The Rise and Fall of Marcio Maximo...Discuss.

CECAFA imetuonyesha MAXIMO ni nani, WaTZ mnasemaje? Hii sio aibu ya nchi? Uzalendo na nidhamu anavyotoa kama vigezo vya kuwakataa wachezaji hawa mbona yeye vimemshinda? Ni jana tu amelimwa barua ya utovu wa nidhamu na CECAFA. Kocha gani huyu mhuni. Mie binafsi nimemuona kwenye TV baada ya mechi na RWANDA akimshambulia wazi wazi kwa matusi kocha wa Rwanda. Je, kocha wa Rwanda alikuwa anacheza au alikuwa Refa. Mpira umeisha matokeo yamipatikana kutokana na maelekezo yake au aina ya uchezaji alitaka. Sio hapo tu TZ ni timu iliyoonyesha nidhamu ya hali ya chini sana. Kufunga kumechangiwa na kuwa na wachezaji pungufu kutokana na wachezaji kutojua kuwa makosa au rafu zisizo na maana uwanjani zinaigharimi timu. Haya kila mechi TZ walikuwa wakimaliza mpira wakiwa pungufu. Jamani mnakubali kuwa refs walikuwa wanatuonea kama sio reflection ya quality ya COACH. PIMA NA TOA UAMUZI.

Kama ni swali - jibu lake ni MAXIMO.
 
Mh!!!!!! hapo dhairi mnataka kumchokoza Mkulu mimi simo! mnajua wazi mkulu anampenda sana Max, kubwa zaid yeye ni mnazi wa young sasa mnaanza kumfananisha na phiri! ingawa ukweli ni kwamba Phiri ni zaidi!
young
 
JF wanasoka,

Majority wanasema hata kuwaringanisha hawa ni kitu ambacho hakipo kabisa sasa najiuliza maswali yafuatayo

1. Hiyo TFF haioni tatizo hili? je hatuna wataalamu wa ufundi kubaini tatizo?
2. Joe Bendera ulishawahi kuwa kocha wa taifa, hata wewe pia hulioni tatizo
hili?
3. Tactics ni mbovu hasa defensive, Tenga ulikuwa Central defender, Je pia hujagundua tatizo la kiufundi la timu hii? kama timu inafanya vibaya kwa kwanza kupewa lawama ni nani? Kocha, Rais wa TFF au aliyomtafuta na kumpa ajira huyu jamaa au wachezaji wenyewe?

Imefikia hatua watu wanasema hii si timu ya TAIFA ni timu ya MAXIMO.

OMBI

Kwa kuwa huyu jamaa hana jipya aondoke atuachie timu yetu wenyewe, kama njaa kashanganga vya kutosha. tunaomba aondoke wa heshima tu laa asubiri kitakachofuata.

Tuna imani tunaweza kuliko kuwa na kocha MSHIRIKINA kama huyu, hatufai kwa lolote, majungu tu utadhani kakulia Tandare kwa bi nyau.

Walio mleta nchini chukueni mzigo wenu huo umetushinda kuubeba - HAUBEBEKI. kama contract ataimalizia kwao brazil.
 
Tuna imani tunaweza kuliko kuwa na kocha MSHIRIKINA kama huyu, hatufai kwa lolote, majungu tu ka kakulia Tandare kwa bi nyau.

Walio mleta nchini chukueni mzigo wenu huo umetushinda kuubeba - HAUBEBEKI. kama contract ataimalizia kwao brazil.
Mshirikina tena? duuh! unahasira inaonyesha ukikutananae mitaa furani unampa za chembe teh teh
 
..Kwa nini Simba isingewakilisha Tz kwenye challenge lazima wangerudi na kombe!!! Phiri yuko juu!!..utawasikia sasa hivi wale wa homa ya manjano!!!!!!!!!!!!!!
simba ingewakilisha vp Tz wakati yenyewe ni klabu yenye wachezaji kutoka Uganda na nchi nyinginezo, mkuu vikilia kwanza kabla hujamwaga maoni...... kwa busara na hekima maximo aachie ngazi amuachie mwingine na kama tatizo sio yeye tutaliona coz ameifundisha timu kwa muda mrefu sasa, kuna uwezekano mkubwa hakuna jipya atakaloliongeza zaidi ya kuhangaika jinsi ya kuweka mambo sawa,...its tym 2 go now max!
 
Nyie acheni unazi bwana, miaka kadhaa iliyopita hakuna hata aliyekuwa akijishughulisha na timu ya taifa....tena kuna wengine walikuwa wakitabiri kufungwa kabla hata timu haijaingia uwanjani....nasema mwacheni afanye anavyoweza.

Kwanza mlishajiuliza akitoka maximo atakuja nani? Huyo mzirai anaesambaza fitina yuko hoi bin taabu atuonyesha basi kwanza kwa soka la wadada limefikiwa wapi. Mnanikera sana mnaojifanya mmemchoka kocha maximo. Jengeni uvumilivu na subra eboo! Nyie mliona wapi mtu katoka jela tu anaanza kujenga majumba au kutanua na mihela kibao.

Nasema tena mwacheni kocha maximo afanye kilichomleta nacho ni kujenga soka la tanzania, leo wapo watu wanatamani kushuhudia japo mazoezi ya timu ya taifa wakati zamani ilikuwa kichekesho kutaja neno taifa stars. UKWELI UNABAKI PALE PALE MAXIMO BADO ANAHITAJIKA SANA NCHINI KWENU....mkiweza tutajie mbadala wake. Mnataka kuleta haditth za Riki Abadalah na takwimu za intaneti.
 
Jee huyu mtangazaji wa michezo wa kimataifa wa Redio 1 Abdulmuhammed anaubia na Maximo? Kwani imekuwa kawaida ktk kipindi chake cha michezo akimtetea na akisema hafai kulaumiwa. sasa kama yeye maximo hafai kulaumiwa nani wa kulaimiwa ktk timu yetu ya taifa?

Rafiki yake sana kawaida huwa wanacheki naye Premiership na UEFA games nyumbani kwa Maximo tena kwenye nyumba tunayomlipia sisi walipa kodi, huko ndiko anamharibu kwa kupika majungu.
 
Jee huyu [COLOR="Blue"[/COLOR]wa Redio 1 Abdulmuhammed anaubia na Maximo? Kwani imekuwa kawaida ktk kipindi chake cha michezo akimtetea na akisema hafai kulaumiwa. sasa kama yeye maximo hafai kulaumiwa nani wa kulaimiwa ktk timu yetu ya taifa?
...Mtangazaji wa kimataifa??!!!
 
Nyie acheni unazi bwana, miaka kadhaa iliyopita hakuna hata aliyekuwa akijishughulisha na timu ya taifa....tena kuna wengine walikuwa wakitabiri kufungwa kabla hata timu haijaingia uwanjani....nasema mwacheni afanye anavyoweza.

Kwanza mlishajiuliza akitoka maximo atakuja nani? Huyo mzirai anaesambaza fitina yuko hoi bin taabu atuonyesha basi kwanza kwa soka la wadada limefikiwa wapi. Mnanikera sana mnaojifanya mmemchoka kocha maximo. Jengeni uvumilivu na subra eboo! Nyie mliona wapi mtu katoka jela tu anaanza kujenga majumba au kutanua na mihela kibao.

Nasema tena mwacheni kocha maximo afanye kilichomleta nacho ni kujenga soka la tanzania, leo wapo watu wanatamani kushuhudia japo mazoezi ya timu ya taifa wakati zamani ilikuwa kichekesho kutaja neno taifa stars. UKWELI UNABAKI PALE PALE MAXIMO BADO ANAHITAJIKA SANA NCHINI KWENU....mkiweza tutajie mbadala wake. Mnataka kuleta haditth za Riki Abadalah na takwimu za intaneti.

Yawezekana Maximo anafaa kufundisha Kabumbu, lakini hadhi yake siyo ya Kocha wa Timu ya Taifa bali angefaa zaidi kama angeenda sehemu kama Shule ya Makongo hivi ambapo angepata fursa ya kufundisha tu pasipo kuhitajika keshinda vikombe. Kocha wa Timu ya Taifa au Timu inayoshiriki ligi ufanisi wake unapimwa kwa vikombe na siyo kufukuza wachezaji kwenye Timu. Kama ni nidhamu nayeye ameonyesha kutokuwa nayo kiasi cha kupelekea kuonywa na CECAFA.

Kimsingi Maximo hastahili kuinoa Timu yetu, ila tu bahati mbaya iliyopo ni kwamba ni Mwajiriwa wa Mkuu wa Kaya sasa TFF inawawia vigumu kumtupia virago.
 
Yawezekana Maximo anafaa kufundisha Kabumbu, lakini hadhi yake siyo ya Kocha wa Timu ya Taifa bali angefaa zaidi kama angeenda sehemu kama Shule ya Makongo hivi ambapo angepata fursa ya kufundisha tu pasipo kuhitajika keshinda vikombe. Kocha wa Timu ya Taifa au Timu inayoshiriki ligi ufanisi wake unapimwa kwa vikombe na siyo kufukuza wachezaji kwenye Timu. Kama ni nidhamu nayeye ameonyesha kutokuwa nayo kiasi cha kupelekea kuonywa na CECAFA.

Kimsingi Maximo hastahili kuinoa Timu yetu, ila tu bahati mbaya iliyopo ni kwamba ni Mwajiriwa wa Mkuu wa Kaya sasa TFF inawawia vigumu kumtupia virago.

Nimekusoma Mkuu, huo ndo ukweli Halisi.
 
Maximo mwisho atagombea ubunge tu hapa bongo..


Siyo kugombea atateuliwa kwenye zile nafasi 10 za Mkuu wa Kaya ili akawe mshauri wa masuala ya michezo. Na afadhali ingekuwa hivyo ili aiache wazi nafasi ya Ukocha wa Timu ya Taifa maana inavyoonyesha Tenga na TFF yake wamefyata mkia katika hili, kwani shida iko wapi kwao wakati mkwanja unatiririka kwenye mifuko yao.

Ingewezekana kufanya maandamano kwenye mtandao ingekuwa raha kweli ili tumuonyeshe Mkuu wa Kaya kwamba huyo Mshikaji wake Max anatukwaza na kutukera kwelikweli.
 
Waungwana, hivi huyu Maximo ni hakuna halichotufanyia watanzania au tulikuwa tumeweka IMANI KUBWA SANA KWAKE. Nadhani tujaribu kuangalia mahali alipotukuta ndipo tulipo? kama jibu ni ndiyo BASI HANA JIPYA, kama jibu ni hapana, je ametusogeza mbele au ameturudisha nyuma. nadhani kama ameturudisha nyuma basi hana sababu hata ya kuaga ni kuchapa lapa kwa kwenda mbele kama ametusogeza mbele basi tunayo sababu ya kuangalia hiyo hatua utuliyosogea tulistahili kwa hiyo hatua au la. Haisaidii kila siku kuhoji swala la kaseja, boban na chuji kuwezpo stars, sitaki kuamini kwamba matokeo mabaya inayoyapata stars ni kukosekana kwa hao wachezaji watatu. Naamini kila kocha anachagua wachezaji kutoka na mfumo anaotaka kuutumia, na vilevile hakuna kocha ambaye atachagua wachezaji ili timu ikose ushindi.
Tujaribu kunyoosha vidole kwenye vilabu vyetu kwanza, vipi mafanikio ya vilabu vyetu katika michezo ya kimataifa? Kama vilabu havifanyi vizuri sidhani kama timu ya taifa itafanya vizuri kwani ndio hao hao wacheza tutakaokuwa nao kwenye national team.
 
Back
Top Bottom