jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,987
- 22,515
Nakumbuka 2008 kulikuwepo na thread ya uchaguzi wa marekani ambayo kama sikosei ilikuwa ya GT.This year,miaka minne imepita na sasa uchaguzi ni November.Tunaweza kuitumia thread hii kutoa maoni yetu na pia kupashana habari za kuhusiana na kampeni na uchaguzi wenyewe.
Binafsi ninaamini mchuano utakuwa mkali,na sasa kampeni zimepamba moto,tumeshuhudia vituko na mambo ya kushangaza,mfano ni ile hotuba ya Clint Eastwood kuweka kiti na kuongea nacho kama vile anaongea na Obama.Lakini kwa dharau kubwa na matusi!
Mpinzani wa Obama,yani Romney,yeye anajinasibisha na ufanya biashara,kwamba ana uzoefu na biashara na ameendesha biashara zake kwa faida na hivyo ujuzi wake huo anaweza kuutumia kulikwamua taifa kwenye matatizo ya kiuchumi inayokabiliana nayo.
Obama wote tunajuwa,yeye anasema anapigania haki za middle class pamoja na wananchi wenye vipato vya chini.
Anasema kwamba maendeleo ya nchi yanatokana na kipaumbele kupewa middle class,amekuwa akitumia maneno kama vile "we will build the economy from "the middle out" and "from the bottom to top"
Anasema wanaostahili msamaha wa kodi ni wananchi ambao hizo pesa watazitumia na hivyo uchumi kukuwa,na si kuwapa misamaha zaidi matajiri wakubwa ambao hawazihitaji, kwani hilo ndilo Bush alilolifanya lakini matokeo yake ni economic crisis,kwahiyo anasema hatuwezi kurudia hayo tena kwani doing the same thing over and over again expecting different results ni dalili za ukichaa!
Issue wanazopingana ni nyingi,tutaendelea kukumbushana,kuna women rights na mambo mengine kama vile health care na National security vikiwemo vita.
Lakini kubwa kuliko yote ni uchumi,na wakipimwa kwenye hilo,inaonekana kama vile Romney ana upper hand kwani polls zinaonyesha kuwa watu wana imani naye kwenye issue za kiuchumi kuliko Obama.
Jambo ambalo wengine tusingependelea,ni kama watu wa Obama wataanzisha vita kwasababu wanajuwa kuwa ikija kwenye security,basi Obama yuko juu especially mara baada ya seal 6 team kumwua Bin Laden kwa amri yake...Tuombe Mungu hilo lisiwe the case kwasababu vita always si nzuri,lakini tumeshashuhudia mambo kama hayo yakitokea.
Nitaendelea kuleta habari na maoni kuhusiana na uchaguzi huu,pia mnakaribishwa kuchangia lolote kuhusiana na uchaguzi na wagombea pamoja na kampeni zao.
Kama kuna thread kama hii imeshaazishwa,basi mods mniwie radhi na muiunganishe na hiyo nyingine kama ipo.