Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 44
Meneja wa Fedha wa Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Mjini Bukoba (BUWASA), Jackob Laizer, jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Bukoba akidaiwa kumsaidia mwanafunzi anayetuhumiwa kuwa na uhusiano naye wa mapenzi, kutaka kujiua kwa sumu ya thiodan.
Tangu Septemba mosi mwaka huu, Laizer alikuwa anashikiliwa na Polisi mkoani Kagera kwa tuhuma za kutaka kumuua kwa sumu mwanafunzi huyo wa Shule ya Sekondari ya Mugeza mwenye umri wa miaka 16 anayesoma Kidato cha Pili. Jana Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Henry Salewi, alipotafutwa na gazeti hili kuthibitisha kumshikilia meneja huyo, alisema:
Ndiyo tunamshikilia, na leo (jana) tumemfikisha mahakamani kwa kusaidia mtu kutaka kujiua unajua alikuwa na kahawara kake mwanafunzi Awali, meneja huyo alilazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera chini ya uangalizi wa Polisi akidaiwa kusumbuliwa na ugonjwa ambao haukutajwa na aliugua baada ya kukamatwa.
Inadaiwa meneja huyo alipeleka sumu hiyo ya kuulia wadudu ya thiodan shuleni anakosoma mwanafunzi huyo kwa lengo la kumtaka ajiue kupoteza ushahidi wa kesi inayomkabili ya kutuhumiwa kumbaka mwanafunzi huyo. Mwanafunzi huyo (jina tunalo) amelazwa Hospitali ya Mkoa wa Kagera.
Inadaiwa baada ya kupelekewa sumu hiyo na meneja huyo, aliipokea na kuweka katika chakula na kisha kuwapatia wanafunzi wenzake wawili waliotajwa kuwa ni Magdath Kafuba na Yakilila Ruta, wote wa Kidato cha Pili ambao ni marafiki zake. Kutokana na hali hiyo, mwanafunzi huyo na wenzake walikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera ambako wamelazwa hadi sasa katika wadi namba tano.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Henry Salewi, tukio hilo lilitokea Septemba mosi jioni wakati wanafunzi walipokuwa wakipata chakula cha jioni shuleni hapo. Hata hivyo, msichana anayedaiwa kuwa na uhusiano na meneja huyo amelazwa chini ya ulinzi wa Polisi pamoja na Laizer anayedaiwa kukabiliwa na shinikizo la damu na kuharisha damu, magonjwa ambayo yalijitokeza baada ya kukataliwa dhamana na polisi.
Kamanda Salewi alisema kukamatwa kwa Laizer kumetokana na maelezo ya mwanafunzi huyo kumtaja kuwa ndiye alimpelekea sumu hiyo ajidhuru, kuepuka kuandamwa na vyombo vya dola na aibu kwa jamii na wanafunzi wenzake wanaodaiwa wamekuwa wakimzomea kuwa ana mpenzi wakati anasoma. Alisema baada ya kupewa dawa hiyo, hakutaka ionekane kuwa yeye ndiye amejiua hivyo kutokana na kuwa karibu na wenzake hao.
Inadaiwa aliiweka sumu katika chakula na kushiriki nao kwa pamoja bila wao kujua kinachoendelea. Baada ya kula chakula hicho, watoto hao walianza kujigaragaza chini kwa maumivu huku wakiishiwa nguvu na kupoteza fahamu, ndipo uongozi wa shule ulipowakimbiza hospitalini kupata matibabu.
Baba mzazi wa binti huyo, mkulima wa Nkwenda wilayani Karagwe, Ibrahimu Seleman alisema tangu awali amekuwa akiwasiliana na uongozi wa shule baada ya kujua taarifa za mwanawe kuendelea kuwa na uhusiano ya mapenzi na meneja huyo ambaye alifunguliwa kesi namba 257/2008 katika Mahakama ya Wilaya na kuachiwa kwa dhamana, lakini hakukoma kuendelea na mapenzi na binti huyo.
Agosti 28, mwaka huu, baba huyo alipokea ujumbe wa simu kutoka kwa binti yake aliyedai anaumwa kichwa, na kutokana na ujumbe huo aliwasiliana na uongozi wa shule kujua kilichompata. Aliambiwa mtoto wake haumwi, bali alikuwa amenyanganywa simu na mkuu wa shule iliyodaiwa kununuliwa na Laizer na kwa hasira mkuu huyo wa shule aliitupa chini na kuivunja vunja.
Septemba mosi, baba huyo alisema alipokea simu kutoka kwa uongozi wa shule hiyo na uongozi wa Polisi wakimjulisha kuwa mwanawe amekula sumu na amekimbizwa hospitalini, hali iliyosababisha baba huyo kufunga safari kutoka wilayani Karagwe hadi Bukoba kumwona mwanawe. "Nilipata mshtuko kusikia mwanangu amekula sumu.
Jana saa sita za mchana mimi na mamake tulifika hapa Bukoba kumwona, lakini sikukuta mgonjwa, bali nilikuta wagonjwa inashangaza mwanangu sijazungumza naye, mama yake ndo anaongea naye kwa sababu kuna mengine labda hawezi kuniambia.Taarifa niliyosoma aliyoandikisha polisi inasikitisha, alisema mzazi huyo. Juni mwaka huu, polisi walimkamata meneja huyo wa BUWASA kwa tuhuma za kubaka na kumweka kinyumba mwanafunzi huyo na alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Bukoba Julai 2, mwaka huu. Alikana mashitaka na aliachiwa kwa dhamana yenye thamani ya Sh milioni moja.
Tangu Septemba mosi mwaka huu, Laizer alikuwa anashikiliwa na Polisi mkoani Kagera kwa tuhuma za kutaka kumuua kwa sumu mwanafunzi huyo wa Shule ya Sekondari ya Mugeza mwenye umri wa miaka 16 anayesoma Kidato cha Pili. Jana Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Henry Salewi, alipotafutwa na gazeti hili kuthibitisha kumshikilia meneja huyo, alisema:
Ndiyo tunamshikilia, na leo (jana) tumemfikisha mahakamani kwa kusaidia mtu kutaka kujiua unajua alikuwa na kahawara kake mwanafunzi Awali, meneja huyo alilazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera chini ya uangalizi wa Polisi akidaiwa kusumbuliwa na ugonjwa ambao haukutajwa na aliugua baada ya kukamatwa.
Inadaiwa meneja huyo alipeleka sumu hiyo ya kuulia wadudu ya thiodan shuleni anakosoma mwanafunzi huyo kwa lengo la kumtaka ajiue kupoteza ushahidi wa kesi inayomkabili ya kutuhumiwa kumbaka mwanafunzi huyo. Mwanafunzi huyo (jina tunalo) amelazwa Hospitali ya Mkoa wa Kagera.
Inadaiwa baada ya kupelekewa sumu hiyo na meneja huyo, aliipokea na kuweka katika chakula na kisha kuwapatia wanafunzi wenzake wawili waliotajwa kuwa ni Magdath Kafuba na Yakilila Ruta, wote wa Kidato cha Pili ambao ni marafiki zake. Kutokana na hali hiyo, mwanafunzi huyo na wenzake walikimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Kagera ambako wamelazwa hadi sasa katika wadi namba tano.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Henry Salewi, tukio hilo lilitokea Septemba mosi jioni wakati wanafunzi walipokuwa wakipata chakula cha jioni shuleni hapo. Hata hivyo, msichana anayedaiwa kuwa na uhusiano na meneja huyo amelazwa chini ya ulinzi wa Polisi pamoja na Laizer anayedaiwa kukabiliwa na shinikizo la damu na kuharisha damu, magonjwa ambayo yalijitokeza baada ya kukataliwa dhamana na polisi.
Kamanda Salewi alisema kukamatwa kwa Laizer kumetokana na maelezo ya mwanafunzi huyo kumtaja kuwa ndiye alimpelekea sumu hiyo ajidhuru, kuepuka kuandamwa na vyombo vya dola na aibu kwa jamii na wanafunzi wenzake wanaodaiwa wamekuwa wakimzomea kuwa ana mpenzi wakati anasoma. Alisema baada ya kupewa dawa hiyo, hakutaka ionekane kuwa yeye ndiye amejiua hivyo kutokana na kuwa karibu na wenzake hao.
Inadaiwa aliiweka sumu katika chakula na kushiriki nao kwa pamoja bila wao kujua kinachoendelea. Baada ya kula chakula hicho, watoto hao walianza kujigaragaza chini kwa maumivu huku wakiishiwa nguvu na kupoteza fahamu, ndipo uongozi wa shule ulipowakimbiza hospitalini kupata matibabu.
Baba mzazi wa binti huyo, mkulima wa Nkwenda wilayani Karagwe, Ibrahimu Seleman alisema tangu awali amekuwa akiwasiliana na uongozi wa shule baada ya kujua taarifa za mwanawe kuendelea kuwa na uhusiano ya mapenzi na meneja huyo ambaye alifunguliwa kesi namba 257/2008 katika Mahakama ya Wilaya na kuachiwa kwa dhamana, lakini hakukoma kuendelea na mapenzi na binti huyo.
Agosti 28, mwaka huu, baba huyo alipokea ujumbe wa simu kutoka kwa binti yake aliyedai anaumwa kichwa, na kutokana na ujumbe huo aliwasiliana na uongozi wa shule kujua kilichompata. Aliambiwa mtoto wake haumwi, bali alikuwa amenyanganywa simu na mkuu wa shule iliyodaiwa kununuliwa na Laizer na kwa hasira mkuu huyo wa shule aliitupa chini na kuivunja vunja.
Septemba mosi, baba huyo alisema alipokea simu kutoka kwa uongozi wa shule hiyo na uongozi wa Polisi wakimjulisha kuwa mwanawe amekula sumu na amekimbizwa hospitalini, hali iliyosababisha baba huyo kufunga safari kutoka wilayani Karagwe hadi Bukoba kumwona mwanawe. "Nilipata mshtuko kusikia mwanangu amekula sumu.
Jana saa sita za mchana mimi na mamake tulifika hapa Bukoba kumwona, lakini sikukuta mgonjwa, bali nilikuta wagonjwa inashangaza mwanangu sijazungumza naye, mama yake ndo anaongea naye kwa sababu kuna mengine labda hawezi kuniambia.Taarifa niliyosoma aliyoandikisha polisi inasikitisha, alisema mzazi huyo. Juni mwaka huu, polisi walimkamata meneja huyo wa BUWASA kwa tuhuma za kubaka na kumweka kinyumba mwanafunzi huyo na alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Bukoba Julai 2, mwaka huu. Alikana mashitaka na aliachiwa kwa dhamana yenye thamani ya Sh milioni moja.