The Zitto saga: Vyombo vya habari vinaiua CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Mie niliandika mapema kabisa kuwa sipo hapa Kumtetea Zitto au kusema Zitto hana hatia.

Pia sipo hapa kusema Waandishi wa habari wanasema uongo.

Nafahamu kuwa ukweli siku zote uko katikati.

Ninachosikitika ni kuwa Magazeti yanahusiana na Chadema, kuanza kutumia njia za Zitto. Ni juzi tu hapa watu walimkalia kooni Zitto kwa kwenda TBC na kuongea aliyoongea. Hilo wengi hawakulipenda. Sasa hawa Waandishi, wanafanya hilohilo la kutatua matatizo ya CHADEMA kwenye Media. Hili linaongeza tatizo badala ya kulitatua.

Kila chama kina matatizo yake na hata watu kwenye familia wana matatizo yao. Ila ningelitegemea watu wenye akili zao na Wasomi kama wanavyojulikana Chadema na huku wana wanasheria wazuri sana na wazee wenye busara kama akina Baregu, Slaa nk watakaa na kutatua mataizo yao ndani ya mikutano ya chama na si kuja kushambuliana hapa kama vita ya Iran na Iraq.

Kama mtu anaona kuwa Matatizo ya CHADEMA yatatatuliwa kwa Zitto kwenda TBC na CDM wanamsiliba kwenye magazeti kwa ule msemo "wewe mwaga mboga, mie namwaga ugali........" basi endeleeni hivyo na kila la kheri.
 
Chadema tokea kumaliza uchaguzi imekosa muelekeo.

Hakuna lolote walilofanya likawa na muelekeo.

1. Wabunge wanachukua hatua zao watakazo na kujisifia kwenye vyombo vya habari.

2. Slaa na Mbowe misimamo iliyotofautiana.

3. Mdahalo usioeleweka malengo waliofanya na Cuf.

4. Magazeti yanayomilikiwa na Chadema yaliyojaa 'hujuma' dhidi ya Zitto.

5. Kesi za viti vya wanawake na kujitoa baadhi ya watu.

Wanahitaji kukaa chini na kujipanga upya. Inatupa picha kuwa Mbowe hana ubavu mbele ya watu fulani ndani ya chama kama Slaa na Zitto. Kuna hitajika uthabiti kwenye uongozi.

Unaandika mambo meeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeengi kwa kuhishisi tu.
 
Si kuwa Waberoya anamtetea Zitto nia yake ni kuona viongozi wa Chadema wanavurugana na Zitto, Waberoya ni mmoja wa Zitto haters toka UDSM hapa anajaribu kuwachanganya watu tu ambao hawamjui yeye toka enzi za 'Kubwajinga', soma article yake hii




Mkuu hii kitu kama ina ukweli 80%, ila naamini Zitto will turnish politically very sun!
 
I think huyu kijana [Zitto] anasumbuliwa na kitu wazungu wanaita "egocentric," that's all.
 
Si kuwa Waberoya anamtetea Zitto nia yake ni kuona viongozi wa Chadema wanavurugana na Zitto, Waberoya ni mmoja wa Zitto haters toka UDSM hapa anajaribu kuwachanganya watu tu ambao hawamjui yeye toka enzi za 'Kubwajinga', soma article yake hii

Quinine, mimi siyo najisifu nina mawazo huru sana, Zito simchukii hata siku moja labda wewe wa juzi ndio unafikiri hivyo, maskini kwa article hiyo moja tu!!
Zitto nilikuwa naye na nilisupport sana alipotaka kuwa mwenyekiti wa cdm na chadema walipobaka demokrasia niliwachukia sana, Zitto nilimsupport hata alivyosupport dowans (why not) maana niliwaza kama yeye.

Zito juzi aliporopoka na kumsifia Kikwete nilimpinga!!! na nikapelekea kuandika hiyo article na ukiisoma hiyo article kama mtu mwenye akili, narudia kama mwenye akili, vitu vingi niMESPECULATE NA zito alijibu hizo tuhuma!

sina beef na mtu, sina chuki, situmii jina langu la ukweli, nasema ukweli!!!

sina cha mkumbo, ukinifuatilia kesho nitampinga Slaa kwa hili na kumpa kuddos kwa lile! nitakusifu wewe kwa hili na kesho nitakupinga kwa lile! naamini kwangu inaniweka huru na sina unafiki

siwachanganyi viongozi wa chade,a, soma thread zingine za watu wengine wanavyowaza, siko peke yangu, na ukifikiria sana na pengine niwe mwazi ninamzimikia Zitto ile mbaya!!! na ninapomrarua ni kutaka kuridhisha nafsi kuwa tuko pamoja!!!!

Kama wewe ni kijana na umeishawhi kufanya kazi na Zitto kama mimi ninavyomfahamu.

I repeat I dont hate Zitto, I hate all people who are against the truth, especially you!
 
Acha porojo. Inawezekana speed yako ya kusoma Tanzania Daima na MwanaHALISI ni mara moja baada ya miezi mitatu. Una-judge msimamo wa mtu kwa kusoma article yake moja!!! Madhara ya zitto kwenye chama hayana mfano. Ili chama ki-operate kama taasisi lazima ki-dscipline wanachama wa aina ya zitto wanaodhani kuwa bila wao chama hakisongi mbele. Chadema siyo ccm wanaosema mtaji wake ni jk. Mtaji wa chadema ni kila mwanachama bila kujali nafasi ya mwanachama kwenye chama.
Mie sipingi watu hapa kuadhibiwa kwa Zittoma Zitto anastahili hiyo adhabu. Ila kama Mkeo ni Malaya na wewe unaamua Kumuaibisha kwa kuitangazia jumuiya nzima mnayoishi kuwa Mkeo ni Malaya, Mama watoto wako ni Malaya na tena hadi unawaambia wanao "wanangu ehh, mama yenu ambaye ni Mke wangu ni Malaya....." unafikiri utakuwa umemkomoa mkeo peke yake? Ukipita wewe na wanao pia mtaonyeshwa kidole.

Sikonge

Hivi unafikiri CHADEMA haijui kinachoandikwa kwenye magazeti hayo?
Wajue au wasijue, mimi hiyo hainihusu so longer naona maandishi ya kumsiliba Zitto na Zitto akiendelea kutesa kwenye Media na vimbwanga vyake. Wamchukue Zitto na kumuweka Angle Thita kwa kumuambia yeye si Msemaji wa Chama. Kama hasikii basi waanze kumtenga kidogokidogo hadi mwenyewe ajuwe hatakiwi. Akilalamika, wao wanasema "si kweli" na hamna zaidi.

Chadema tokea kumaliza uchaguzi imekosa muelekeo.

Hakuna lolote walilofanya likawa na muelekeo.

1. Wabunge wanachukua hatua zao watakazo na kujisifia kwenye vyombo vya habari.

2. Slaa na Mbowe misimamo iliyotofautiana.

3. Mdahalo usioeleweka malengo waliofanya na Cuf.

4. Magazeti yanayomilikiwa na Chadema yaliyojaa 'hujuma' dhidi ya Zitto.

5. Kesi za viti vya wanawake na kujitoa baadhi ya watu.

Wanahitaji kukaa chini na kujipanga upya. Inatupa picha kuwa Mbowe hana ubavu mbele ya watu fulani ndani ya chama kama Slaa na Zitto. Kuna hitajika uthabiti kwenye uongozi.
Haya ni Mawazo yako Mkuu. Nina hakika mtu kama Slaa hawezi kukurupuka kwa jambo kama hili lisilo na haraka namna hiyo. Mbowe na Slaa hawajatofautiana ila wewe hujaelewa wanachokisema. Mengine Mbowe anaweza kuwa anakosea kwa sababu hakuwa Bungeni na hivyo hayafahamu vizuri. Magazeti hayamilikiwi na Chadema ila ni Wanachama wa Chadema wanamili hayo Magazeti. Ni sawa na mali za Mo Dewji, Rostam Azziz, Lowassa nk si mali ya CCM kwa sababu tu wao ni wanachama wa CCM. Kesi ya Wanawake iliongelewa sana hapa na kujibiwa.

Vita ya Panzi=?
Ehhh bwana wee, sasa hivi CCM wanapumua kidogo maana hakuna tena anayelalamika kuhusu Chadema kuzuiliwa Mikutano na maandamano. Hakuna tena anayelia kuhusu Tume mpya ya Uchaguzi, katiba mpya nk nk. Wote tumekaa kumkodolea macho ZITTO. Tunacheza kwa kadri wanavyotupigia mziki. Tukija kukumbuka shuka, kumeshakuwa kweupe na Screen inaonyesha sisi 0 na wao 5. Yes, kama Real Madrid na Barceona, 5 bila mwanawane.
 
Mie siamini kama ni sahihi endapo mtu atafanya jambo la kuleta hisia za kifisadi na wote tukasema lisisemwe kwasababu anatokea chama fulani. Huu ni ubaguzi mkubwa na unafiki. Kamwe sitalikubali hili. Hivi Zitto si alipendwa na watanzania baada ya kulalamikia mazingira ya kifisadi katika mkataba wa Buzwagi? Ukisoma Mwanahalisi ya leo utaona kuna upande wa pili wa Zitto, ningeomba akanushe yaliyosemwa ili tujue kama hizo ni njama za kumbomoa au ni uandishi wa Mwanahalisi kwa manufaa ya taifa kama walivyozoea.

Narudia, kama kuna ufisadi lazima uwekwe adharani bila kujali nani anahusika na chama gani kinahusika. Tanzania kwanza, vyama vyenu baadae!
 
Nashawishika kuwa kuna madhara ya Zitto kwa nafasi ya Uenyekiti wa Mbowe na hivyo gazeti lake la Tanzania Daima na nashawishika pia kuwepo kwa harufu ya madhara ya Zitto kwa nafasi ya Mtunza Hazina wa Chadema Antony Komu na hivyo Gazeti lake la Mwanahalisi ni dhahiri, mwanaChadema usikubali kuingizwa kwenye vita hii ya maslahi ya watu binafsi walioifanya Chadema kama kampuni yao binafsi kwa jina la Chama.

Hii inanikumbusha hadithi ya Spika Sita kukihatarisha chama cha Mapinduzi wakati kimsingi nyuma ya pazia ilikuwa ni hatari kwa Lowasa na marafiki zake.

MwanaChadema...beware, usikubali kufuata mkumbo na kukiacha kitovu cha matatizo yaliyopo ndani ya Chadema!!

Zito kama kiongozi kutotekeleza maamuzi ya wabunge wenzie, na kwenda kueleza wazi kuwa yeye hakukubaliana na uamuzi huo, hiyo ina uhusiano gani na gazeti la Mbowe au la Kubenea? Umeunganisha habari ili kupata tafsiri unayoitaka lakini imeshindwa kudhihirisha ukweli. Kama hufahamu, kwa ufupi tu ni kwamba, Mbowe si mmilki pekee wa gazeti la Tanzania Daima bali ni mmoja wa wamilki, na gazeti halifanyi kazi kwa matakwa ya Mbowe kwa vile tu ni mmoja wa wamilki.

Gazeti la Tanzania Daima, wakati wa kipendi cha kampeni, lilitajwa na ofisi ya msajili wa Vyama Vya Siasa kuwa ni gazeti lililokuwa linaripoti kwa kufuata kanuni zote bila ya upendeleo.
 
Sikonge..hawa waandishi wametumwa Rasmi na Viongozi wa Chadema....Viongozi wenzako wanapokuwa hawakutaki na hawana njia ya moja kwa moja ya kukutoa, wanaanza tumia njia hizi za "Kupiga Filimbi"....article wanazozitoa sasa sio za mwanzo....!!!

kwa wanaofuatilia siasa za Tanzania hili sio geni...Wakati Marehem Kighoma Ali Malima...anapigwa vita na magazeti ya Chama chake cha "Uhuru" na 'Mzalendo" na ya Serikali...hii ilikuwa picture kamili ya kuwa CCM walikuwa hawamtaki Marehem Malima...Hii ilimfanya Malima mwenyewe kutoka bila kufukuzwa ndani ya Chama...
 
Nimekuwa nafuatilia mwenendo wa Zitto kwa siku nyingi sana hapa JF na kwenye vyombo vingine vya habari duniani. Nimekuja kuanza kupata mashaka na mwenendo wa Zitto kama wengi wanavyosema pale alipoanza kushangilia kununua kwa mitambo ya Umeme ya wizi. Wengine wanakuja na kusema kuwa tangu aingie kwenye kamati ya Madini, ametoka akiwa siye yule Zitto tunayemfahamu.
Unataka avumiliwe mpaka lin?
Sipo hapa kuonyesha kama Zitto ana makosa au lah maana hili limeshasemwa sana na sasa linaanza kutia kinyaa. Jana pia niliandika kuwa, tawi lisilozaa, hukatwa na kutupwa motoni ila Mkono Mchafu, haukatwi na kutupwa, bali huoshwa kwa sabuni na kukaushwa huku ukisubiri kuendelea na shughuli utakazopangiwa na Ubongo.
Kwani hajui kama anayoyafanya ni kama kansa ambayo mkono usipokatwa mwili wote utaoza?
Kipi Bora,kubaki na maumivu au mwili kuoza na kufa
Zitto ni MKONO, na hivyo bila kujali mabaya aliyoyafanya, hatuwezi kumkata. Kitendo kinachofanywa na akina Kubenea, Kibanda na Ngurumo ni kuukata Mkono. Na kwa sababu wao si madaktari, wanakata huo mkono na kusababisha maumivu kwa mwili mzima na kuvuja damu. Hii inaweza kupelekea Binadamu huyu (CHADEMA) kuvuja damu hadi mwisho akakata roho (soma maelezo ya Waberoya).
Kwa nini usiseme kuwa n1 mkono wenye kansa unaohitaji kukatwa!!!
wakati mwingine huwa inabidi kuukata Mkono au Mguu au ........ ili kuzuia Kansa isiendee mwili mzima. Ila hii hufanywa na Madaktari baada ya kufanya utafiti wa kutosha na kujua ugonjwa umeanzia wapi na umeishia wapi, wapi wakate ili kuzuia ugonjwa. Ukifanya vibaya, utashangaa kansa bado inaendelea. Pia kuna hata bahati mbaya ambapo kansa hiyo huendelea kuula mwili hadi kumuuwa binadamu kama njia nyingine nzuri hazitatumika kuitibu hii kansa.
Thanks,by then kwa sasa Huwezi ku compea nafasi ya Zitto CHADEMA na kiungo muhimu mwilini kama mkono au mguu,may be "Apendix" ambayo hata ikitolewa mwilini mwili unapata afadhali.

Zitto si wa kukata ila pia si wa kuacha aendelee na tabia yake. Jana nilimalizia kwa kusema "Zitto Kabwe ni kama glass ya Wine - Handle with care."
Atakuwa handled with care hadi lini?!!!
Mimi naamini huyu bwana kendelea kubaki CDM ndo itakuwa ni mwanzo wa anguko la CDM.
Ni mtazamo tu masela ...
 
Chadema ni taasisi
chadema ni chama makini
chadema ndio chama pekee cha upinxzania tanzania wengine vibaraka
chadema ina taratibu zake za kutatua migogoro kama ipo
kubenea na mwanahalisi, ulimwengu na raia mwema ni people's speakers for chadema na wanyonge watanzania
sokomoko,sikonge, malaria sugu na waberoya hawa wote ni vibaraka wa ccm wanalambwa na ridhiwani
 
Sikonge, Wabz,

KUna ule wimbo ulikuwa inaimbwa zamani "uliambiwa na wewe ukayapuuza, na leo hii dunia inakucheka".. Mara nyingine huwa nafika hatua kujilaumu kwa kuyaona tangu awali matatizo ya Chadema na nilipoandika kwa muda mrefu na kudhihakiwa na kubezwa na kama laana niliposema wanahitaji mfumo mpya, reforms na hata uongozi mpya, sasa matendo yao yanaonyesha wazi kuwa chama kimedoda na kinahitaji sura mpya kabisa kukinusuru.

Waswahili husema mwanzo wa ngoma ni lele, zaidi ya miaka mitatu iliyopita, Chadema imekuwa na msuguano wa kiongozi ndani yake, yako ya kinza Chacha Wangwe, Zitto, Kafulila, BawaCha, vijana na sasa kukosekana kabisa kwa uongozi kukiandaa chama kwa uchaguzi, kuchanganyikiwa kwa baada ya uchaguzi na huu mvutano wa kumsusia Kikwete.

Leo tunamtuhumu Zitto kwa kukosa umoja na kwenda ropoka TBC, lakini si hata Mbowe naye karopoka na kudai wao hawampingi au kumkataa Rais? Then what is Lissu and Slaa doing wasting time and hope za watu kudai eti wanapinga matokeo na leo hii kuna legitimace gani ya kudai wale waliokataa kwenda Bungeni na kufanya matembezi ya mshikamano kumwacha Kikwete Solemba wanapaswa wajieleze?

To me, this is a party in shambles and rather than taking Mwanakijiji advice of comeout clean kwa Watanzania, sasa wanatafurta Bangusilo within.

I have nothing personal against Zitto or Mbowe, but this is a fact, the two can never see eye to eye and they do not have an ounce of repsect towards another one.

Solution is for both to step down from party leadership and stop the internal bleeding.

Sasa kila mmoja wao ana kundi lake ndani ya chama na wafuasi katika magazeti. Then ni slander, smear and whatever crap left and right. Kama watu hawakumuelewa Chacha Wangwe au hata kuelewa kilichotokea wakati wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa Chadema 2009, then wanachama wa Chadema na wafuasi wake ama wameshakuwa kama Wanachama wa CCM wa kuwa na ile blinding trust na kuchukua makundi. Tofauti ya CCM na Chadema ni kuwa Wanachama wa CCM pamoja na tofauti zao, azma zao ni kuhakikisha kuwa CCM inaendelea kushika madaraka na kupewa dhamana na wananchi.

If you ask me today what is Chadema or directly what is Mbowe and Zitto are there for or to gain, I have no clue to equate their bickering fight to the better good of Chadema ir Tanzania rather it is about selfishness and personal interest.

Bottom line, Chadema is becoming a myopic party which does not embrace diversity and it is not inclusive. What we see is artificial image, full of wanja, facial powder, sijui skin foundation lakini ukiwaambia wasafishe uso kama ndio wametoka kitandani, ni mautangotango na chunusi kibao na hawatazamiki.

It has been almost 5 years of lack of cohesiveness ndani ya chama, na wamebakia kuwindana na kufanyiana blackmail and as a result, hakpakuwa na united front hata strong leadership kwa ajili ya huu uchaguzi ambao ni ghadhabu za Watanzania na wala si umahiri wa Chadema ambao karibu almanusra uikoseshe CCM Urais (this is a fact).

So leo watu wanapumua mapavu na Zitto anakaangwa, mnaacha kujiuliza, mbona hii ni Chacha Wangwe part 2?
 
Naheshimu mawazo yako ndicho kilichopo moyoni hata YESU ALISEMA ....ACHENI MAGUGU NA NGANO VIKUE PAMOJA KISHA MTAVUNA NGANO NA KUWEKA GHALANI NA MAGUGU NI KUCHOMA MOTO hatumzidi ujanja sasa ni wakati wa mavuno.... CDM kama chama kina taratibu zake na malengo yake vivo hivyo wana taratibu za kupembua hii ni ngano na haya magugu Hawakosi Fth colome ndani ya CDM lakini pia code na anti jaming sytem Ya kuwatambua! IISHI CDM IISHI TANGANYIKA!! WAISHI WATANGANYIKA...
 
Zitto si wa kukata ila pia si wa kuacha aendelee na tabia yake. Jana nilimalizia kwa kusema "Zitto Kabwe ni kama glass ya Wine - Handle with care."

Inawezekana Zitto ni kama glass ya Gongo ambayo ni hatari kwa matumizi ya binadamu!!!!
 
naheshimu mawazo yako ndicho kilichopo moyoni hata YESU ALISEMA ....ACHENI MAGUGU NA NGANO VIKUE PAMOJA KISHA MTAVUNA NGANO NA KUWEKA GHALANI NA MAGUGU NI KUCHOMA MOTO hatumzidi ujanja sasa ni wakati wa mavuno.... CDM kama chama kina taratibu zake na malengo yake vivo hivyo wana taratibu za kupembua hii ni ngano na haya magugu Hawakosi Fth colome lakini pia code na anti jaming sytem IISHI CDM IISHI TANGANYIKA WAISHI WATANGANYIKA...

Duh!umenigusa sana kwenye nyekundu!ni kweli kabisa!
 
Quinine, mimi siyo najisifu nina mawazo huru sana, Zito simchukii hata siku moja labda wewe wa juzi ndio unafikiri hivyo, maskini kwa article hiyo moja tu!!
Zitto nilikuwa naye na nilisupport sana alipotaka kuwa mwenyekiti wa cdm na chadema walipobaka demokrasia niliwachukia sana, Zitto nilimsupport hata alivyosupport dowans (why not) maana niliwaza kama yeye.

Zito juzi aliporopoka na kumsifia Kikwete nilimpinga!!! na nikapelekea kuandika hiyo article na ukiisoma hiyo article kama mtu mwenye akili, narudia kama mwenye akili, vitu vingi niMESPECULATE NA zito alijibu hizo tuhuma!

sina beef na mtu, sina chuki, situmii jina langu la ukweli, nasema ukweli!!!

sina cha mkumbo, ukinifuatilia kesho nitampinga Slaa kwa hili na kumpa kuddos kwa lile! nitakusifu wewe kwa hili na kesho nitakupinga kwa lile! naamini kwangu inaniweka huru na sina unafiki

siwachanganyi viongozi wa chade,a, soma thread zingine za watu wengine wanavyowaza, siko peke yangu, na ukifikiria sana na pengine niwe mwazi ninamzimikia Zitto ile mbaya!!! na ninapomrarua ni kutaka kuridhisha nafsi kuwa tuko pamoja!!!!

Kama wewe ni kijana na umeishawhi kufanya kazi na Zitto kama mimi ninavyomfahamu.

I repeat I dont hate Zitto, I hate all people who are against the truth, especially you!


Unajaribu kujitetea sana lakini ukweli wako ndio huu. Unawachukia viongozi wa chadema kwa sababu walimnyima rafiki yako zito nafasi ya kugombea uenyekiti wa chadema. Hata hiyo article ya kumponda zito uliitoa kwa nia ya kupima upepo hapa jf, wala hukuwa na nia yoyote ya kumsema rafiki yako zitto. Kwa sababu unakiri mwenyewe kwamba mambo mengi uliyoandika ilikuwa ni speculations, ungekuwa umedhamiria kweli ungeandika facts, sio speculations. Unapowakandia viongozi wa chadema unasema ni facts lakini kwa zito unasema ni speculations, hapa ndipo rangi na sura yako halisi inapoonekana. Hujakatazwa kumshabikia zito hata kama unaamua kuweka pembeni weledi wako kwa sababu ya mapenzi yako kwake lakini hiyo sio sababu ya kuwaona wengine wasio-support zito kwamba hamnazo.

Hebu acha chuki hizi za kirejareja dhidi ya viogozi wa chadema na wanajf wasio na mrengo mmoja na wewe, uwaheshimu nao watakuheshimu lakini ukianza kuleta maneno mbofu mbofu hapa, tutakwenda na wewe sambamba.
 
Mie niliandika mapema kabisa kuwa sipo hapa Kumtetea Zitto au kusema Zitto hana hatia.

Pia sipo hapa kusema Waandishi wa habari wanasema uongo.

Nafahamu kuwa ukweli siku zote uko katikati.

Ninachosikitika ni kuwa Magazeti yanahusiana na Chadema, kuanza kutumia njia za Zitto. Ni juzi tu hapa watu walimkalia kooni Zitto kwa kwenda TBC na kuongea aliyoongea. Hilo wengi hawakulipenda. Sasa hawa Waandishi, wanafanya hilohilo la kutatua matatizo ya CHADEMA kwenye Media. Hili linaongeza tatizo badala ya kulitatua.

Kila chama kina matatizo yake na hata watu kwenye familia wana matatizo yao. Ila ningelitegemea watu wenye akili zao na Wasomi kama wanavyojulikana Chadema na huku wana wanasheria wazuri sana na wazee wenye busara kama akina Baregu, Slaa nk watakaa na kutatua mataizo yao ndani ya mikutano ya chama na si kuja kushambuliana hapa kama vita ya Iran na Iraq.

Kama mtu anaona kuwa Matatizo ya CHADEMA yatatatuliwa kwa Zitto kwenda TBC na CDM wanamsiliba kwenye magazeti kwa ule msemo "wewe mwaga mboga, mie namwaga ugali........" basi endeleeni hivyo na kila la kheri.

Nnavyoelewa mimi ni kuwa hayo ni magazeti yanafanya kazi zake na CHADEMA ni chama kinafanya shughuli zake. Hivyo vyombo viwili vipo independent kabisa ila wewe mwenzetu una mtIzamo kuwa hayo magazeti ndio CHADEMA.

Hapo ndipo unapochanganyikiwa.
 
Status
Not open for further replies.
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom