This is pathetic

Mkuu! Hata wapenda kunyonga wamarekani wamekubali kuwa mtu aliye chini ya miaka 16 hastahili kunyongwa hata akifanya nini! Huyu ni mtoto bado na si ajabu kwa akili zake alikuwa anaona ndiyo anaonyesha mapenzi kwa huyo jamaa. Nadhani kubaka nayo ni felony. Miaka 30 si mchezo katika jela zetu. Kwa upande ni sawa na hukumu ya kifo.

Habari inasema kwamba mlalamikaji anao umri wa miaka 16 (na siyo chini ya miaka 16 kama unavyodai). Huyo si mtoto tena kisheria kwenye majimbo yaliyo mengi zaidi (majority of states) kule Marekani, na penginepo hata Tanzania. Isitoshe, felonies zinatofautiana. Kubaka kamwe haiwezi kusababisha mtuhumiwa akapewa adhabu ya kifo, na adhabu ya kifo si sawa na kifungo cha miaka 30. Kama huyu msichana angefanikiwa kuwaua wenzake wawili kwa sumu aliyopewa na mwenyewe akapona, nadhani hata huko Marekani kwa vyovyote wangemnyonga tu, mitigating circumstances notwithstanding.
 
Hiyo kusema kweli sina uhakika kisheria ni umri gani (it appears to be either 16 or 18-years-old depending on which source you choose to go with). All the same, argument yangu n kwamba independent of age of consent, binadamu wa wastani wa miaka 16 anategemewa kuwa na moral judgement inayotosha kumfanya aelewe kwamba si sawa kukubali kupokea sumu na kuitumia kuondoa maisha yake binafsi na wenzake wawili wasiyo na hatia.

Ahsante, ni wazo zuri sana. Lakini, na naomba usishtuke, lakini Wamarekani wana msemo, "mawazo ya mtu ni kama matako maana kila mtu ana yake"!

Sheria inasemaje ?

Sheria ya umri wa kujiamulia kuolewa na hivyo kujamiwa na mumeo kihalali inahusika sana hapa. Huwezi kuliweka pembeni hilo, na ukasema binadamu wa miaka kadhaa anategemewa...Anategemewa na nani?

Nataka kusikia jamii inavyotegemea, kwa mujibu wa sheria. Halafu ndio tujadili mawazo yetu mimi na wewe, bila kujali mawazo ya jamii ya wanasheria.

Jamii yetu, kwa mujibu wa sheria, inamtegemea mwanamke kuwa mtu mzima wa kujiamulia kujamiwa na mumewe akiwa na umri gani?
 
Habari inasema kwamba mlalamikaji anao umri wa miaka 16 (na siyo chini ya miaka 16 kama unavyodai). Huyo si mtoto tena kisheria kwenye majimbo yaliyo mengi zaidi (majority of states) kule Marekani, na penginepo hata Tanzania. Isitoshe, felonies zinatofautiana. Kubaka kamwe haiwezi kusababisha mtuhumiwa akapewa adhabu ya kifo, na adhabu ya kifo si sawa na kifungo cha miaka 30. Kama huyu msichana angefanikiwa kuwaua wenzake wawili kwa sumu aliyopewa na mwenyewe akapona, nadhani hata huko Marekani kwa vyovyote wangemnyonga tu, mitigating circumstances notwithstanding.

Unazidi kukosea. Hakuna mahali niliposema ana umri chini ya miaka 16. Nilichosema ni kuwa taarifa inasema kuwa sasa ana miaka 16 lakini uhusiano haukuanza leo. Sasa kwa vile hatujui basdei yake na hatujui huo uhusiano ulianza lini, moja ya scenario ni kuwa alikuwa na umri chini ya miaka 16 alipoanza uhusiano. Au uhusiano ulianza baada ya yeye kutimiza miaka 16. Zote ni speculation. Lakini kwa vile ameshitakiwa kwa kubaka basi imani yangu ni kuwa hao waliomshtaki walijua kuwa alianza uhusiano wakati msichana hajatimiza umri wa consent. Hakuna mahali panaposema kuwa nguvu ilitumika katika uhusiano huo kwa hiyo kubakiza statutory rape kama option iliyobaki.

Nakubali kuwa kifungo chochote sio sawa na death penalty. Lakini hii haiondoi ukweli kuwa kubaka ni kosa linalochukuliwa kwa uzito wa pekee nchini kwetu. Na ukweli kuwa kutokana na hali ya jela zetu, mtu kuweza kukamilisha miaka 30 mle si kitu given.

Marekani hawanyongi watoto. Marekani mtoto ni chini ya miaka 18. Supreme Court imepitisha na kuokoa maisha ya watoto wengi waliokuwa death row. Ndiyo maana Lee Boyd Malvo hakuhukumiwa kifo wakati John Allen Mohamed amehukumiwa kifo. Malvo alikuwa na miaka 17 wakati wanaua watu Maryland,Virginia, Lousiana na Alabama. Waliua jumla ya watu 13. Randomly.
 
Haya mwenye facts, tuambie huyu msichana alizaliwa lini? Swala si kuwa mtoto wa miaka 16 ana akili tosha au la, ni sheria inasemaje! Mbele ya sheria msichana wa miaka chini ya hii hana kibali cha kufanya mapenzi hasa na mtu aliye na umri zaidi ya hapa. Mbele ya sheria msichana aliyechini ya umri huu , (hata kama ana matiti na anapasua darasani) bado hawezi kutambua kikamilifu kati ya kitu kibaya na kizuri. Si kuwa ni mazezeta bali hawajakomaa.

Hao prosecutors si wajinga kumshitaki mtu kwa kubaka kama alikuwa anatembea na mtu aliyevuka age of consent! Hii ni factual basis kulingana na taarifa husika!


Mchundo
Ndio maana Tz hatuendelei yani hatufuati sheria na katiba ina sema nini? tunafanya kwa maamuzi yetu tu na utashi wetu tu .

Sheria ya TZ kama sikosei inasema msichana chini ya miaka 18 hana uelewa wala utashi hivyo kuchapa naye ngono ni kumbaka kuanzia kifikira hadi kimwili.

Ni tendo linalovuruga saikorojia yake na kumdharirisha mbele ya watoto wengine kama unavyoweza mpa sumu na kumdaganya ni pipi hiyo kula.

Ila hofu yangu tu ni matukio mengi ya namna hii ni ya kupikwa .

Kama lile la PADRE SIXTUS KIMARO sina uhakika ila mazingira yake yalikua yanatia shaka kama ilivyo kwa huyu mazingira tata pia kwa BABU SEYA pia na wale wafanya biashara wa MAHENGE.

Nasikia SIXTUS walimwachia huru !!
 
Unazidi kukosea. Hakuna mahali niliposema ana umri chini ya miaka 16.

Nilichosema ni kuwa taarifa inasema kuwa sasa ana miaka 16 lakini uhusiano haukuanza leo.


Jee, ni wapi kwenye habari panataja kwamba uhusiano kati ya mdaiwa na mlalamikaji ulianza kabla ya mlalamikaji kufikisha miaka 16? Hebu tuonyeshe tafadhali. Vinginevyo ni wazi kwamba insination ulizoonyesha sehemu mbalimbali zinakufanya uamini kwamba mlalamikaji (yaani msichana) alikuwa hajafikisha miaka 16 wakati akianza uhusiano wa kimapenzi na mdaiwa bila ya kuwa na ushahidi kamili kuhusu madai yako, mfano:

Swala si kuwa mtoto wa miaka 16 ana akili tosha au la, ni sheria inasemaje! Mbele ya sheria msichana wa miaka chini ya hii hana kibali cha kufanya mapenzi hasa na mtu aliye na umri zaidi ya hapa.

Sasa kwa vile hatujui basdei yake na hatujui huo uhusiano ulianza lini, moja ya scenario ni kuwa alikuwa na umri chini ya miaka 16 alipoanza uhusiano. Au uhusiano ulianza baada ya yeye kutimiza miaka 16. Zote ni speculation. Lakini kwa vile ameshitakiwa kwa kubaka basi imani yangu ni kuwa hao waliomshtaki walijua kuwa alianza uhusiano wakati msichana hajatimiza umri wa consent.

Si kweli kwamba mdaiwa ameshitakiwa kwa kosa la kubaka, na nashangaa umetoa wapi madai kama haya kwani hakuna sehemu yoyote kwenye habari husika inayodai kitu kama hiki. Tunaambiwa kwamba mdaiwa alifikishwa mahakamani kwa shitaka la kusaidia mtu kutaka kujiua.

"...Jackob Laizer, jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Bukoba akidaiwa kumsaidia mwanafunzi anayetuhumiwa kuwa na uhusiano naye wa mapenzi, kutaka kujiua kwa sumu ya thiodan."



Hakuna mahali panaposema kuwa nguvu ilitumika katika uhusiano huo kwa hiyo kubakiza statutory rape kama option iliyobaki. Na ukweli kuwa kutokana na hali ya jela zetu, mtu kuweza kukamilisha miaka 30 mle si kitu given.

Haya ni maoni yako binafsi. Suala la mdaiwa kushutumiwa kwa kosa la kubaka halitajwi na halipo kabisa kwenye habari tuliyopatiwa. Hata hivyo, ukweli unabakia kwamba kisheria na kihali halisi, adhabu ya kifungo cha miaka 30 kamwe si sawa na adhabu ya kifo aidha kwa Tanzania, Marekani au nchi yoyote duniani.

Marekani hawanyongi watoto. Marekani mtoto ni chini ya miaka 18.

Siyo sahihi. Inatofautiana baina ya jimbo na jimbo. Kulingana na vyanzo vyangu vya habari, majimbo kadhaa ya Marekani yanaruhusu kuhukumiwa kwa adhabu ya kifo kwa mtuhumiwa aliye chini ya miaka 18:

http://www.e-archives.ky.gov/Pubs/Public_Adv/mar98/juvdp.html

THE DEATH PENALTY IS USED IN ONLY HALF THE STATES FOR JUVENILES.
in 14 states with the death penalty, 18 is the age of accountability.
In 4 states, 17 year olds are eligible.
in 21 states, 16 year olds are eligible for the death penalty

Supreme Court imepitisha na kuokoa maisha ya watoto wengi waliokuwa death row. Ndiyo maana Lee Boyd Malvo hakuhukumiwa kifo wakati John Allen Mohamed amehukumiwa kifo. Malvo alikuwa na miaka 17 wakati wanaua watu Maryland,Virginia, Lousiana na Alabama. Waliua jumla ya watu 13. Randomly.

Tafadhali soma takwimu nilizotoa hapo juu. Hiyo uliyotaja ni kesi moja tu iliyotokea jimbo moja tu kati ya 21 yanayoruhusu adhabu ya kifo kwa watuhumiwa waliyo chini ya miaka 16 Marekani. Kwa hiyo sidhani kama ni mfano mahususi wa suala la adhabu ya kifo kwa watuhumiwa waliyo chini ya umroi wa miaka 16 kwenye majimbo 21 yanayoruhusu dhabu ya kifo kwa watuhumiwa waliyo chini ya miaka 16 kule Marekani.
 
Ndio maana Tz hatuendelei yani hatufuati sheria na katiba ina sema nini? tunafanya kwa maamuzi yetu tu na utashi wetu tu .

Sheria ya TZ kama sikosei inasema msichana chini ya miaka 18 hana uelewa wala utashi hivyo kuchapa naye ngono ni kumbaka kuanzia kifikira hadi kimwili.

Ni tendo linalovuruga saikorojia yake na kumdharirisha mbele ya watoto wengine kama unavyoweza mpa sumu na kumdaganya ni pipi hiyo kula.

Sheria gani haifuatwi?

Huwezi kusema sheria haifuatwi halafu ukasema "kama sikosei" au sina uhakika hiyo sheria ni nini. Utawezaje kujadili sheria ambayo hatujui inasemaje?

Ni sheria gani hiyo imesema msichana chini ya miaka 18 hana uelewa wala utashi ?
 
Jee, ni wapi kwenye habari panataja kwamba uhusiano kati ya mdaiwa na mlalamikaji ulianza kabla ya mlalamikaji kufikisha miaka 16? Hebu tuonyeshe tafadhali. Vinginevyo ni wazi kwamba insination ulizoonyesha sehemu mbalimbali zinakufanya uamini kwamba mlalamikaji (yaani msichana) alikuwa hajafikisha miaka 16 wakati akianza uhusiano wa kimapenzi na mdaiwa bila ya kuwa na ushahidi kamili kuhusu madai yako, mfano:

Mimi nimekiri kuwa sijui huo uhusiano ulianza lini.

Hivi ndivyo alivyosema baba mzazi kuwa huyu jamaa hakuanza jana. Sasa wewe mwenye uhakika tuambie wapi wametaja basidei yake huyu binti inayokufanya usisitize kuwa alikuwa na miaka 16 alipoanza huo uhusiano. Mimi sijui. Naspeculate! Mwenzangu?


Baba mzazi wa binti huyo, mkulima wa Nkwenda wilayani Karagwe, Ibrahimu Seleman alisema tangu awali amekuwa akiwasiliana na uongozi wa shule baada ya kujua taarifa za mwanawe kuendelea kuwa na uhusiano ya mapenzi na meneja huyo ambaye alifunguliwa kesi namba 257/2008 katika Mahakama ya Wilaya na kuachiwa kwa dhamana, lakini hakukoma kuendelea na mapenzi na binti huyo.

Si kweli kwamba mdaiwa ameshitakiwa kwa kosa la kubaka, na nashangaa umetoa wapi madai kama haya kwani hakuna sehemu yoyote kwenye habari husika inayodai kitu kama hiki. Tunaambiwa kwamba mdaiwa alifikishwa mahakamani kwa shitaka la kusaidia mtu kutaka kujiua.

Ninachojua ni kuwa madai ni kuwa Jacob alimpa huyu binti sumu ili apoteze ushahidi unaotokana na kesi yake ya kumbaka huyu msichana iliyofunguliwa awali. Nadhani tunasoma sehemu tofauti. Mimi nimesoma haya yafuatayo.

Inadaiwa meneja huyo alipeleka sumu hiyo ya kuulia wadudu ya thiodan shuleni anakosoma mwanafunzi huyo kwa lengo la kumtaka ajiue kupoteza ushahidi wa kesi inayomkabili ya kutuhumiwa kumbaka mwanafunzi huyo.

Swala si kuwa mtoto wa miaka 16 ana akili tosha au la, ni sheria inasemaje! Mbele ya sheria msichana wa miaka chini ya hii hana kibali cha kufanya mapenzi hasa na mtu aliye na umri zaidi ya hapa.


"...Jackob Laizer, jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Bukoba akidaiwa kumsaidia mwanafunzi anayetuhumiwa kuwa na uhusiano naye wa mapenzi, kutaka kujiua kwa sumu ya thiodan."

Hakuna mahali panaposema kuwa nguvu ilitumika katika uhusiano huo kwa hiyo kubakiza statutory rape kama option iliyobaki.


Haya ni maoni yako binafsi. Ukweli unabakia kwamba kisheria na kihali halisi, adhabu ya kifungo cha miaka 30 kamwe si sawa na adhabu ya kifo aidha Tanzania, Marekani au nchi yoyote duniani.

Sikatai. Ni mawazo yangu binafsi kuwa hukumu ya miaka 30 katika jela zetu ni sawa na adhabu ya kifo. Uko sahihi kabisa kunipinga.



Siyo sahihi. Inatofautiana baina ya jimbo na jimbo. Kulingana na vyanzo vyangu vya habari, majimbo kadhaa ya Marekani yanaruhusu kuhukumiwa kwa adhabu ya kifo kwa mtuhumiwa aliye chini ya miaka 18:

http://www.e-archives.ky.gov/Pubs/Public_Adv/mar98/juvdp.html

THE DEATH PENALTY IS USED IN ONLY HALF THE STATES FOR JUVENILES.
in 14 states with the death penalty, 18 is the age of accountability.
in 4 states, 17 year olds are eligible.
in 21 states, 16 year olds are eligible for the death penalty



Tafadhali soma takwimu nilizotoa hapo juu. Hiyo uliyotaja ni kesi moja tu iliyotokea jimbo moja tu kati ya 21 yanayoruhusu adhabu ya kifo kwa watuhumiwa waliyo chini ya miaka 16 Marekani. Kwa hiyo sidhani kama ni mfano mahususi wa suala la adhabu ya kifo kwa watuhumiwa waliyo chini ya umroi wa miaka 16 kwenye majimbo 21 yanayoruhusu dhabu ya kifo kwa watuhumiwa waliyo chini ya miaka 16 kule Marekani.

Tarehe 1 Machi mwaka 2005,Supreme Court ya Marekani (ambayo ndiyo mamlaka ya mwisho katika ufafanuzi wa sheria nchini humo) katika uamuzi uliopitishwa 5-4 ilipiga marufuku hukumu ya kifo kwa juveniles. Kwa msingi huo, hakuna state inayonyonga juveniles, period. Walikuwa wananyonga,ndio, lakini sio sasa. Quotation zako zimepitwa na wakati.

Soma hapa:


http://www.washingtonpost.com/wp-dyn/articles/A62584-2005Mar1.html
 
Tarehe 1 Machi mwaka 2005,Supreme Court ya Marekani (ambayo ndiyo mamlaka ya mwisho katika ufafanuzi wa sheria nchini humo) katika uamuzi uliopitishwa 5-4 ilipiga marufuku hukumu ya kifo kwa juveniles. Kwa msingi huo, hakuna state inayonyonga juveniles, period. Walikuwa wananyonga,ndio, lakini sio sasa. Quotation zako zimepitwa na wakati.

Soma hapa:


http://www.washingtonpost.com/wp-dyn/articles/A62584-2005Mar1.html

Lets face it, Fundi Mchundo, that's a fairly recent development in the more than 200 years history of the US Supreme court. At any rate, USA is not Tanzania and it doesn't change the essence of my argument that the girl in question should either be deemed to be severely mentally impaired i.e. retarded or be held responsible for attempted murder regardless of her age and prosecuted and punished according to applicable law in Tanzania.
 
Well,

Nadhani sheria ya ndoa inaruhusu msichana kuolewa akiwa na miaka 15, http://www.right-to-education.org/content/age/tanz.html
Hapa issue kubwa naona
1.Kufanya mapenzi na msichana akiwa bado mwanafunzi na ukampa ujauzito

2.Na hilo swala la kutoa sumu ili msichana ajiue au msichana kuataka kujiua ambayo inaweza kukuingiza hatiani kwa kosa la kushiriki au kusabisha kifo.
 
Nyuma ya Mahakama ya Kisutu kuna juvenile court ambako wale walio chini ya miaka 18 wanashitakiwa. Nadhani tunafanya hivi kwa sababu sheria inaamini kuwa wale walio chini ya umri huu si watu wazima kwa hiyo wanatakiwa kupimwa (?) na kuhukumiwa tofauti kwa matendo yao! Hii si ina ashiria kuwa tunaamini kuwa aliye chini ya umri huo hana uelewa na utashi kama aliyokuwa nao mtu mzima?

Kuhusu uwezo wa kuolewa nadhani kuna mparanganyo. Kuna mila na watu wanaodai kuwa msichana (?) aliye chini ya miaka 18 anaweza kuolewa. Kuna wengine walitaka umri wa kuweza kuolewa ushushwe hadi miaka 14. Lakini sidhani kama msichana wa chini ya miaka 18 anaweza kuolewa kisheria bila kibali cha mzazi au mlezi wake. Uwezo wa kufanya hivyo anaupata anapotimiza miaka 18 ( au whatever). Kwa hiyo bado tunabaki palepale hauwezi kuwa na uhusiano wa mapenzi nje ya ndoa na msichana mwenye umri chini ya miaka 18 ( au 16, nakiri sina uhakika). Na hauruhusiwi kufanya mapenzi na mwanafunzi wa shule ya msingi hata awe na umri gani. Ukimpa mimba mwanafunzi huyo ni miaka 30 lupango!
 
Well,

Nadhani sheria ya ndoa inaruhusu msichana kuolewa akiwa na miaka 15, http://www.right-to-education.org/content/age/tanz.html
Hapa issue kubwa naona
1.Kufanya mapenzi na msichana akiwa bado mwanafunzi na ukampa ujauzito

2.Na hilo swala la kutoa sumu ili msichana ajiue au msichana kuataka kujiua ambayo inaweza kukuingiza hatiani kwa kosa la kushiriki au kusabisha kifo.



...Kuhusu uwezo wa kuolewa nadhani kuna mparanganyo. Kuna mila na watu wanaodai kuwa msichana (?) aliye chini ya miaka 18 anaweza kuolewa. Kuna wengine walitaka umri wa kuweza kuolewa ushushwe hadi miaka 14. Lakini sidhani kama msichana wa chini ya miaka 18 anaweza kuolewa kisheria bila kibali cha mzazi au mlezi wake. Uwezo wa kufanya hivyo anaupata anapotimiza miaka 18 ( au whatever). Kwa hiyo bado tunabaki palepale hauwezi kuwa na uhusiano wa mapenzi nje ya ndoa na msichana mwenye umri chini ya miaka 18 ( au 16, nakiri sina uhakika). Na hauruhusiwi kufanya mapenzi na mwanafunzi wa shule ya msingi hata awe na umri gani. Ukimpa mimba mwanafunzi huyo ni miaka 30 lupango!

Nina sababu ya kung'ang'ania suala la sheria ya ndoa japo inaonekana sio mada hapa.

Sheria ya ndoa ya 1971 inasema msichana wa miaka 15 anaweza kuolewa. Anahitaji idhini ya mzazi, lakini idhini sio lazima iwapo msichana ni yatima, au haipatikaniki kwa sababu za kiutendaji (impracticable), au wazazi wanakataa bila sababu ya msingi.

Ina maana, sheria yetu inaona msichana wa miaka 15 kakomaa.

Anaweza, hata kama yuko darasa la nne, kujiamulia kuolewa. Akajamiwa usiku kucha. Akazaa watoto.

Lakini katika umri wa miaka 16 huyu Mama akiruka ukuta akajamiwa pembeni na mtu ambae sio muweme, huyu Maumba ataenda jela kwa kubaka mtoto, au tuseme Mama watoto - au mtoto Mama - asiyejua jema na baya!

Itakuwaje?

Itakuwaje Jaji ?
 
Sheria is an ass! Kwa wenzetu kijana wa miaka 18 anaweza kupiga kura, kujiandikisha kwenda vitani, kuendesha gari n.k. Lakini huyu haruhusiwi kununua sigara wala pombe mwenyewe.

Kuruhusiwa mtoto wa miaka 15 kuolewa ni kujaribu kuaccomodate mila na desturi zetu. Lakini tunaona hajakomaa ndiyo maana anahitaji kibali cha mzazi na hayo mengine.

Sidhani kama mzazi anaruhusiwa kumwachisha mtoto shule ya msingi ili aweze kuolewa. Kwa upande mwingine mtoto akishaolewa anachukuliwa kuwa mtu mzima kwa hiyo kuweza kufanya maamuzi juu ya mapenzi. Sidhani kama ukitembea nae itahesabika kuwa ni statutory rape. Itakuwa adultery.Swali ni je akiolewa na kuachika katika umri huu, ataruhusiwa kuendeleza libeneke?
 
Lets face it, Fundi Mchundo, that's a fairly recent development in the more than 200 years history of the US Supreme court. At any rate, USA is not Tanzania and it doesn't change the essence of my argument that the girl in question should either be deemed to be severely mentally impaired i.e. retarded or be held responsible for attempted murder regardless of her age and prosecuted and punished according to applicable law in Tanzania.

Mkuu, ukimpa mtoto kibiriti kuchezea akaunguza nyumba hauwezi kumlaumu kwa kudai kuwa heri angeunguza chumba chake tu! ni wewe uliyempa kibiriti ndiye utakayesulubiwa!

Unayempa mtoto sumu ili ajiue unabeba lawama zote. Usingempa sumu haya mengine yasingetokea.
 
Sheria gani haifuatwi?

Huwezi kusema sheria haifuatwi halafu ukasema "kama sikosei" au sina uhakika hiyo sheria ni nini. Utawezaje kujadili sheria ambayo hatujui inasemaje?

Ni sheria gani hiyo imesema msichana chini ya miaka 18 hana uelewa wala utashi ?


Sheria ya tanzania hairuhusu mtoto chini ya miaka 18 kuolewa.

Ila anaweza ruhusiwa kwa sababu maalumu na itambidi wazazi na mtoto wafuate taratibu ni kula kiapo mahakamani.

Kufanya ngono na mtoto chini ya miaka 18 ni kinyume cha sheria ya Tanzania na hua inatafsiriwa moja kwa moja ni tendo la kubaka.
 
Sheria ya tanzania hairuhusu mtoto chini ya miaka 18 kuolewa.

Ila anaweza ruhusiwa kwa sababu maalumu na itambidi wazazi na mtoto wafuate taratibu ni kula kiapo mahakamani.

Kufanya ngono na mtoto chini ya miaka 18 ni kinyume cha sheria ya Tanzania na hua inatafsiriwa moja kwa moja ni tendo la kubaka.

Sheria is an ass! Kwa wenzetu kijana wa miaka 18 anaweza kupiga kura, kujiandikisha kwenda vitani, kuendesha gari n.k. Lakini huyu haruhusiwi kununua sigara wala pombe mwenyewe.

Kuruhusiwa mtoto wa miaka 15 kuolewa ni kujaribu kuaccomodate mila na desturi zetu. Lakini tunaona hajakomaa ndiyo maana anahitaji kibali cha mzazi na hayo mengine.

Sidhani kama mzazi anaruhusiwa kumwachisha mtoto shule ya msingi ili aweze kuolewa. Kwa upande mwingine mtoto akishaolewa anachukuliwa kuwa mtu mzima kwa hiyo kuweza kufanya maamuzi juu ya mapenzi. Sidhani kama ukitembea nae itahesabika kuwa ni statutory rape. Itakuwa adultery.Swali ni je akiolewa na kuachika katika umri huu, ataruhusiwa kuendeleza libeneke?

Naomba kurudi kwenye sheria ya ndoa tena, maana ni muhimu sana hapa, na nitasema kwa nini.

LAW OF MARRIAGE ACT, 1971
Restrictions on Marriage: Part II (b) Section 13 (1) and 17 (1), (2)


Minimum Age

No person shall marry who, being male, has not attained the apparent age of eighteen years or, being female, has not attained the apparent age of fifteen years.

A female who has not attained the apparent age of eighteen years shall be required, before marrying, to obtain the consent:
(a) of her father; or
(b) if her father is dead, of he mother; or
(c) if both her father and mother are dead, of the person who is her guardian, but in any other case, or if all those persons are dead, shall not require consent.

(2) Where the court is satisfied that the consent of any person to a proposed marriage is being withheld unreasonably or that it is impracticable to obtain such consent, the court may, on application,
give consent and such consent shall have the same effect as if it had been given by the person whose consent is required by subsection (1).


Ninachotaka kusema ni kuwa, sidhani kuna atakaepinga kwamba uamuzi wa kuolewa ni mzito na wenye madhara (matokeao, consequences, implications) makubwa mara mia zaidi ya uamuzi wa kujamiwa kwa siku moja na chekibobu mpita njia.

Sasa, sheria hii ya ndoa inaruhusu msichana wa miaka 15 kijiamulia kuolewa na hivyo kuanza kujamiwa. Inahitaji idhini ya mzazi lakini sio lazima wakati wote upate idhini. Tena, hata baba akikatalia hiyo idhini ahakikishe ametoa sababu za maana, maana msichana anaweza kupinga akijisikia baba anamzibia tu. Kisheria baba hawezi kukataa kwa maamuzi yake tu, yaani objective standard.

Kwa hiyo, iwe chimbuko lake ni mila, au iwe ni desturi, au ni falsafa za Kiafrika, sheria ya ndoa inamchukulia msichana wa miaka 15 kwamba amekomaa!

Utaambiwaje kwamba tunatambua kwamba chini ya miaka 18 wewe ni mtoto na huwezi kufanya maamuzi ya kujamiwa kwa siku moja lakini unaweza kuolewa na miaka 15, ukalalwa usiku kucha, au kutwa kucha, kila siku, na kuzalishwa, na kufanyishwa kazi.

Huku unasoma?
 
nachanganyikiwa; Alitaka kumsaidia kujiua au alitaka kumuaa? Kwa nini alimbaka wakatiw alikuwa na uhusiano wa kimapenzi?

Kama utakuwa na kumbukumbu nzuri, sheria mpya iliyoletwa na Tamwa inasema uhusiano wowote wa kingono na msichana aliye chini ya miaka 18 kisheria ni ubakaji hata kama kulikuwa na consent, unless msichana huyo ni mwislamu ambaye shehe ameruhusu awe mke wa mtu huyo kwa mujibu wa kitabu kitakatifu, kwa hiyo kisheria huyo jamaa anaweza kubanwa kwa ubakaji
 
Naomba kurudi kwenye sheria ya ndoa tena, maana ni muhimu sana hapa, na nitasema kwa nini.

LAW OF MARRIAGE ACT, 1971
Restrictions on Marriage: Part II (b) Section 13 (1) and 17 (1), (2)


Minimum Age

No person shall marry who, being male, has not attained the apparent age of eighteen years or, being female, has not attained the apparent age of fifteen years.

A female who has not attained the apparent age of eighteen years shall be required, before marrying, to obtain the consent:
(a) of her father; or
(b) if her father is dead, of he mother; or
(c) if both her father and mother are dead, of the person who is her guardian, but in any other case, or if all those persons are dead, shall not require consent.

(2) Where the court is satisfied that the consent of any person to a proposed marriage is being withheld unreasonably or that it is impracticable to obtain such consent, the court may, on application,
give consent and such consent shall have the same effect as if it had been given by the person whose consent is required by subsection (1).


Ninachotaka kusema ni kuwa, sidhani kuna atakaepinga kwamba uamuzi wa kuolewa ni mzito na wenye madhara (matokeao, consequences, implications) makubwa mara mia zaidi ya uamuzi wa kujamiwa kwa siku moja na chekibobu mpita njia.

Sasa, sheria hii ya ndoa inaruhusu msichana wa miaka 15 kijiamulia kuolewa na hivyo kuanza kujamiwa. Inahitaji idhini ya mzazi lakini sio lazima wakati wote upate idhini. Tena, hata baba akikatalia hiyo idhini ahakikishe ametoa sababu za maana, maana msichana anaweza kupinga akijisikia baba anamzibia tu. Kisheria baba hawezi kukataa kwa maamuzi yake tu, yaani objective standard.

Kwa hiyo, iwe chimbuko lake ni mila, au iwe ni desturi, au ni falsafa za Kiafrika, sheria ya ndoa inamchukulia msichana wa miaka 15 kwamba amekomaa!

Utaambiwaje kwamba tunatambua kwamba chini ya miaka 18 wewe ni mtoto na huwezi kufanya maamuzi ya kujamiwa kwa siku moja lakini unaweza kuolewa na miaka 15, ukalalwa usiku kucha, au kutwa kucha, kila siku, na kuzalishwa, na kufanyishwa kazi.

Huku unasoma?

Kuhani. Sidhani kama inaruhusiwa mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari kuendelea kusoma akiwa ameolewa. Pengine Zanzibar lakini si bara.

Matatizo yetu ni katika kujaribu ku'accomodate' secular morals, misimamo ya kidini na ile ya kitamaduni. Ukisoma kuwa sheria imemwekea mizengwe mingi msichana wa umri wa miaka 15 kuolewa. Si uamuzi wake pekee unaotosha.

Pamoja na yote haya, ukweli ni kuwa mtoto wa umri huu hajakomaa bado. Wengi wanapata matatizo katika uzazi. Hormone zao ndiyo kwanza zimepata kichaa na wanaweza kufanya maamuzi ya ajabu. Hawa ndiyo wanaorubuniwa kwa chipsi na makonda wa dala dala. Bado ni watoto na wanahitaji kulindwa.
 

Kuhani. Sidhani kama inaruhusiwa mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari kuendelea kusoma akiwa ameolewa. Pengine Zanzibar lakini si bara.

Matatizo yetu ni katika kujaribu ku'accomodate' secular morals, misimamo ya kidini na ile ya kitamaduni. Ukisoma kuwa sheria imemwekea mizengwe mingi msichana wa umri wa miaka 15 kuolewa. Si uamuzi wake pekee unaotosha.

Pamoja na yote haya, ukweli ni kuwa mtoto wa umri huu hajakomaa bado. Wengi wanapata matatizo katika uzazi. Hormone zao ndiyo kwanza zimepata kichaa na wanaweza kufanya maamuzi ya ajabu. Hawa ndiyo wanaorubuniwa kwa chipsi na makonda wa dala dala. Bado ni watoto na wanahitaji kulindwa.

Niko na wewe kabisa. Ila nasema kuna jambo limepinda hapa.

Nasema tunapokuwa na sheria ya statutory rape inayozuia kulala na mtoto chini ya miaka 18 wakati huo huo mtoto wa miaka 15 anaweza kuolewa ni utaahira!

Kuolewa ukiwa na miaka 15 - ambayo inawezekana kisheria - ina madhara makubwa kama au hata kuzidi ya kujamiwa na mkaanga chipsi. Ukiolewa shule ndio basi tena, kama unavyosema. Au hata ukiruhusiwa kuendelea na shule wakati umeolewa huwezi kutegemea afanikiwe huyu msichana maana anaanza kuhudumia vibabu badala ya kutilia maanani shule.

Kujamiwa na mkaanza chipsi chini ya miaka 18 ni kubaka. Hakuna walakini wala idhini. Lakini kuolewa chini ya miaka 15 kunawezekana. Ni ajabu iliyoje.

Wanasema upate idhini ya baba. Lakini hiki kibabu kinachotaka kuoa mtoto kitakuwa kinatoka katika mila zinazoona ni poa kuoa vitoto, hivyo atakapoomba idhini ya jirani yake kuoa kitoto chake, utakuta yule baba anayeombwa idhini na mwenyewe ana vike vitoto vimejaa humo ndani. Hawezi kukataa!

Isitoshe, kama mzazi hapatikani, mahakama inaweza kutoa idhini. Kwa hiyo ni kiasi cha msichana aliyekufa na muuza chipsi kusema tu Baba yangu sijui alipo, hapatikanini. Mahakama itamruhusu kwa kigezo kile cha impracticability. Kwa hiyo kisichana cha miaka 15 kinaolewa vizuri tu!

Kama tunataka kulinda watoto wa kike tufute hii sheria ya ndoa.

Ningekuwa mimi muuza chipsi nataka kukilala kitoto cha miaka 15 ningekiambia kikajaze fomu za kuoana. Wakikuuliza idhini ya Baba na Mama sema wazazi wangu walinikimbia sijui walipo. Nakioa kwa mkuu wa kaya, nakishughulikia miezi 6, nakitema, natafuta kitoto kipya, manake kisheria tunaruhusiwa kuoa saba mara sabini!
 
Ni utaahira kweli. Ndiyo maana huko uswahilini kumejaa ndoa za mkeka. Watu wanafumaniwa na watoto wadogo, wanaozwa chap chap, mchezo umekwisha! Kama ulivyosema, kama tunaona si haki mtoto wa miaka 15 kujamiana na Fundi Mchundo mwenye miaka 60 kwa nini tunamruhusu Fundi Mchundo huyo huyo kumuoa? Na hakuna kinachomzuia Fundi Mchundo kumpa talaka mara kiu chake kinapokatika au anapotokea binti mwingine wa umri huo huo maana yule wa kwanza keshachoka! Nionavyo mimi tunalea pedophiles. Sielewi kwa nini tusipige tu marufuku kujamiana na mtu wa chini ya umri wa miaka 18? In other words, hakuna kuolewa chini ya umri huo hata kama Sarah Palin anaona sawa!
 

Ni utaahira kweli. Ndiyo maana huko uswahilini kumejaa ndoa za mkeka. Watu wanafumaniwa na watoto wadogo, wanaozwa chap chap, mchezo umekwisha! Kama ulivyosema, kama tunaona si haki mtoto wa miaka 15 kujamiana na Fundi Mchundo mwenye miaka 60 kwa nini tunamruhusu Fundi Mchundo huyo huyo kumuoa? Na hakuna kinachomzuia Fundi Mchundo kumpa talaka mara kiu chake kinapokatika au anapotokea binti mwingine wa umri huo huo maana yule wa kwanza keshachoka! Nionavyo mimi tunalea pedophiles. Sielewi kwa nini tusipige tu marufuku kujamiana na mtu wa chini ya umri wa miaka 18? In other words, hakuna kuolewa chini ya umri huo hata kama Sarah Palin anaona sawa!

Kwa sababu sisi wanaume - ambao ndio tumeandika hizi sheria - tunataka kuendelea kuwatumia wanawake kama chombo cha ngono.

Kuhusu Sarah Palin, yule mkwe wake mtarajiwa hajaonekana ni mbakaji kwa kumtia mimba mtoto wa miaka 17 kwa vile na yeye pia ni mtoto. Sisi sheria yetu ya statutory rape ya mwaka 1998 mtoto wa kiume wa miaka 12 anaweza kubaka msichana mkubwa kuliko mvulana! Yani, konda wa miaka 15 akimjamia msichana wa miaka 17 atakuwa amembaka.

Yule msichana wa miaka 17 karubuniwa - na hivyo kisheria kabakwa - na mtoto mvulana wa miaka 15. Kwa maneno mengine wanawake akili zao hazikuwi haraka kuliko za watoto wa kiume. Ujuha mwingine huo!

Tubadilishe hii sheria ya 1998 ili watoto wakijamiana wenyewe kwa wenyewe kitoto cha kivulana cha miaka 14 kisiambiwe kimembaka msichana wa miaka 17 na nusu!

Tunashindwa mpaka kuandika sheria zenye mantiki, huwezi kuniambia UDSM ni moja ya vyuo vilivyo juu katika orodha ya vyuo bora Afrika.
 
Back
Top Bottom