Thread za Babu Loliondo

wanaJF nimewamiss sana

nimerudi safari ya kwenda kupata kikombe cha dawa kwa Babu anawasalimu sana nilipata angalau muda wa kuuliza swali
dawa inatibu magonjwa yote kama utakuwa na imani na pia wakati unakunywa unaweka ombi kwa ugonjwa unaokusumbua.

Safari ilikuwa nzuri na niliifurahia sana isipokuwa barabara mmmmmmmmmmmh

Napenda kusema kwamba tofauti na kwenda kwa Babu niliweza kufanya utalii wa ndani nimeweza kuona ziwa Natron likiwa limezungukwa na Flamingo pamoja na magadi nimeweza kuchukua na kuja nayo huku, pia nimeweza kuona Twiga, Pundamilia na zaidi niliweza kuona mlima wa OldonyoLengai kwa karibu nafikiri tunaukumbuka huu Mlima.

Maisha niliyoyakuta kule niliyafananisha na kile kipindi kilikuwa kikirusha na TBC1 kilikuwa kinaitwa MAISHA PLUS watu walikwenda Loliondo na majiko ya gesi, na wengine walitumia kuni zilizokuwepo pale pamoja na vyombo vya kupika na vyakula. Walikuwa wanakwenda kuchota maji mtoni wanapika kuosha vyombo na mambo mengine mabalimbali ilikuwa kama Picnic.

kwa sasa wingi wa watu umepungua kiasi
kwa yeyote anayetaka kwenda asiwe na wasiwasi wa foleni kubwa



 
Ni kweli hapa sio mahali pake kabisa. Mi mwaka jana mwishoni nilienda kupata kikombe, wakati huo watu hawakuwa wengi kwa sababu babu alikuwa bado hajapata umaarufu ilivyo sasa. Sijapona kabisa ila nina nafuu kubwa ukilinganisha na mwanzo. Dawa yenyewe inahusisha mambo ya imani so kwa kauli ya babu ni kwamba kama una imani kubwa utaanza kupokea uponyaji mara moja. Kama imani yako haba utapona baada ya muda mrefu alisema inaweza kukuchukua hadi miezi mitano. Ila nina ushuhuda wa watu waliokuwa wanaumwa magonjwa mengine kama ya kisukari wamepona kabisa na wamehakikisha kwa vipimo hospitali.
 
wanaJF nimewamiss sana

nimerudi safari ya kwenda kupata kikombe cha dawa kwa Babu anawasalimu sana nilipata angalau muda wa kuuliza swali
dawa inatibu magonjwa yote kama utakuwa na imani na pia wakati unakunywa unaweka ombi kwa ugonjwa unaokusumbua.

Safari ilikuwa nzuri na niliifurahia sana isipokuwa barabara mmmmmmmmmmmh

Napenda kusema kwamba tofauti na kwenda kwa Babu niliweza kufanya utalii wa ndani nimeweza kuona ziwa Natron likiwa limezungukwa na Flamingo pamoja na magadi nimeweza kuchukua na kuja nayo huku, pia nimeweza kuona Twiga, Pundamilia na zaidi niliweza kuona mlima wa OldonyoLengai kwa karibu nafikiri tunaukumbuka huu Mlima.

Maisha niliyoyakuta kule niliyafananisha na kile kipindi kilikuwa kikirusha na TBC1 kilikuwa kinaitwa MAISHA PLUS watu walikwenda Loliondo na majiko ya gesi, na wengine walitumia kuni zilizokuwepo pale pamoja na vyombo vya kupika na vyakula. Walikuwa wanakwenda kuchota maji mtoni wanapika kuosha vyombo na mambo mengine mabalimbali ilikuwa kama Picnic.

kwa sasa wingi wa watu umepungua kiasi
kwa yeyote anayetaka kwenda asiwe na wasiwasi wa foleni kubwa

Blaki Woman nilivyokuwa na hamu na feedback yako ila FONT mama umenikwaza sana imebidi nikopi na kuweka kwenye word ndo nimeweza kusoma.

Hujatuambia dawa ikoje bana leta feedback ya nguvu
 
Hapo unanipa imani kuwa dawa ya babu ni kiboko ila pawepo na chembe ya imani. Hapo kwa imani itakuwa ni ngumu kwa wengi. Karibuni tuendelee kutoa shuhuda.
 
Blaki Woman nilivyokuwa na hamu na feedback yako ila FONT mama umenikwaza sana imebidi nikopi na kuweka kwenye word ndo nimeweza kusoma.

Hujatuambia dawa ikoje bana leta feedback ya nguvu

IKOJE KIVIPI DA
tamu au chungu
 
BW umeandikwa kweli kabisa, DaMie na Mdogo wangu Loveness love tulikuwa huko kwa muda wa wiki moja. tumeweza kuchukua magadi na kuona wanyama wa porini waliochanganyikana na ngomb'e za wenyeji wakila majani kwa pamoja Ilifurahisha sana. Mlima na majivu yake tumeona kwa ukaribu kabisa. foleni iliyopo pia kutafuna nyama za kuchoma na mihogo iliyokuwa inauzwa huko . Tumefanikiwa kunywa dawa na kupata marafiki wa kisonjo. Inapendeza kwa kweli.
 
Wapendwa,

Hizi thread mimi zimeanza kuniudhi sana zimekuwa nyiiiiiiiiiiiiiiiiiingiiiiiiiiiiiii

Ombi: Unganisheni maoni/salamu/ushuhuda kwenye thread zilizokwishwa anzishwa hii sasa imekuwa kero wajameni. AAkkkhhhhhh

Kama nitakuwa nimewakwaza poleni ila zimekuwa nyingi mno halafu ukingalia ni same issue haa kila mahala babu babu wajameni
 
Wapendwa,

Hizi thread mimi zimeanza kuniudhi sana zimekuwa nyiiiiiiiiiiiiiiiiiingiiiiiiiiiiiii

Ombi: Unganisheni maoni/salamu/ushuhuda kwenye thread zilizokwishwa anzishwa hii sasa imekuwa kero wajameni. AAkkkhhhhhh

Kama nitakuwa nimewakwaza poleni ila zimekuwa nyingi mno halafu ukingalia ni same issue haa kila mahala babu babu wajameni

Na mm nataka kwenda kunywa juice ya babu Loliondo nichangie nauli basi
 
Ruhusa yangu bado inasuasua, mwajiri bado hataki kuruhusu watu hapa kwetu. Ikibidi nitatoroka, liwalo na liwe.
 
Angekua anaruhusu kuagiza kwa sisi tusio na nauli bwana!!!
Nwyz asante kwa feedback BW!!
 
Ni kweli hapa sio mahali pake kabisa. Mi mwaka jana mwishoni nilienda kupata kikombe, wakati huo watu hawakuwa wengi kwa sababu babu alikuwa bado hajapata umaarufu ilivyo sasa. Sijapona kabisa ila nina nafuu kubwa ukilinganisha na mwanzo. Dawa yenyewe inahusisha mambo ya imani so kwa kauli ya babu ni kwamba kama una imani kubwa utaanza kupokea uponyaji mara moja. Kama imani yako haba utapona baada ya muda mrefu alisema inaweza kukuchukua hadi miezi mitano. Ila nina ushuhuda wa watu waliokuwa wanaumwa magonjwa mengine kama ya kisukari wamepona kabisa na wamehakikisha kwa vipimo hospitali.

Sawa kabisa unayoyasema J_N Imani ndio kila kitu hata ukipewa Panadol usipokuwa na imani hutapona kichwa kinachokuuma.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom