This is Rostam I know... The Story Behind the Man

mzee utaona nawajibu vile wale wanaoanza kunishambulia...lakini pia (niliwahi kusema huko nyuma) kwenye lugha inaruhusiwa sarcasm, rhetorics n.k So, si kila wakati ni vibaya kutumia lugha ya kejeli pale inapotumiwa vizuri huongeza utamu wa hoja. Lengo ni kuonesha uduni wa hoja siyo uduni wa mtu.

ndiyo maana utaona siulizi motives za mtu anaponijibu kama wametumwa au wanalipwa.. nachukulia hoja zao tu. Simtukani mtu anayeshindana nami hata wale ambao wanatumia vibaya vitu hivyo isipokuwa pale ninapoamua tu kuwa fyatu for a second! (which does happen sometimes if i don't take my medication)..

Hamna haja ya kuuzidisha huu mjadala. Kwa kifupi, sikubaliani na wewe. Humu ndani nimeitwa ngumbalu, kilaza,n.k. nimetumwa na wala sikuwaona mkisema, "hapana hiyo sio lugha inayotumiwa hapa!" Sasa mnataka kugeuza ishu kuwa Fundi Mchundo anawafukuza wachangiaji kwa kuwa sarcastic? Nimetumiwa wapi sarcasm kuonyesha uduni wa mtu? Mara zote ninajaribu kuwa mvumilivu lakini ikibidi nitatumia sarcasm when necessary. Na nitafanya hivyo kwa makusudi kabisa ili kutoa ujumbe. Nadhani tumeelewana.

Amandla.......
 
Unajua... si kwamba hajasoma Oxford.. nadhani atakuwa amesoma huko lakini point yangu ni kuwa hakuwa anatokea Tanzania... on the other hand, kama hakusoma Oxford ali graduate wapi? Tovuti ya Bunge inasema yeye ni graduate wa Economics labda Mlimani ...

Tatizo credentials za viongozi wengi wa Tanzania huwaga hazielewi eleweki. Sasa tovuti ya chombo cha kutunga sheria kama bunge inaweka vitu nusu nusu kama hivyo sisi wananchi wa kawaida tuwachukulieje hao watunga sheria wetu?

Yaani hovyo hovyo na shagalabaghala tupu!!
 
Unajua... si kwamba hajasoma Oxford.. nadhani atakuwa amesoma huko lakini point yangu ni kuwa hakuwa anatokea Tanzania... on the other hand, kama hakusoma Oxford ali graduate wapi? Tovuti ya Bunge inasema yeye ni graduate wa Economics labda Mlimani ...

Mlimani mate zake wangeisha sema hapa, hata huko oxford lazima itaonyesha entry qualification ukisearch kwenye admission, lazima itaonyesha aliingia kutokea wapi?

Hata hivo ni kwa vile bongo sasa hivi ni usiku, kesho asubuhi wakiamka waungwana watamwaga yote! Pengine muanzisha mada hapo juu akipachika tangazo la mtu aliye soma na RA popote na katika level yoyote ile atupe data. am sure majibu yatapatikana, kama kweli alisoma chini ya mwembe 'Igunga shule ya msingi'
 
Hamna haja ya kuuzidisha huu mjadala. Kwa kifupi, sikubaliani na wewe. Humu ndani nimeitwa ngumbalu, kilaza,n.k. nimetumwa na wala sikuwaona mkisema, "hapana hiyo sio lugha inayotumiwa hapa!" Sasa mnataka kugeuza ishu kuwa Fundi Mchundo anawafukuza wachangiaji kwa kuwa sarcastic? Nimetumiwa wapi sarcasm kuonyesha uduni wa mtu? Mara zote ninajaribu kuwa mvumilivu lakini ikibidi nitatumia sarcasm when necessary. Na nitafanya hivyo kwa makusudi kabisa ili kutoa ujumbe. Nadhani tumeelewana.

Amandla.......

Babu mbona una jazba hivyo leo? Ni adha za kimaisha au ni ukali wa mijadala ya hapa JF?
 
Unajua... si kwamba hajasoma Oxford.. nadhani atakuwa amesoma huko lakini point yangu ni kuwa hakuwa anatokea Tanzania... on the other hand, kama hakusoma Oxford ali graduate wapi? Tovuti ya Bunge inasema yeye ni graduate wa Economics labda Mlimani ...

Niliingia Mlimani 1989 na nikaondoka 1993, hakukuwa na mtu mwenye jina la Rostam Aziz ama wa kufanana nae na kwa bahati nzuri nilisoma Uchumi huo huo, na watu wenye asili ya Kiarabu/Kihindi ilikuwa ni rahisi kuwafahamu wote. Kwa hiyo rule out Mlimani.
 
Mwanakijiji,

Mkuu wangu nadhani kuhusiana na Elimu ya Rostam na shule zipi kasoma sio issue hapa zaidi ya kutafuta ukweli unaohusiana na Ufisadi..

Binafsi nimesoma na Wahindi, wairan na Waarabu kibao, leo hii wengine wako Oman, UAE, US canada na UK na hawa watu wamezaliwa Tanzania huko Kibara sehemu ambazo huwezi kuamini na nina hakika kabisa nikiweka majina yao hapa wengi mtatoka kapa..

Nakumbuka udogo wangu nakua pale kibara kulikuwa na mzungu mmoja akiitwa John Walker (Welder) sijui kama hilo lilikuwa jina lake au la laa! lakini mkuu wangu mzungu yule amekulia pale na kafa kama Mtanzania.. amezikwa hapo Kibara na hakuna mtu hata mmoja aliyejali Uzungu au uraia wake kwa sababu ya rangi yake..

Mimi naona tunatoka ktk issue yenyewe na sababu hasa mnayowekea mashaka uraia wake ni kutokana na rangi yake.. nothing else.. wapo weusi kibao ambao sii wazawa na wanatuongoza.. Uhuru wetu wenyewe ulipatikana tokana na watu wengi wa kuja.. kina Kreist asili yao ni South Afrika lakini leo huwezi kuhoji Uhalali wa uraia wa wajukuu zake..

Binafsi naamini kabisa kutokana na lafidhi yake huyu Rostam bila shaka amezaliwa kama sio amekulia Tanzania, hivyo anaweza soma shule yoyote ile isipokuwa labda tunahoji nafasi yake ktk uongozi kulingana na Elimu yake. Maadam tumeambiwa kasoma Oxford basi na tuamini hivyo hadi pale itakapo kuja issue inayohusiana na elimu hiyo na sii Ufisadi..
Mambo yoote yataulizwa hakuna la kuachwa. Ni kwa nini hata kwenye historia yake katika website ya bunge hajaandika kitu? na huo ni ubaguzi? wote wanao mtetea hapa hakuna anayejua jamaa amesoma wapi zaidi ya Oxford. Kama anajua kuongea na kuita waandishi wa habari pale hotelini najua kama angekua hana la kuficha angetoa historia yake ili aonekane ni mbongo aliyezaliwa na kukulia au hata kama alisomea nje angesema tuu. Si anajua kuongea?
 
Kwa kuwa Ballali alishakufa, swali lako la yupi Fisadi kati ya Rostam na Ballali, mimi naona halina nafasi kwa sasa. Kama Ballali angekuwa bado yuko hai jibu langu kwa jumla lingekuwa ni moja kwamba Ballali na Rostam wote ni mafisadi na hayo yalikuwa yakisemwa hata kabla Ballali hajafa. Halafu kwenye hiyo orodha nitaongeza jina la Mkapa maana ndiye aliyemwagiza Gavana akatoe hela.

Kwa hiyo mtu yeyote muovu akifa ndiyo basi uovu wake unasafishwa? Kama hii habari hatuwezi kuepuka kumnyooshea mkono marehemu kuwa ndiye aliyetuingiza kote huku. Kututangulia kwake hakubadili ukweli huo!

Amandla.......
 
Prince William... tunaomba source... hapa sio vyema kusema mambo ambayo hatuwezi confirm. Na ukileta dataz zozote.. make sure unayo vielelezo.. JF sio sehemu ya soga....

Kama uliipata habari First Hand source yako ni nini?Ni Website, Gazeti, Bariua ya serikali au ni wewe mwenyewe.Uzuri wa Online ni mmoja.Panya akiweza Kuregister hapa JF naye ataingia na kutoa habariza za Chwiiiiiiiiiiiii!!!Vile vile mtu wa maana na wajikoni kabisa mwenye taarifa zote akiingia hapa hato kuwa tofauti na panya mwerevu alozmia JF. AI KEN NOT BILIVU ABOUTI ENESING, NEIZA AI WILI NOTI STOPU AGIUNG ANTILI YU GIVU ME KIZIBITI. KILI MI IFU YU WANTI I MNI ITI...................EHEE! BIFOO AI FOGETI, MISTA FILDI MASHO IZI ITI TRUU ZATI MUUNGWANA TOSADI ROSTAMU AT CC MITINGI ??? ACHA WEE!! HAU DIDI HI DU ITI WHAILI ZEI SEI ROSTAM HEZI OLL KONTRO OVA MUUNGWANA???
 

Why did Mkapa ordered the money to be given to Rostam? The Main answer is that he was strategically well positioned in Lake Zone right? Why Rostam?Secondly, You said Mpaka called Ballali to ask him to Give RA money to elect Kikwete, that means the Operations to steal money from BOT was planned and initiated by CCM Chairman for the Benefit of CCM? Which means RA was just an implementer


- Mkuu wangu again, hili suala la EPA mbona mnalikoroga sana bila ya kujua ukweli? Ukweli ni kwamba hii ilikuwa ni tabia ya CCM kuchukua hela toka Hazina na BOT toka awamu ya kwanza kwa ajili ya uchaguzi, inasemekana huko nyuma zilikua zikichukluliwa baada ya muda zinarudishwa, sijui kama ni kweli lakini kuna waziri wa serikali ya sasa aliyeniambia hayo,

- Kikao kimoja cha siri cha Mtandao, likubaliana wachukue shillingi billioni 31 tu zitatosha uchaguzi, lakini zikaishia kuchukuliwa bilioni 133, Rostam ndiye aliyekua mfadhili wa uchaguzi na kuzichukua zile hela ilitakiwa order ya rais Mkapa, kulikuwa na vikao vya awali mara kwa mara Ikulu, kati ya Rostam na Mkapa,

- Kama unakumbuka BCS, niliwahi kusema hivi Rostam alianza kuonekana sana Ikulu, na kukutana sana na Mkapa kule, siku moja Mangula alikuwa amekwenda Ikulu kumuona Mkapa, Rostam na Mangula walikua wanamsubiri Mkapa, alipoingia tu huku akiwa amewaona wote wawili pale, aliagiza Rostam aingie kwanza, to Mangula's shock, na alipoingia alikaa karibu masaaa mawili huku Mangula akiwa anasubiri, eventually Rostam alitoka ndipo Mangula akaingia, alipofika tu swali la kwanza alimuuliza Mkapa, kwamba amesikia minong'ong'ono sana kuhusu Mkapa na Rostam what is going on?, in which Mkapa alimjibu kwa ukali sana kwamba Rostam ni mbunge mweeye haki zote za kumuona wakati wowote ule,

- Ni wakati huu ndipo mstaafu wa idara naye akaanza kuonekana kwa siri na Rostam na Lowassa, kwa sababu alihitajika sana kuangalia the other way wakati hela zinachotwa BOT, he did, infact ndio kwa mara ya kwanza uadui wa Muungwana na mstaafu wa idara ukamalizwa maana kabla ya hii walikuwa hata hawaongei wanapitana tu! Sasa ndio kwa mara ya kwanza ikaanza kueleweka ni kwa nini Rostam aliwaajiri Ruhinda rafiki wa karibu wa Mkapa na Msekwa, kule Vodacom!

Mkuu I can go on and on, lakini the masterminder wa EPA na Kagoda alikua Rostam, Mkapa alikuwa anapewa orders tu what to do! Hizi hela zilikuja later on kutumiwa na Rostam kununua influence ya almost kila kiongozi wa CCM, lakini hazikuwa hela za CCM kama chama!

Respect.

FMEs!
 
Tatizo credentials za viongozi wengi wa Tanzania huwaga hazielewi eleweki. Sasa tovuti ya chombo cha kutunga sheria kama bunge inaweka vitu nusu nusu kama hivyo sisi wananchi wa kawaida tuwachukulieje hao watunga sheria wetu?

Yaani hovyo hovyo na shagalabaghala tupu!!

Wana siasa wengi ni wasanii, ni wachache sana ambao wameweka full details za background zao.

Mimi nilidhani kwamba kwenye fomu ya kuomba kugombea Ubunge wanatakiwa kujaza hizo taarifa zote na mtu akishinda Ubunge, fomu yake ama nakala ya fomu yake inapelekwa bungeni kwa ajili ya kumbukumbu na kuingiza details kwenye website na kwenye ma-file yao.

Kwanini watu kama hao huwa hawafanyiwi background check kwa ajili ya kuhakiki info walizo-provide?
 
- This is the fact on what happened in the past and is what continuing to happen!

Mkuu umeniacha nje hapo, what is the fact as far as you are concerned ya mtu kama mimi ku-support hoja za Mengi dhidi ya Rostam? Unasema ni wka sababu ya ukabila au rangi?

With all due respect, naomba ufafanuzi hapo mkuu kama unaweza!

FMES!

Sababu ya kimsingi ya RA kuwa game player wa Kikwete ni kwasababu anatokea kanda ya ziwa na si sababu nyingine.Ndio maana hata pesa za EPA alipewa yeye ,Mengi Anamchukia RA because he is more influencial near the power
 
Lusajo,

Mkuu wangu acha hizo.. Yaani ulitegemea Rostam ajieleze amezaliwa na kukulia wapi?..mbona Mengi hakufanya hivyo!.. ebu nambie wewe unajua Mengi amezaliwa, kakulia na kasoma wapi au ndio kwanza uta google!..

Na unapofanya hivyo unatafuta kitu gani kumjua Mengi ili iweje?..kuwa yeye anaweza kuwa msafi zaidi ya Rostam..Umeona kiongozi gani akiitisha waandishi wa habari hutanguliza historia yake kwanza.. hii sheria imetoka wapi!

Mkuu wangu tunachotafuta hapa ni kumjua Rostam Fisadi na kama alivyozungumzia mwanzilishi wa mada hii kachambua maafa yake kwa jamii yetu badala ya historia ya masiha yake..Hakuna mtu anayetaka kumchagua Rostam kugombea Urais hapa..

Na nimevutiwa na mada hii kwa sababu inanipa picha halisi ya nani Rostam kwa mapana ya Uchafu wake sio nani mzazi wake na ana asili gani..

Kuna watu wanasema Nyerere asili yake ni toka Rwanda sijui Burundi kuna mtu aliuliza kama alikwenda kuapishwa kuwa Mtanzania?..
 
- Mkuu leo asubuhi kuna mahali umeshambuliwa kwamba unatumwa, ukadai hutumwi na ukanitaja kama shahidi wako na kweli nikaweka ushuhdua wangu kwamba hutumwi ni mawazo yako tu kumtetea fisadi papa Rostam,

FMES!

Ushuhuda huo uliuweka wapi? Au ndiyo ile asante uliyonipa kwa mchango wangu? Kama ulipitiwa basi tafadhal, rudi kaandike loud and cleear kuwa ingawa Fundi Mchundo anamtetea fisadi papa Rostam, hajatumwa. Hayo ni mawazo yake tu. I am not holding my breath on this one.

Amandla........
 
Sababu ya kimsingi ya RA kuwa game player wa Kikwete ni kwasababu anatokea kanda ya ziwa na si sababu nyingine.Ndio maana hata pesa za EPA alipewa yeye ,Mengi Anamchukia RA because he is more influencial near the power

kwa hiyo rostam is a just a poor victim? ambaye amejikuta "at the wrong place, at a wwrong time)? Kwanini unafikiri RA ana influence kanda ya ziwa? Hiyo influence ilianzia lini kulinganisha na watu waliokuwa na nguvu maeneo hayo.. unless kama kuna ushahidi wowote kuwa familia yake ilikuwa na nguvu kanda hiyo.. kwa sababu siuoni kihistoria ushawishi wa Rostam au familia yake kabla ya 1995.. help me out.. you might be onto something.
 
Third MENGI and RA they are in same shoes they are both Mafisadis , Mengi through ITV he was a benefitery of EPA money, not only that Mengi kwa kupitia ITV he missleaded all Tanzania on how Good CCM was in returns he has access to all guarantees and loans na ndio maana MENGI anamwita RA fisadi na sio CCM because he still love CCM and what it does to him personally .


- Again haiko sawa hii mkuu, Mengi kama wa-Tanzania wengi wengine alikuwa anamiliki biashara inayoweza kutumika kisiasa yaani TV ambayo ukitaka unakipa na unarushiwa matangazo yako ya kisiasa, hiyo ni biasahara sio anything else wala rushwa, wananchi wengi walinufaika sana na hela hizo wenye biashara zinazoingiliana na kampeni za siasa.

- Na ninaomba kukusaidia zaidi ni kwamba Mengi hakuwahi hata siku moja kushirki kwenye vikao vya mtandao, alichokuwa akifanya kama ninavyojua mara kwa mara Mtandao walipokuwa wanahitaji hela walikuwa wanamtumia messenger, hasa el that is how alichangia Mtandao, WHy he did this? Simply kulinda bisahra zake, ninaamini kwa 100% pia alikua akisaidia upinzani pia, ndivyo wafanyabiashara wote walivyo, is it a crime in Tanzania kusaidia uchaguzi hell no!

- Mengi amemwita Rostam fisadi, baada ya Rostam kumuanza kwa kumtuma Makamba kwenda CC kumchafua Mengi na yeye akaamua kumjibu master wa Makamba, yaani Rostam, sasa chanzo cha haya malumbano ni rostam sio Mengi mkuu kwa hiyo hii hapo juu haijakaa sawa!

Respect!

FMES!

 
Ushuhuda huo uliuweka wapi? Au ndiyo ile asante uliyonipa kwa mchango wangu? Kama ulipitiwa basi tafadhal, rudi kaandike loud and cleear kuwa ingawa Fundi Mchundo anamtetea fisadi papa Rostam, hajatumwa. Hayo ni mawazo yake tu. I am not holding my breath on this one.

Amandla........

- Kukupa thanks yangu maana yake ni moja tu kwamba nina-approve message yako nilipokupa kwenye ile hoja yako ilikuwa na maana ya kukubali hoja yako kwamba hutumwi, sasa usiite wengine tena jina lile lile uliloliktaaa, eti wanatumwa au wakawaulize waliowatuma.

Ahsante.

FMES!
 
- Mkuu wangu again, hili suala la EPA mbona mnalikoroga sana bila ya kujua ukweli? Ukweli ni kwamba hii ilikuwa ni tabia ya CCM kuchukua hela toka Hazina na BOT toka awamu ya kwanza kwa ajili ya uchaguzi, inasemekana huko nyuma zilikua zikichukluliwa baada ya muda zinarudishwa, sijui kama ni kweli lakini kuna waziri wa serikali ya sasa aliyeniambia hayo,

- Kikao kimoja cha siri cha Mtandao, likubaliana wachukue shillingi billioni 31 tu zitatosha uchaguzi, lakini zikaishia kuchukuliwa bilioni 133, Rostam ndiye aliyekua mfadhili wa uchaguzi na kuzichukua zile hela ilitakiwa order ya rais Mkapa, kulikuwa na vikao vya awali mara kwa mara Ikulu, kati ya Rostam na Mkapa,

- Kama unakumbuka BCS, niliwahi kusema hivi Rostam alianza kuonekana sana Ikulu, na kukutana sana na Mkapa kule, siku moja Mangula alikuwa amekwenda Ikulu kumuona Mkapa, Rostam na Mangula walikua wanamsubiri Mkapa, alipoingia tu huku akiwa amewaona wote wawili pale, aliagiza Rostam aingie kwanza, to Mangula's shock, na alipoingia alikaa karibu masaaa mawili huku Mangula akiwa anasubiri, eventually Rostam alitoka ndipo Mangula akaingia, alipofika tu swali la kwanza alimuuliza Mkapa, kwamba amesikia minong'ong'ono sana kuhusu Mkapa na Rostam what is going on?, in which Mkapa alimjibu kwa ukali sana kwamba Rostam ni mbunge mweeye haki zote za kumuona wakati wowote ule,

- Ni wakati huu ndipo mstaafu wa idara naye akaanza kuonekana kwa siri na Rostam na Lowassa, kwa sababu alihitajika sana kuangalia the other way wakati hela zinachotwa BOT, he did, infact ndio kwa mara ya kwanza uadui wa Muungwana na mstaafu wa idara ukamalizwa maana kabla ya hii walikuwa hata hawaongei wanapitana tu! Sasa ndio kwa mara ya kwanza ikaanza kueleweka ni kwa nini Rostam aliwaajiri Ruhinda rafiki wa karibu wa Mkapa na Msekwa, kule Vodacom!

Mkuu I can go on and on, lakini the masterminder wa EPA na Kagoda alikua Rostam, Mkapa alikuwa anapewa orders tu what to do! Hizi hela zilikuja later on kutumiwa na Rostam kununua influence ya almost kila kiongozi wa CCM, lakini hazikuwa hela za CCM kama chama!

Respect.

FMEs!

Sasa ni vipi kila mtu ndani ya CCM ni kama vile anakubali kufa kibudu kwaajili ya Rostamu na Genge lake??Tulipokuwa Tosa High School enzi zile za Marehemu DUDU tulikuwa tukienda kuiba mahindi ya shule usiku Usiku na kyachemsha kwa Heater kisha kumpa mahindi kadhaa Kilanja Mkuu Kitwanga ili kuua So.Taabu ni pale akijaribu kusema neno kuhusu wizi wa mahindi unaofanywa na baadhi ya wanafunzi, hilo jicho tutakalo mkata mwenyewe inabidi awasingizie Ma local wa kule Msombwe kwamba ndio wezi.Nadhani Rostam alikula Nyama ya mtu akawalisha CC wote.
 
the masterminder wa EPA na Kagoda alikua Rostam, Mkapa alikuwa anapewa orders tu what to do! Hizi hela zilikuja later on kutumiwa na Rostam kununua influence ya almost kila kiongozi wa CCM, lakini hazikuwa hela za CCM kama chama!

Respect.

FMEs!

RA alikuwa hana uwezo nor power to give orders kwa Mkapa, RA alikuwa ana represent CCM katika hii game paln, Kwhiyo Mkapa alikuwa anatekeleza orders za wana CCM wenzake wanaojua mazambi yake.

Swala la Billion 133 Kuchukuliwa badala ya 31, Ukweli wake uko wazi. Kuna madeni ya Moja kwa Mojaa amabayo CCM ilkuwa ime incur before hata hawajamchagua mgombea wa Uraisi,

Magari CCM yalikuwa yanawekewewa mafuta Bure na Vituo Mbali mabli vya mafuta, E.g Oil Com, and Njake kule maeneo Ya Arusha, Which in return ndio unaona hadi kama kina njake wakawa katika Plot ya kuchota PESA za EPA,
Hebu leo nenda kamwulize mzee njake, kama ana furaha na kuingizwa kwake kwenye huu mtego.

Mwisho, Kwa wewe na wengine mnaozidi kupush kwamba RA ndie EPA ninawauliza maswali ya Msingi? Bila CCM kuweka Baraka za huu wizi RA angewezaje kuchota hizo pesa? Bila CCM na serikali yake kuweka baraka how is the Money Launderling due deligency didnt catch RA?
 
Lusajo,

Mkuu wangu acha hizo.. Yaani ulitegemea Rostam ajieleze amezaliwa na kukulia wapi?..mbona Mengi hakufanya hivyo!.. ebu nambie wewe unajua Mengi amezaliwa, kakulia na kasoma wapi au ndio kwanza uta google!..

Na unapofanya hivyo unatafuta kitu gani kumjua Mengi ili iweje?..kuwa yeye anaweza kuwa msafi zaidi ya Rostam..Umeona kiongozi gani akiitisha waandishi wa habari hutanguliza historia yake kwanza.. hii sheria imetoka wapi!

Mkuu wangu tunachotafuta hapa ni kumjua Rostam Fisadi na kama alivyozungumzia mwanzilishi wa mada hii kachambua maafa yake kwa jamii yetu badala ya historia ya masiha yake..Hakuna mtu anayetaka kumchagua Rostam kugombea Urais hapa..

Na nimevutiwa na mada hii kwa sababu inanipa picha halisi ya nani Rostam kwa mapana ya Uchafu wake sio nani mzazi wake na ana asili gani..

Kuna watu wanasema Nyerere asili yake ni toka Rwanda sijui Burundi kuna mtu aliuliza kama alikwenda kuapishwa kuwa Mtanzania?..
Kaka ni kweli sio lazima aseme, lakini kuna wakati ambapo unaona watu wanajiuliza kuhusu wewe unaweza ku-clarify once and for all kuhusu hilo suala ili watu wasione kwamba lina utata. Kuna watu wanaoongea kuhusu RA ndio wananichanganya kwa sababu kuna mtu alisema alikuwa wa kwanza darasa la saba, hawasemi ni wapi na ni shule gani? Mara nyingine hata kujua kazaliwa wapi ni muhimu anaweza akawa anaifisadi nchi kwa sababu haijalii na hana machungu nayo.
 
Back
Top Bottom