliyokua ina mfanya anajiona yu on top of everythin n everyone pale dar...

na pia tuombe tu huko jela asije kuta alikua under wajanja bin ma baunsa waliomzidi
 
Huyu jamaa nafikiri atakuwa amepata funzo japo mimi naona bado hakuwa ametumikia vya kutosha kwani kuna watu wengine wasiojulikana ambao wanatumikia vifungo mpaka mwisho kwa makosa ya kuku na vitu vingine vidogo. Au kusamehewa nayo ni kama bahati nasibu yaani bahati? Maana ilitakiwa kuwa na utaratibu fulani unaojulikana kama nchi nyingine na magazeti ya huko ukisoma yanaongelea lakini hapa mhh...

Au mwana kikundi maana viongozi wetu ni watu wakujirusha...
 
Akikutwa na hatia atapewa tena msamaha wa Rais?
 
Kwani Masha ni member wa Parole Board? May be it is just a mere coincidence...I give him(Masha) a benefit of doubt on this matter unless proved otherwise.

Shadow

At least atakuwa na adabu kwa kila raia, kama tulivyofundishwa tangu utotoni!

karibu mzee, wa kukupigia zeze sijui bado yupo, au kaota mbawa!

Haya TID uache kutishia wazee na vijana wenzako kuwa utawavutia bangi.Hope kifungo hicho kimekufundisha. Nasubiri utoke na single ukielezea kwa masikitiko maisha ya jela

Karibu tenaa uraiani kama ambavyo nilitabiri kuwa atatoka kwa msamaha wa rais dec.....ni kwelii....

Karibu tena uraiani TID we hope umapata fundisho la kutosha....... Kaza buti sasa zingatia mziki kama umeamua kuwa ndio ajira yako.

ohhh afadhali TID ametoka

Huyu jamaa nafikiri atakuwa amepata funzo japo mimi naona bado hakuwa ametumikia vya kutosha kwani kuna watu wengine wasiojulikana ambao wanatumikia vifungo mpaka mwisho kwa makosa ya kuku na vitu vingine vidogo. Au kusamehewa nayo ni kama bahati nasibu yaani bahati? Maana ilitakiwa kuwa na utaratibu fulani unaojulikana kama nchi nyingine na magazeti ya huko ukisoma yanaongelea lakini hapa mhh...

Au mwana kikundi maana viongozi wetu ni watu wakujirusha...

Kama habari za kumpiga mpenziwe ni za kweli akikutwa na akikutwa na hatia atapewa tena msamaha wa Rais?
 
hope kapunguza kuvuta mibangi yake iliyokua ina mfanya anajiona yu on top of everythin n everyone pale dar...

na pia tuombe tu huko jela asije kuta alikua under wajanja bin ma baunsa waliomzidi
Sasa hivi kahamia kwenye unga
 
Back
Top Bottom