1. Katika kipindi hiki tumeshuhudia sheria zikivunjwa na viongozi wetu wazi wazi na watuhumiwa wasichukuliwe hatua, eti ushahidi hautoshi.
2. Raisi anapounda serikali na kuteua viongozi, sasa ikionekana dhahiri kabisa mbele ya umma kuwa wanaboronga - halafu asite kuwatimua, eti anasubiri ushahidi au uamuzi wa mahakama - kwani mahakama zilimshauri katika kuwateua ?
3. Ni wazi hapa anasukumwa na dhamira moja tu nayo ni kulinda maslahi ya marafiki na wabia wake ndani ya chama na serikali - huu ni ukosefu wa nia na ujasiri.
4. Tanzania inaangamia kwa kuwa maslahi ya wachache yamewekwa mbele ya maslahi ya taifa na watu wake.
5. Chama chochote kile kinachoendeleza dhana hii ya kijinga, hakitufai.
6. Watanzania tuamke - we have been taken for a ride for too long !!
7. Serikali inaonekana imeelemewa na inahitaji msaada wetu. Gari limekwama na dereva ujanja umemwishia, tushuke, tulisukume na tuliondoe kwenye tope.
swali langu ni kuwa tuhuma dhidi ya Chenge na Dr. Idris ni kubwa mno. Ni kubwa kiasi cha kutisha. Sasa kinachongojewa ni nini?
Hivi SFO wakisema hawawashtaki na sisi tusiwashtaki?
Kwanini tusiamue kufuta tu makosa yote ya nyuma tuanze na ukurasa mpya?
Kinachoweza kuwabadilisha watu ni kusimamisha sheria...
Sisi sote ni reflection ya viongozi wetu kwa sababu sheria zetu ni butu, lakini kama tunaweza kuchukia Ufisadi kama tunavyochukia vibaka wa Kariakoo basi bila shaka wananchi wote kwa ujumla tutabadilika...
Ni kweli kabisa kuwa hujuma yoyote dhidi ya uchumi wa Taifa huitwa ujanja..ni sifa kubwa kuvuta deal serikalini ukifahamu kwamba nyayo zako ziko covered na sheria butu.
Mimi nina hakika kabisa kusimamisha sheria ndio msingi wa mienendo ya binadamu wote..maneno matupu na viapo kuwa rushwa ni adui wa haki - sintatoa wala sintapokea rushwa ni hadithi tupu kama hakuna sheria na utamaduni unaofikisha ujumbe huu kwa wananchi wote...Na kwa bahati mbaya CCM wamekuwa mbele kuweka ubani kufukiza azimio lao la Zanzibar...
Mnategemea nini kama kiongozi wa chama mtu kama Makamba anayekuja wambia wananchi wake kwa ujeuri na majigambo kuwa chama ni safi isipokuwa kuna baadhi ya watu ndio wachafu wakati mwongozo wa chama chake unasisitiza kuwa:-
"Kiongozi wa CCM katika kukijenga na kukilinda Chama ni kubwa. Athari katika Chama za Kiongozi kutenda maovu, au kutotimiza wajibu, ni kubwa kiasi kwamba Maadili yake yakitetereka Chama kitavurugika; na nchi itakwenda mrama."
swali langu ni kuwa tuhuma dhidi ya Chenge na Dr. Idris ni kubwa mno. Ni kubwa kiasi cha kutisha. Sasa kinachongojewa ni nini?
Hivi SFO wakisema hawawashtaki na sisi tusiwashtaki?
Kwanini tusiamue kufuta tu makosa yote ya nyuma tuanze na ukurasa mpya?
Kwa hali ilivyo hapa nchini kuna haja ya kutathmini role ya Moral institutions katika kujenga jamii staarabu nchini kwetu, hasa kwa kuangalia dini zetu kuu yaani ukristo na uislamu.Mkuu Mwenzangu FMES,
Nchii ilianza kuangakuka Pale viongozi walipoamua kuwa matajiri kupitia Vyeo vyao walivyopewa. Dhambi hii ilianzishwa na wachache na wengine wakaamua kuifuata kwa kuogopa kuchekwa wakimaliza uongozi wao serikalini. Serikalini hakuna Maadili hata kidogo, kila mtu anajiona yeye ana uwezo wa kimaamuzi kuliko mtu yeyote.
Nchi ilianza kupotea pale Wafanyakazi wa Umma waliopoanza kuajiriana kutokana na ukabila,Udini na ukanda. Hii ilichangai kuvunja maadili na miiko ya Uongozi sababu kila mtu ana mtu nyuma yake... Hata Masha ana mtu nyuma yake kwa sasa!
Watu wa kulaumiwa katika hili,mmoja wapo na Mamvi nd ndiyo maana Mwalimu alikuwa akimpinga,Huyu ndiye aliyeonesha kuwa unaweza ukawa Tajiri kupitia Uongozi.Kinachoniuma ni hawa wachungaji na maaskofu kumkumbatia huyu mwenye historia chafu na asliyeshindwa kujisafisha mbele ya Mwalimu na waumini wote wa kitanzania.
Nakubaliana na maneno ya Zitto Kabwe kuwa Kunahitajika suluhisho la kitaifa katika mambo yahusuyo Nchi hii na wala siyo chama cha siasa.
Mzee Mwanakijiji umenena!
nilikuwa najiuliza tu,hivi kizazi hiki chote kitakuja kutoweka? halafu tutaacha wengine nyuma? nao watakuwa hivihivi? basi hii biashara kichaa kabisa.