Kaa la Moto
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 7,903
- 1,053
Yahya asante sana kwa kuyatoa maoni yangu hewani. Bahati mbaya hayakupata michango sana tokana na kukatika kwa mawasiliano ya Dar. Lakini naona umedhamilia kusaidia katika kuyaunganisha mawazo ya watanzania juu ya msatakabali wa nchi yao. Na hakuna namna nyingine sasa mbali na nyinyi waandishi wa habari kutusaidia. Bahati mbaya tulidhani wawakilishi wetu (wabunge) wangebeba jukumu hili lakini badala yake wanapofika kule Dodoma wao upeleka mambo ambayo hatukuyachangia mawazo. Fikra zao wengi ni je nitarudije tena bungeni baada ya miaka mitano na malalamiko kuwa kuna watu wanawaingilia kwenye majimbo yao. Mungu akubariki sana. Tuendelee na tusiache kwa namna yoyote kushirikiana kuijenga na kuiendeleza nchi yetu.
Jambo moja la ziada bwana Yahya, ningeomba kama utaweza hizi video ya mada hizi ungeweza kuziweka hapa na kule Youtube ili wale wenzetu walio nje ya nchi wasioweza kuiona star tv wajue nini kimekuwa kikiendelea katika michango ya haya mambo na waweze kujua na kuyatolea maoni pia.
Jambo moja la ziada bwana Yahya, ningeomba kama utaweza hizi video ya mada hizi ungeweza kuziweka hapa na kule Youtube ili wale wenzetu walio nje ya nchi wasioweza kuiona star tv wajue nini kimekuwa kikiendelea katika michango ya haya mambo na waweze kujua na kuyatolea maoni pia.