Mlalahoi
JF-Expert Member
- Aug 31, 2006
- 2,182
- 883
Tanzania Daima,Jumatano 10,2008
Ni matumizi mazuri ya msamaha wa Rais kwa wafungwa wenye tabia nzuri au Masha kapata kitu cha kumpa ujiko?MSANII wa muziki wa kizazi nchini Khalid Mohammed ‘maarufu kama TID' aliyekuwa akitumikia kifungo cha mwaka mmoja katika gereza la Segerea, jana aliachiwa huru kupitia msamaha kwa wafungwa uliotolewa na Rais Kikwete katika maadhimisho ya miaka 47 ya Uhuru.
TID ambaye Julai 23, mwaka huu alihukumiwa katika mahakama ya Kinondoni kutokana na kujeruhi, alikuwa ni mmoja ya wafungwa 4,306, walionufaika na msamaha huo ambao ni kwa mujibu wa Ibara ya 45 (1) (d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa mujibu wa Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrance Masha, ana imani wafungwa watakaoachiliwa watarejea tena katika jamii kushirikiana na wenzao katika ujenzi wa taifa na watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani.
Kutokana na kuachiwa huru huko kwa TID, mashabiki wa msanii huyo jana walikuwa katika furaha za aina yake kwa kupita katika maeneo ya Kinondoni yalipo makazi ya msanii kuyo na kushangilia huku baadhi yao wakiwa wamevua mashati.
TID alirejea nyumbani kwake akiwa ndani ya gari aina ya Pajero, akisindikizwa na magari kadhaa alionekana ni mpole na mtulivu tofauti na alivyozoeleka kabla ya kukumbwa na kifungo hicho.