The Tanzania Political Chaseboard: Tafsiri ya Mambo Mazito Kisiasa Tukielekea 2015

CCM KUSHUKA VIWANGO VYA SIASA KIASI HIKI WATANZANIA TUTARAJIE KUSIKIA MAAJABU MAZITO ZAIDI KULIKO YALE YALIOIBULIWA NA KAMPENI ZA ARUMERU MASHARIKI

Ukiona CCM sasa inainamia silaha mpya kama vile:

(1) 'VURUGU ZA GREENGUARD-Mwigulu', (2) 'Ukabila-Ole Sendeka' na sasa (3) 'Oparesheni Kimbiza Kivuli cha Mwalimu Nyerere kila kona ya Nchi' inayoongozwa na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa akisaidiana kwa karibu sana na Mzee wa Usingizi wa Pono Mzee Wasira a.k.a. Mzee Tyson, ni wazi kwamba hali si shwari hata kidogo ndani ya CCM

Si miezi mingi sana Watanzania tutashuhudia maajabu ya dunia zaidi ya yale yanyoendelea kuibuliwa kwa CCM kwenye kampeni kule Arumeru Mashariki; watch this space.
 
CCM hakiwezi kupiga hatua yoyote ya maana kisiasa katika kipindi cha sasa cha uelewa mkubwa kwa wananchi kwa sababu tngu waondoke kwenye ITIKADI ZILE ZA UJAMAA NA KUJITEGEMEA mpaka hivi sasa hawana tena msingi wowote kunakogotea siasa zao.

Hii ndio maana mara nyingi watu wamejaribu kujaza pengo hilo la ki-itikadi kwa kudadavua kwamba huenda sera mama ya chama hiki hivi sasa ni UFISADI NA KUJITEGEMEA.

Kwa mantiki hiyo, wala watu wenye akili hawatoona ajabu yoyote inapotokea kwamba hivi sasa kila mwana CCM siasa zao zimegeuka kuwa ni zile za
KUKIMBIZANA NA KIVULI CHA MWALIMU NYERERE kote majukwaani.

Na kama hilo halijatosha, nani alidhani kwamba ile CCM ya Baba wa Taifa kingegeuka kuwa ni kinara wa vurugu, uhuni na mauaji kikiongozwa na Mwigullu Nchemba??

Je nai alidhani ile CCM leo hii kingegeuka kuwa
KINARA WA UKABILA MAJUKWANI bila aaibu yoyote??

Na kama mtu unabaki umepigwa bumbwazi basi ni wakati mwafaka mkazifahamu hizo sera zake mpya na kujihadhari sana na hicho chama.
 
CHADEMA MKOA WA ARUSHA NA TAIFA, HONGERENI SANA KWA UTEUZI MAKINI WA TIMU YA KAMPENI KULE ARUMERU MASHARIKI PAMOJA NA VIONJO VYA 'SIASA ZA KISTAARABU' KWA WATANZANIA

Katika yeye huyu kijana mdogo mwenzetu asiyejikweza wala kupenda kuonekana kimbelembele, WaTanzania sikilizeni maneno haya kwamba Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kazaliwa upya katikati yetu.

Hakika kuna nuru ya matumaini mapya pale hivyo sote tumsaidie kwa kumpa ushirikiano mkubwa atakaohitaji kwetu.

Uongozi wa CHADEMA mkoa wa Arusha pamoja na uongozi wa chama taifa, hongereni sana kwa umakini wa hali ya juu kumpa 'huyu mwanafunzi wenu wa siasa za kistaarabu CHADEMA' kazi ya kwenda kuongoza kampeni akishirikiana kwa karibu sana na WaTanzania wenzake wakazi wa vijiji vya kule Arumeru Mashariki.

Sote tunafahamu kwamba lengo kuu la chama kufanya uteuzi huu wala haukua kwa ajili ya jina tu la 'Nyerere' bali zaidi uteuzi ulitokana na kiu kubwa ya kwenda kuonyesha WaTanzania wa Arumeru Mashariki nini maana ya 'siasa za kistaarabu' kama ambavyo mlivyopata kumfundisha katika darasa kubwa iliojaa Makamanda Chipukizi wengine kibao (Sugu, Mnyika, Kabwe, Lema, Lissu, Heche, Msigwa, Mdee, Nassari ...) waliopata kusifika na kuogopeka kwingineko nchini.

Hakika kazi nzuri siku zote huleta matunda mazuri kama haya tunayoyasubiria kule Arumeru Mashariki hivi karibuni.


Kazi ipo! Jina Nyerere ni tishio Arumeru, hadi ifike tarehe 1 mapovu yatawatoka sana, inaonesha Vicent anawanyima usingizi viongozi wa ccm.

Lakini mbona iko wazi tu, Vicent ni mwanaukoo tu katika ukoo wa Nyerere, anaitwa Vicent Josephat Kiboko Nyerere, Wasira, Mkapa sijui nani wote wanalijua hili na huyu kijana hayuko Arumeru kwasababu anatumia jina la Nyerere, yuko pale kama mwanaCHADEMA na ndiye meneja wa kampeni za Chadema hapo Arumeru, sasa kina wasira mapovu yanawatoka.

Mbona hawamsemi yule mbuge wa viti maalum anaetumia jina la Nyerere, na yule alikuwa ni mke wa Madaraka Julius Kambarage Nyerere, na ndoa yao ilishavunjika lakini mbona anatumia jina la Nyerere? Why Vicent Nyerere ambaye huyo mwenye jina Nyerere ni babu yake kabisa?

Ninyi CCM ninyi, mmekosa sera kabisa, na ninawaambia mkiendelea na huu ujinga wenu jimbo mnalipoteza hilo, mmefikia hatua mnapiga kampeni eti Sioi achaguliwe ili apate mshahara wa kutunza familia kwasababu ameachiwa mzigo mkubwa wa kutunza familia?

Hii ni sera au ni ujinga? hay endeleeni na ujinga wenu mtakalia Nyerere, sijui sioi kaachiwa familia, wenzenu wanzidi kujipanga,tarehe 1 april jimbo hiloooooooo linago
 
NI FARAJA ILIOJE PALE HATA MMACHINGA, MKULIMA, MFUGAJI NA MFANYAKAZI WA KITANZANIA PINDI ANAPOJIHISI KUWA NI MWANAHISA MUHIMU KATIKA CHAMA SAWA TU NA WENGINE????

Jamani ni jambo la kheri ilioje kwa akina kabwela kama vile Wamachinga wa Dar, Mbeya, Arusha na Mwanza kuchangia chama chao CHADEMA hata kama ni sumni tu na wakaondoka mahali pale wakiwa wamejiridhisha moyoni kwamba hapa na yeye pamoja na kipato chake duni pia ni MWANAHISA wa kutegemewa na chama chake!!!

Naam, nasema ya kwamba ni furaha ilioje kwa mfugaji tu hata kuku pindi anapochangia japo ka-kuku wake tena kwa hiari bila kuletewa Balozi wa Nyumba 10, ili na yeye apate kujihesabu kuwa ni sehemu muhimu kati ya MATOFALI YA TAIFA yatakayotumika kujenga misingi imara iliopotea kule CCM ya kulinda HESHIMA NA UTU WA KILA MTANZANIA bila kuzingatia mitabaka katika jamii.

Ndio, nauliza hivi kwamba kama hata nchi tajiri duniani kama Marekani unakuta mgombea wa chama kama vile Obama kwa Democrats anachangiwa hadi dola moja moja na vijana vijiweni tu hadharani, tangu lini CHADEMA kikawa kimegeuka kuwa chama cha matajiri wachache kuchangiwa ma-bilioni na akina Chenge, Lowassa na Rostam Aziz kifichoni??

Ni kweli kabisa kwamba nahoji hapa kwamba inakua vipi mtu kukejeli Tshs 26/- milioni zilizochangiwa na wlalahoi kwa hiari na mapenzi yao wenyewe kwa CHADEMA eti mtu akiona kwamba ni kiasi kidogo mno wakati sote tunajua kwamba siri ya bei ya mafuta ya taa kupaa angani, petroli, dizeli na bidhaa nyingine kibao nchini ni shauri ya CCM kuingiza kitenesi chao mle, bila huruma kwa walalahoi, hivyo kufanya maisha kuwa magumu kupindukia ilmradi wao wawe wanaingiza ma-bilioni ya fedha za kununulia kura hata kama wananchi tunakufa?

Hakika mtu au watu walioiunda hii propaganda dhidi ya CHADEMA nawashauri muende mkamuombe kwanza ushauri Mh Tambwe Hizza ili siku nyingine msije mkajitokeza hadharani na upuuzi kama huu, kukidhalilisha chama chenu, na hata nyinyi wenyewe kupitia huko huko Clouds FM mkaonekana hamnazo!!!

Kila mwana-CHADEMA popote pale ulipo, jitokezeni twende tukamuumbue SHETANI YA UFISADI kule CCM kwa kwenda kukichangia chama chetu wenyewe CHADEMA ili kusaidia kuharakisha juhudi za ukombozi nchini.

Hakika ni jukumu letu sote kujipa wenye RAHA ya kuondokana na ukandamizaji na UFISADI wa CCM-Mamboleo, leo leo na wala tusingoje kesho!
 
And I believe whatever the Party says...and trust me you can'y become a tyranny on your own without people upholding you at the top of the pyramid!
 
Ni kweli kabisa,

FISADI akikichangia CCM ni lazima MCHONGO uundwe wa namna gani FISADI huyo atakavyoweza kurejesha fedha zake mara 100 kidogo.

Naam, quid pro quo; nothing goes for nothing katika swala zima la KUNDI GANI LINAPOCHANGI chama cha kisiasa kama vile MAFISADI na michango yao kwa CCM.

Hivyo vivyo ndivyo alivyofanyiwa hata Karamagi kupewa mradi wa kupitisha mizigo pale bandarini kwa kumrudishia fadhila za kuwekeza mabilioni katika CCM kununulia haki za watu kuchagua viongozi wapendao

Quid pro quo
 
HONGERA SANA CHADEMA KWA KUTUWEKA MBELE SISI UMMA WA TANZANIA KUKICHANGIA WENYEWE CHAMA CHETU ILI TUENDELEE KUWA NA SAUTI YA MWISHO NACHO

Safi sana Kamanda Mbowe, CHADEMA ni chama chetu sisi wenyewe wananchi na ili tuwe na sauti nacho wakati wote fedha zote tukichangia chama sisi wenyewe kama ambavyo wananchi wengi tulivyokwishaanza kote nchini.

Acheni CCM kiendelee kuchangiwa na MAFISADI kina Rostam Aziz nyuma ya pazia ili waendelee kuwa naa sauti ya mwisho nacho kuendeleza UFISADI katika kila sekta ya nchi.

Clouds FM, mnapotusikia tukisema CHADEMA ni 'Sauti na Nguvu ya Umma' ni nguvu ya umma kweli hadi sisi wenyewe umma wa Tanzania kuwa ndio chanzo cha fedha zake kujiendesha bila kubabaishwa na MAFISADI sawa na MAPACHA WATATU walivyowashindeni kuvuliwa gamba shauri ya ufadhili binafsi.

Enzi za CCM kuchangiwa fedha na akina kabwela, wakulima na wafanyakazi sote tulisikia kwamba UADILIFU ULIKUA MBEEELE KAMA TAI NA HESHIMA KWA UTU WA MTANZANIA.

Lakini kipindi ambapo sasa chama hiki wachangiaji wake wamekua ni matajiri wachache tu nchini, tangu hapo Heshma ya Utu wa Mtanzania ikawa ni ndoto na wenye sauti hivi sasa pale si walalahoi tena bali ni kambi rsmi ya MAFISADI wachache kukigeuza chama hicho kampuni binafsi.

Kwa sababu tu baadhi ya watangazaji wa Clouds FM ni washabiki mbumbumbu wa CCM kwao wao wanadhani CHADEMA kuchangiwa na wakulima na wafanyakazi walioachwa solemba na CCM katika Umiliki na Uendeshaji wa Siasa za nchi hii eti ni udhaifu - kawaulizeni wale waliopigwa umande miguuni watawafahamisheni kwamba njia hii walioibuni CHADEMA ni kiboko kutokubabaishwa na MAFISADI hata siku moja.

Kila mwana-CHADEMA, kuchangia chama chako kutukomboa kuondokana na dhuluma za miaka nenda rudi chini ya CCM-Mamboleo wala hakuhitaji mtu uwe tajiri bali ni moyo tu na kujua DIRA yetu kuu katika harakati hizi za ukombozi.

Nguvu ya Umma mbeeeele kama tai katika kukichangia wenyewe chama chetu kila kona ya nchi ili wasije MAFISADI wachache wakatupokonya hii lulu ya ukombozi kama ambavyo walivyowahi kutupokonya CCM na kuwaweka akina Adam Malima kuwa ndio 'wakuu wa vitega uchumi' kwenye hoteli za kifahari mikoani.

Njoo wewe, njooni nyote tukakichangie chama chetu tukakipige chini hiki Chama Cha Mafisadi kiulaini kama kutumbukiza mkate mkuuuubwa kwenye chai na kugeuzwa uji uji mara moja.

Wakuu nasikiliza Clouds FM arusha,

nimesikia tangazo ambalo Mwenyekiti wa Chadema na Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Mh. Mbowe akiwakaribisha wafuasi wote wa chadema ktk harambee ya kuchangia chama ambayo itafanyika Naura Spring hotel tarehe 23/02/2012.

Viva Chadema!
 
CCM kuleta vurugu nchini endapo watayarudia yale ya Igunga kule Arumeru Mashariki.
 
Ni kweli kabisa,

FISADI akikichangia CCM ni lazima MCHONGO uundwe wa namna gani FISADI huyo atakavyoweza kurejesha fedha zake mara 100 kidogo.

Naam, quid pro quo; nothing goes for nothing katika swala zima la KUNDI GANI LINAPOCHANGI chama cha kisiasa kama vile MAFISADI na michango yao kwa CCM.

Hivyo vivyo ndivyo alivyofanyiwa hata Karamagi kupewa mradi wa kupitisha mizigo pale bandarini kwa kumrudishia fadhila za kuwekeza mabilioni katika CCM kununulia haki za watu kuchagua viongozi wapendao


Ndo maana unaona watu wanatumia nguvu nyingi sana kuhajihalalisha kama nchi imekuwa nyumba zao.
 
KWA TIDO MHANDO HAKIKA MZEE AGHA KHANI HAPO UMELAMBA DUME SASA TV KAMA ULAYA NA VYOMBO VYENU VYOTE KUPUMUA HEWA SAFI ZAIDI

Mzee Agha Khani, kwa Dastan Tido Mhando, hapo umelamba Dume; JEMBE la ukakika hilo.

Hakika huyu ni mfanyakazi asiendekeza hulka za U-Bosi wa kijinga, mwenye kuruhusu ubunifu, changamoto na wa kujituma mwenyewe kazini bila kujificha nyuma ya wengine wala kuning'iniza koti kwenye kiti kwenda kupiga shoga Breakpoint au Rose Guarden.

Enyi wafanyakazi wa ngazi za chini hapo Mwananchi Communication sasa nyote mkae miguu sawa maana Tido Mhando majungu anayoyasikia na kuyafanyia kazi mara moja UTENDAJI KAZI WAKO (atalijua hilo hata bila ya wewe kutambua kajuaje).

Ndio, kwake yeye gwiji huyu wa habri duniani majungu safi ni WELEDI wako katika kila unachofanya, na kule KUJIWEKA HURU AKILINI bila kuleta vikwazo binafsi kazini kama vile itikadi za kichama, kidini, 'Sisi Wa Hapa ametukuta' na uchafu mwingine wa ina hiyo.

Mwananchi Communication sasa katuleteeni TV kama za Ulaya zisizotegemea memo toka kwa Waziri ndio zirushe habari hewani.

Nasema tuleteeenii TV ile funika bovu Tanzania nzima hakuna mfano wake.
Kwa kweli mkiangalia vizuri mwenendo wa mambo nchini ni wazi kwamba WaTanzania tunatamani sana tena sana TV HURU KWA UHALISIA WA NENO HILO HURU lakini mpaka leo hii pengo hilo halijajazwa katika soko la habari nchini; do something tangible here and now!!!

Lakini kwa upande wenu enyi wazembe wazembe na wapika majungu kwenu nyie ujio wa Jembe Tido Mhando ni habari mbaya sana hivyo mkae migu nje kwenda TBC Ujima.
 
Na hiyo itakua ni DOSARI YA KUDUMU katika CV ya Makamba kisiasa mbele ya WaTanzania endapo atathibitisha kwa mara nyingine kwamba hana heshima kuacha demokrasia ifanye kazi yake bila kuingiliwa.

Sote tunakumbuka taarifa aliyotoa kwenye vyombo vya habari siku chache kabla ya uchaguzi Igunga kuhusu madai hewa kwamba CHADEMA wanaleta vijana kutoka Mara kuja kuleta vurugu na kwamba hilo CCM ITAJIBU MAPIGO; kilichofuata ilikua ni damu kila mahali ya wafuasi wa CDM wenyeji wa Igunga.

Hadi hivi sasa watoto wamebaki yatima kutokana na kauli zisizo na umakini kama hiyo aliyotoa Makamba; damu ya WaTanzania bado inaendelea kumlilia na wala hatutopenda kuliona hili likijirudia Arumeru.

The World is watching the situation very closely now than ever, and that's a fact anyway!!!!!!


Ikumbukwe ata Igunga awa Jamaa walikwenda mwishomwisho. Awa ndiyo wanaosuka mpango mzima wa wizi wa kura.[/QUOTE]
 
MTAZAMO WA KI-CCM KWENYE UENDESHAJI WA VYOMBO VYA HABARI NCHINI TANZANIA UNATUKOSESHA ZAIDI YA DOLA MILIONI 3,750,000 (TSH 5,812,500,000) KUNUFAIKA NA LUGHA YA KISWAHILI KWENYE VYOMBO VYA HABARI KIMATAIFA KILA KUNAPOPITA MIAKA 5

Tanzania yetu haitoweza kunufaika vya kutosha na 'ALMASI LUGHA YA KISWAHILI' ambayo taifa letu ndilo kinara wake duniani, endapo mtazamo wa kudhibiti vyombo vya habaari visitoe fursa sawa kwa sauti pinzani tofauti na ile ya CCM haitobadilika hivi karibuni.

Ingawaje Rais Kikwete amepata kusema kwamba yeye ametoa uhuru mkubwa kwa vyombo vya habari nchini na kwamba kiwango anayotoa nao uhuru huo kamwe hauwezi kupatikana katika mataifa mengi sana duniani, lakini tunapokumbuka swala la Danstan Tido Mhando na utendaji wake TBC na jinsi serikali ya Kikwete ilivyoamua kuzika almasi mtu huyu kwenye samadi ni wazi kwamba yote aliokua akisema mkuu wa nchi hadi hapo umeshaingia maswali kama si dosari kamili.

Siku zote ukitaka kujua uhuru wa habari ukoje katika nchi wala usipotezewe wakati kwa watumishi wa serikali katika eneo hilo kukuletea nyaraka kibao zenye kuthibitisha hilo, cha msingi wewe kawatazame tu uso wale wenye SAUTI HURU NA PINZANI katika jamii; kama nyuso zao zina bashasha basi huo ndio ukweli kuhusu uhuru wa vyombo vya habari katika nchi hiyo ila kinyume chake ni usaliti mkubwa kwa mtu yeyote kudai kuna uhuru wa maoni na uhuru kwa vyombo vya habari vya kutosha.

Hadi hivi sasa malalamiko ya CUF na CHADEMA kuzuiwa habari zao kutokurushwa kwenye TV, radioni na wakati mwingine kuandikwa kwenye magazeti hivi sasa ni kilio kisichopata mtu yeyote mwenye kujali katika wizara husika ili kuingilia kati na watu tuone tofauti wazi wazi.

Kimsingi, mantiki yote inatuelekeza kwamba endapo mtu yeyote atakua anadhani kwamba kulazimisha kila chombo cha habari kwenda chini ya viwango vya medani hiyo ilimradi tu CCM kipate kipaumbele kwa kila namna, hilo nalo lina hasara zake kwa njia mbili mbaya zaidi; kwanza jambo hilo linafanya wananchi walio wengi kuchukia vyombo vya nyumbani na kutegemea vile vya nje ya nchi, pili matokeo ya hali ya aina hii husababisha chama tawala kichukiwe zaidi kinyume kabisa na matarajio ya wale wanaohimiza upendeleo kwa vitisho kwa wamiliki wa vyombo hivo.

Tatu na mbaya zaidi ni kwamba kwa mazingira ya aina hii katika serikali kusimamia vyombo vya habari ki-upendeleo isiokua na mvuto kwa wataalam wetu wanaorejea kutumikia nchi kama Ndg Tido Mhando, taifa linapoteza fursa na fedha za kigeni kwa kiwango cha hali ya juu mno kama ambavyo imedadavuliwa hapa chini

Laiti serikali yetu ingefunguka akili japo hata kidogo tu na kumpa ushirikiano mzuri na murua huyu Gwiji wa Habari Duniani, Danstan Tido Mhando, hakika nawambieni Tanzania tutakua na uwezo kuzalisha WATUMISHI KIWANGO zaidi ya 10 kila mwaka kupitia kwa mikono ya huyu baba kwenda kutumikia vyombo vya kimataifa kwa ufanisi mkubwa.

Endapo kweli fikra za watu wanaosimamia swala zima la uendeshaji wa vyombo vya habari nchini kweli utabadilika kuwa huru zaidi basi maana yke ni kwamba nchi yetu ambayo ndio imejaliwa Kiswahili murua ingeweza kutumia hiyo
'Absolute Advantage' (kidhungu kidogo kwa msisitizo tu) taifa lingeweza kuingiza malipo ya fedha za kigeni zisizopungua USD 75,000 (Tshs 116,250,000/-) kwa kila MWANDISHI KIWANGO ambaye tutaweza kumpeleka huko nje ya nchi na kutumikia kwa viwango zaidi ya alivyofanya Ndg Mhando hapo nyuma kidogo.

Ndio, nasema kwamba laiti baadhi ya viongozi wetu wangejiruhusu walau kuwa POSITIVE na mtazamo wa ndugu yetu Tido Mhando katika medani ya habari nchini walau hata kwa robo tu basi ninao uhakika kwamba hali itakua ni nyingine kabisa na bora zaidi.

Hakika jambo hili lenye uwezo mkubwa w kutusaidia kutatua japo kakijisehemu ya CHANGAMOTO SUGU LA UKOSEFU WA AJIRA nchini hilo litaweza kushudiwa endapo pale tutakapoweza kuzalisha na kuwepeleka nje ya nchi rasilmali watu hawa mahiri walau 10 kila mwaka ambao wataweza kuingizia taifa USD 750,000 (Tshs 1,162,500,000) kila mwaka.

Na kama kiwango hicho cha uzalishaji wanahabari mahiri kwa viwango vya kimataifa itaendelea walau kwa kipindi cha miaka 5 basi inamaana kwamba nchi yetu itakua ikiingiza USD 3,750,000 (Tshs 5,812,500,000) kutokana tu na watu kumi tu ambao ndugu yetu Tido Mhando ANAO UWEZO wa kuwaandaa na kuwafikisha kunakohitajika ili taifa tunufaike vema na umahiri wetu wa Lugha ya Kiswahili duniani.

Kwa kuhitimisha napenda nihoji kwa kurudisha kumbukumbu nyuma kidogo, ni vema tukakumbushane kwamba ni hivi majuzi tu tumemuona Mhe Nchimbi akitetea kwa nguvu ya ajabu kutaka 'URAIS KWA VIJITOTO' nchini, sasa kama utendaji na usimamizi wa wizara chini ya vijana ka Mhe Nchimbi ndio inazunguka gizani kwenda kuminya sauti za vyombo vya habari kizamani hivi ili sauti pinzani zisisikike je kuna faida gani kwa dhana ya uongozi kwa vijana kama njia zao ni za kizee kuliko hata umri wa babu zao??

Mhe Nchimbi hebu una sababu ya kubadili fikra ili WaTanzania tunufaike na lugha ya Kiswahili katika eneo hili la habari nje ya mipaka yetu kwanza kwa kufungua uhuru wa vyombo vya habari kwa namna inayoonekana na kuhisiwa na kila mwananchi hadi kule TBC bila kuweka utaratibu wa urushaji habari kwa kutegemea KIMEMO cha mtu aitwaye waziri au ikulu.
 
WANA JF WAMPATA SIKIO RAIS KIKWETE KUHUSU CHANGAMOTO ZA UPANGAJI HOLELA WA MISHAHARA NA MARUPURUPU SERIKALINI UNAODIDIMIZA MORALI YA KAZI, TIJA NA UFANISI KWA KADA ZA CHIN KWENYE UTUMISHI WA UMMA

Hongera sana Wana-JF kwa kuona kwamba jambo hili alilolipigia kelele sasa UWEZO TUNAO pamoja na wanajamvi kibao sasa yaelekea kupenya kwenye madirisha ya jumba letu kuu Magogoni.

Mhe Kikwete, hongera zangu katika hili bado nazihifadhi mpaka nije nione jinsi gani Balozi Ombeni atakavyokamilisha jambo hili kwa manufaa yetu walipa kodi, kulinda morali ya watumishi wote, kuongeza tija kiutendaji na kuokoa kodi zetu kusiko na ulazima wa kufujisha ovyo hela za wavuja jasho.

Hata hivyo Mhe Kikwete kidoooooo umetaka kunikuna kwa kupokea CONSTRUCTIVE CRITICISMS tunazotoa hapa jamvini na kuzifanyia kazi kwa faida ya taifa letu sote.

Je kwa vyombo vya habari kweli ni lazima vyote viendelee tu kuimba CCM hata pale ambapo chama hiki hakipo jukwaani? Hebu muite kijana wako Nchimbi faragha abadilishe mwelekeo pale TBC na jinsi anavyomshinikiza Mzee Mengi kufanya visivyo kawaida yake kule ITV.

23 MARCH 2012




Rais Jakaya kikwete

*Ni baada ya kilio cha wananchi,wastaafu
*Ni kile cha kupinga nyongeza za posho zao

Na Grace Ndossa

HATIMAYE dawa ya wabunge na watumishi wengine wa umma kujipangia mishahara na marupurupu makubwa kiasi cha kulalamikiwa na wananchi, imepatikana baada ya Rais Jakaya Kiwete, kuunda Bodi ya Mishahara na Marupurupu katika Utumishi wa Umma.

Rais Kikwete ameunda bodi hiyo huku ndani ya jamii kukiwa na mvutano mkubwa wa kupinga wabunge kujiongezea posho kutoka sh. 70,000 kwa siku hadi sh. 200,000 kwa kile kilichoelezwa na Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda kwamba ni kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma ilieleza kuwa bodi hiyo itakuwa ni kwa ajili ya mishahara na marupurupu katika utumishi wa umma.

Taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu Utumishi Bw. George Yambesi, ilieleza kuwa uteuzi wa bodi hiyo ulianza tangu Februari 20, mwaka huu.

"Rais Kikwete ameunda Bodi ya Mishahara na Marupurupu katika Utumishi wa Umma na kumteua mwenyekiti wa bodi hiyo kuwa Bw. Vicenti Mrisho," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa Katibu Mkuu wa bodi hiyo ni Bi Tamika Mwakahesya wajumbe ni Bi. Assumpta Ndimbo, Bi Celina Wambura, Balozi Charles Mutalemwa, Bw.Yahya Mbila, Bw. Hussein Seif na Bw.Arthur Mwakapugi.

***Wachambuzi wa mambo

Wachambuzi wa mambo wanasema kuanzishwa kwa bodi hiyo kutasaidia kuweka uwiano sawa wa marupurupu na mishahara kwa watumishi wa umma, hivyo kuondoa malumbano kama yaliyotokea wakati Spika wa Bunge, Bi. Makinda alipothibitisha posho za wabunge kupanda kutoka sh. 70,000 hadi 200,000.

Pia baadhi ya wabunge wa vyama vya upinzani walisimama imara kupinga nyongeza ya posho hizo, hatua iliyoonesha kuwagawa wabunge.

***Msimamo wa Sumaye

Hatua hiyo pia ilimfanya Waziri Mkuu Mstaafu, Bw. Frederick Sumaye, kuongelea suala na kukaririwa na vyombo vya habari akipinga posho hizo.

Alionya kuwa nyongeza za posho zisizofuata utaratibu kwa watumishi wa umma ni hatari na ni utawala mbaya kwa nchi.

Alisema suala la posho ni jambo ambalo sasa limekuwa tatizo kwa Serikali na kuwa imefika wakati ofisi za Serikali zimehamia hotelini, lengo likiwa ni watumishi wa umma kutafuta mwanya wa kulipana posho.

"Ndiyo maana watu wa TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) wanakusanya fedha nyingi, lakini ni fedha kidogo sana zinazokwenda kwenye huduma za jamii. Nadhani hili ni tatizo na ni utawala mbaya kabisa, lazima kuwepo mabadiliko kama kweli tunataka kuisaidia nchi yetu," alisema Sumaye.

Kuhusu posho za wabunge, Sumaye alisema ni jambo la hatari kwani ikiwa wabunge watalipwa viwango vya posho vilivyotangazwa, linaweza kuvuruga amani ya nchi.

***Ndungai ajibu mapigo

Akijibu kauli iliyotolewa na Bw. Sumaye Naibu Spika wa Bunge, Bw. Job Ndugai alilifananisha posho hiyo na tone la maji ikilinganishwa na mamilioni ambayo alidai vigogo wa mihimili mingine ya dola wanalipana.

Alisisitiza kuwa posho hizo hazilingani kwa namna yeyote ile na posho wanazopewa viongozi wastaafu serikalini na wale wa Mahakama.

Alisema Watanzania wanapaswa kutambua kuwa posho wanazolipwa wabunge ni kidogo ikilinganishwa na mihimili mingine ya dola.

Alisema pia mishahara ya wabunge ni tone tu la mshahara wa ofisa wa kawaida wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Ofisa wa ngazi ya chini wa Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

"Wenzetu wa Kenya na Mauritius wana tume ambayo ni huru na ina watu ambao wanaaminika kuwa ni waadilifu, ndiyo wanaangalia mishahara ya viongozi wa juu kama hapa kwetu labda ni kuanzia kwa mkuu wa mkoa mpaka hata Rais. Ukienda kwenye mtandao unaona kila kitu, hakuna usiri, tupate chombo huru ambacho kitatupangia sisi wote ambao tunapata pesa kutokana na kodi za wananchi... nasema Watanzania wangejua maeneo mengine kukoje wangeachana kabisa na suala la posho za wabunge."

Kwa sasa inakadiriwa kuwa kila mbunge analipwa zaidi ya sh. milioni 7 kila mwezi, ikiwa ni mshahara pamoja na posho nyingine.



 
JAMANI HAYA MASHINDANO YOTE YA ULIMBWENDE WA KISIASA 'MABINTI' KUJIPITISHA OVYO JUKWANI HATA KABLA HAKUJAGOTA SAA SITA TUME YA UCHAGUZI HUKO MAGOGONI KUNANI???????????

Zitto, Lowassa, Sioi, Membe, Migiro, Lusinde, Januari, Nchimbi, Wasira na sasa hivi Sitta kila mmoja kila mmoja ANAUTAKA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;

jamani Wana-CCM tuambieni ukweli kama kiti hiki kikubwa kuliko vyote nchini kikatiba tayari kipo VACANT tangu mwaka huu 2012 wakati wengine wengi tu huku uswahilini hatuna habari.

Wenzetu tayari mnafahamu nini huko Magogoni wengine tusioijulikana kwetu? Wenzetu mumebaini kitu gani chini ya uvungu msiotuweka wazi mpaka hata wengine wakaja wakaonelea njia ya mkato ki-umri yaweza kutoa jibu la mapema?

Enyi ndugu zetu wachambuzi wa mambo ya siasa nchini, dalili zote hizi si za bure wala wa kupuuza hivi hivi hebu katudadavulieni haraka, kiundani zaidi na bila kupapazapapazi kitu hapo.
 
BAVICHA SASA KIPENGA PIEEEEEEEEEEE MPAKA USHINDI MURUA WA HAKI NA UTETEZI WA UTU WA KILA MTANZANIA UPATIKANE BILA ZENGWE ARUMERU MASHARIKI TANGU SASA!!!!!!!!!!!!!

Askari wetu wa miavuli BAVICHA,

katika hii wiki ya lala salama Arumeru ni vema kuliko kawaida 'Dozi ya Siasa za Kistaarabu' mkanyunyiza mtindo wa Igunga kutwa mara tatu kufikisha ujumbe wa ukombozi katika kila lango la kila mpiga kura katika kila kijiji jimboni hapo na hatimaye kuhitimisha kwa mkakati wa kufa mtu katika kudhibiti usalama wa kila kura itakayopigwa siku hiyo.

Kamanda Heche tunahitaji kuona organisation skills na usimamizi wa kitimu kwa kushirikiana kwa karibu sana na machalii wote wa Arumeru Mashariki (kama Kamanda Vincent Nyerere tangu alivyofanikiwa na msaidizi wake Mchungaji) tangu sasa.

Kipenga pieeeeee, pipoz pawaaaaa mpaka ushindi kuubeba mbeeeele kama tai huku sote tukishirikiana kwa kila hali kila mahali na kila waka!!!!!!!!!
 
... Wananchi wenzangu, tukimuona mtu anapenda sana nyimbo mdomoni za kukimbilia ikulu na hata wakati mwingine mtu huyo kuanza kutumia tumia VIJISENTI visivyojulikana wazi vyanzo vyake kurubuni watu kushoto kulia;

huku akijipitishapitisha ovyo kama malimbwende majukwani wakati wote na hata kupewa msukumo na vikundi vyenye historia ya kuibua maswali mengi kuliko majibu katika jamii;

MTU HUYO HATUNA BUDI WALALAHOI WA NCHI HII SOTE KUMUOGOPA KAMA UKOMA
maana biashara inayomkimbiza ovyo huko hakuna hata mmoja wetu anayeifahamu.

Angalizo ni kwamba WaTanzania tusipozingatia tahadhari kubwa tunazozawadiwa na chemuchemu hizi za busara adimu na ha kihistoria nchini basi sote tusisahau kwamba matokeo yote MAJUTO NI MJUKUU mwisho wa yote.
 
CHADEMA ni muhimu wakati wote kuendelea na mpangilio rasmi wa mbinu mbali mbali za kukijenga chama toka hatua moja hadi nyingine BILA KURUHUSU SIDESHOWS za CCM na au VIRUSI vyake ndani ya chama kuazima sikio lenu hata kwa sekunde moja kwa jambo lolote lisilokuepo kwenye ya wakati uliopo.

Badala yake, ni jambo la msingi CDM kuunda mashine kubwa zaidi itakayojulikana kama RAPID RESPONSE TEAM itakayotumia to CONTIGENCY APPROACHES to ISSUE (NOT HULLABALOOS) as they emerge basing on the strengths of utmost selectivity.

The composition of such a team can be both vitual and physical, but of a relatively smaller number carrying cream of diverse knowledge base; a think-tank on issues.

Haya twendeni sasa sawa.
 
Enyi MAFISADI wote pamoja na chama CCM eleweni hili vema na kwa uwazi wake wote, ukweli wote ni kwamba;

... WaTanzania sote TUMESHAAMUA kwamba mambo yote ya ukombozi wa MTANZANIA kuondokana na MAFISADI ni kwa CHADEMA.

Je ni nani tena wa kutuzuia?????????????
 
Back
Top Bottom