The Radar Scam: Chenge & Rashid...

Invisible

Robot
Feb 11, 2006
9,075
7,878
Japo kuna topic zinaendelea nimeonelea niiweke hii hapa ili kuona wadau kama inaweza kuwa na msaada kwenu. Hebu ipitieni kidogo tu.

Thanks
 

Attachments

  • RadaDeal.zip
    432.2 KB · Views: 479
Asante mkuu invisible. Huu ni ushahidi tosha kabisa wa kuwapandisha mahakamani wahusika.
 
Ahsante sana mkuu hapa naona Idriss hatakuwa na cha kujitetea maana kuna ushaidi wa kutosha sasa
 
Du mkuu Invisible hii si mchezo, ni kweli kuwa nchi inajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye meno a.k.a chenge & Co.
 
- Wakuu ahsanteni sana kwa hii response, Tanzania tumetokewa na nini hasa? I mean tumefikaje hapa jamani ambapo hakuna wa kumuamini? Mimi sasa nimefikia mahali mtu akitaka kunikopa na ni rafiki yangu wa karibu, kama anataka 100, nitampa 50 na kumuomba asinirudishie ili tuendelee na urafiki wetu maana nikimdai tutavunja urafiki.

- Kweli kiongozi mkubwa wa taifa anatafuta risiti za uongo ili akadai hela za wananchi, na huku akijua wazi kuwa anachokifanya ni uizi? Unajua tumefikia mahali huu sasa nationally ya kutafuta risiti yamekubalika kuwa ni tabia ya kawaida tu kwa sisi wafanyakazi wa serikali yetu, wakubwa kwa wadogo bila hata ya aibu kidogo!

- Hatuwezi kuaminiana tena, hatuwezi hata kujali time maana tutatafuta sababu za hapa na pale na kudai tulikuwa na shughuli zilizotufanya tuchelewe kumbe ni uongo uongo usio na mfano. Ninakumbuka nilipokuwa nchi moja majuu, ilikuwa mbongo ukitaka kununua tiketi ya ndege, mhindi mmoja alikuwa na tiketi za cheap kwa hiyo wabongo wengi tulikuwa tunajimwaga huko, sasa hata yule Mhindi alishatushitukia I mean mbongo anapiga simu kuwa anaondoka Jumapili kumbe hata hela hana anategemea kupata Ijumaa jioni, atamzungusha Mhindi mpaka mwisho ataanza kujizungusha mwenyewe, matokeo safari hakuna analaumu Mhindi kumbe ni uongo tu umemzidi!

- Unajua ninashukuru sana kwa wale wote mliolichukulia hili suala on a serious note, wakuu sisi tunao-deal na wabongo kila siku kwa kweli hamjui how bad this thing are, sasa ninajiuliza kama sisi wenyewe kwa wenyewe ni hivi mazishi mazishi hawa viongozi wetu itakuwaje na wako kwenye nafasi na wanaziona hela ziko nje nje?

Wakuuu solution nini hasa na hili tatizo na sisi wabongo? Tumefikaje hapa? Hili taifa letu litakombolewa na nani hasa jamani kama sisi wenyewe ndio hivi hivi? Something ni lazima kifanyike jamani ama sivyo tutacheza mzunguko mpaka mwisho wa dunia ndugu zangu! Unajua yanakatisha tamaa sana huko uongozi wa juu, maana tulisema wakiingia wapya na hasa vijana mambo yatabadilika, kumbe sasa ndio worse kuliko zamani, ni nini hasa sisi na hiii special Tanzania's character?

Ahsante Wakuu
!
 
1. Katika kipindi hiki tumeshuhudia sheria zikivunjwa na viongozi wetu wazi wazi na watuhumiwa wasichukuliwe hatua, eti ushahidi hautoshi.

2. Raisi anapounda serikali na kuteua viongozi, sasa ikionekana dhahiri kabisa mbele ya umma kuwa wanaboronga - halafu asite kuwatimua, eti anasubiri ushahidi au uamuzi wa mahakama - kwani mahakama zilimshauri katika kuwateua ?

3. Ni wazi hapa anasukumwa na dhamira moja tu nayo ni kulinda maslahi ya marafiki na wabia wake ndani ya chama na serikali - huu ni ukosefu wa nia na ujasiri.
4. Tanzania inaangamia kwa kuwa maslahi ya wachache yamewekwa mbele ya maslahi ya taifa na watu wake.

5. Chama chochote kile kinachoendeleza dhana hii ya kijinga, hakitufai.

6. Watanzania tuamke - we have been taken for a ride for too long !!

7. Serikali inaonekana imeelemewa na inahitaji msaada wetu. Gari limekwama na dereva ujanja umemwishia, tushuke, tulisukume na tuliondoe kwenye tope.

- Mkuu haya maneno ni mazito sana na hkuna ubishi kabisa, sawa sawa na tupo pamoja hapa.
 
Kinachokatisha tamaa zaidi ni kuwa hata wale wazalendo wachache waliopo........wanawekwa pembeni/kufukuzwa...........au wanapewa sehemu ambazo they can not perform............

Jambo la kufanya

.....kwa kuwa MAFISADI ni network.....na hata sasa hivi wanapandikiza watoto wao na ndugu zao.......cha msingi sisi tunaoona haya maovu......tujiunge na tu-form namna ya ku-fight na huu upuuzi........chombo kimojawapo cha kupambana nao tunavyo i.e. JF+ Cheche za Fikra........hivyo basi tuongeze nguvu
 
..inawezekana Dr.Rashidi na Chenge ni wanamtandao. ikiwa hivyo Raisi huyu tuliyenaye hawezi kuwachukulia hatua.

..halafu na sisi wananchi tukubali kwamba tulichukuliwa msukule na wanamtandao.

..kinachotokea sasa hivi ni sawa na mtu anayekurupa kutafuta shuka wakati majogoo yanawika.
 
Duhhh,

.....kweli kabisa sijui Chenge na Rashidi kwa nini mpaka sasa hivi ni viongozi.......tunataka kusikia nao wamefikishwa Kisutu kwa Hakimu Hezron.........
 
swali langu ni kuwa tuhuma dhidi ya Chenge na Dr. Idris ni kubwa mno. Ni kubwa kiasi cha kutisha. Sasa kinachongojewa ni nini?

Hivi SFO wakisema hawawashtaki na sisi tusiwashtaki?

Kwanini tusiamue kufuta tu makosa yote ya nyuma tuanze na ukurasa mpya?
 
swali langu ni kuwa tuhuma dhidi ya Chenge na Dr. Idris ni kubwa mno. Ni kubwa kiasi cha kutisha. Sasa kinachongojewa ni nini?

Hivi SFO wakisema hawawashtaki na sisi tusiwashtaki?

Kwanini tusiamue kufuta tu makosa yote ya nyuma tuanze na ukurasa mpya?

Mwanakijiji,

Muamue na nani?au waamue wao..Mara ngapi tumewaeleza hawataki kusikia..

Tatizo ni viongozi wengi tulionao wameingia madarakani kwa pesa ya Rushwa hivyo hawawezi kuwafunga wenzao kwa kesi ya Rushwa
 
Wapo kwa sababu watawala wengine wanafanana nao.Huwezi kuchukuliana na mwovu kama wewe sio mwovu!

toleola25.jpg
 
Kinachoweza kuwabadilisha watu ni kusimamisha sheria...
Sisi sote ni reflection ya viongozi wetu kwa sababu sheria zetu ni butu, lakini kama tunaweza kuchukia Ufisadi kama tunavyochukia vibaka wa Kariakoo basi bila shaka wananchi wote kwa ujumla tutabadilika...
Ni kweli kabisa kuwa hujuma yoyote dhidi ya uchumi wa Taifa huitwa ujanja..ni sifa kubwa kuvuta deal serikalini ukifahamu kwamba nyayo zako ziko covered na sheria butu.

Mimi nina hakika kabisa kusimamisha sheria ndio msingi wa mienendo ya binadamu wote..maneno matupu na viapo kuwa rushwa ni adui wa haki - sintatoa wala sintapokea rushwa ni hadithi tupu kama hakuna sheria na utamaduni unaofikisha ujumbe huu kwa wananchi wote...Na kwa bahati mbaya CCM wamekuwa mbele kuweka ubani kufukiza azimio lao la Zanzibar...

Mnategemea nini kama kiongozi wa chama mtu kama Makamba anayekuja wambia wananchi wake kwa ujeuri na majigambo kuwa chama ni safi isipokuwa kuna baadhi ya watu ndio wachafu wakati mwongozo wa chama chake unasisitiza kuwa:-

"Kiongozi wa CCM katika kukijenga na kukilinda Chama ni kubwa. Athari katika Chama za Kiongozi kutenda maovu, au kutotimiza wajibu, ni kubwa kiasi kwamba Maadili yake yakitetereka Chama kitavurugika; na nchi itakwenda mrama."

Umeongea Mkandara, nchi tunaweza kuimba sana kuwa tunafuata utawala wa sheria lakini ni usanii mtupu. Mifano, ikionekana sheria itamuumiza mkubwa ndio unasikia statement za "leteni ushahidi", hivi Chenge alipotuhumiwa tu kuwa ana mamilioni ameficha nje sijui kama kuna wahusika walienda hata kuchungulia tume ya maadili kama ame-declare utajiri wake.

Mfano mwingine ambao huwa unachochea sheria kuwekwa kando na maslahi ya wakati kuwa muhimu ni wakati wa kukaribia uchaguzi utasikia viongozi wa CCM wakikemea viongozi serikalini wasije wakatekeleza wajibu wao kama kuhamisha machinga etc...wakiongopa kukosa kura. Kwa maslahi ya chama na watu wachache ni bora hata kama sheria zitapindwa. Hii imejijenga sana kwa wananchi kiasi kwamba sasa mtu ukisimamia sheria unaonekana mbaya na una roho mbaya tu.

Well, huu ni mzizi uliopandwa kwa muda mrefu na itahitaji kujitoa kweli kweli ili watu wanyoke.
 
swali langu ni kuwa tuhuma dhidi ya Chenge na Dr. Idris ni kubwa mno. Ni kubwa kiasi cha kutisha. Sasa kinachongojewa ni nini?

Hivi SFO wakisema hawawashtaki na sisi tusiwashtaki?

Kwanini tusiamue kufuta tu makosa yote ya nyuma tuanze na ukurasa mpya?

Ajali kazini. Uongozi wa wa JUU WA serikali ya CCM na CCM yenyewe kwa kua kwa ujumla wao karibu wote wameoza wanaona kama walichofanya Chenge na Rashidi ni halali, lakini imetokea ajali ndogo - yaani bahati mbaya.
Kuiangusha CCM ndio itakua hatua ya kwanza kubadili yote haya. CCM wana kiburi cha kutawala muda mrefu kiasi kwamba hawaoni mbali na pua yao. Inawezekana hata chama KITACHOCHUKUA MADARAKA kimeambukizwa ugonjwa wa CCM, lakini tutaendelea kubadili chama tawala mpaka tutapata chama SAFI.
CCM walipata ridhaa ya kutawala kwa 80%, kimsingi ina maana wanapendwa sana hata tukidai waliiba kura wala haisaidii. Njoo tushirikiane kung'oa CCM, hio ndio dawa. Njia zingine km kupindua, ama Jeshi kuingilia nk zimepitwa na wakati na zinaleta mateso zaidi kwa raia. Usikose kupiga kura.
 
Mkuu Mwenzangu FMES,

Nchii ilianza kuangakuka Pale viongozi walipoamua kuwa matajiri kupitia Vyeo vyao walivyopewa. Dhambi hii ilianzishwa na wachache na wengine wakaamua kuifuata kwa kuogopa kuchekwa wakimaliza uongozi wao serikalini. Serikalini hakuna Maadili hata kidogo, kila mtu anajiona yeye ana uwezo wa kimaamuzi kuliko mtu yeyote.

Nchi ilianza kupotea pale Wafanyakazi wa Umma waliopoanza kuajiriana kutokana na ukabila,Udini na ukanda. Hii ilichangai kuvunja maadili na miiko ya Uongozi sababu kila mtu ana mtu nyuma yake... Hata Masha ana mtu nyuma yake kwa sasa!

Watu wa kulaumiwa katika hili,mmoja wapo na Mamvi nd ndiyo maana Mwalimu alikuwa akimpinga,Huyu ndiye aliyeonesha kuwa unaweza ukawa Tajiri kupitia Uongozi.Kinachoniuma ni hawa wachungaji na maaskofu kumkumbatia huyu mwenye historia chafu na asliyeshindwa kujisafisha mbele ya Mwalimu na waumini wote wa kitanzania.

Nakubaliana na maneno ya Zitto Kabwe kuwa Kunahitajika suluhisho la kitaifa katika mambo yahusuyo Nchi hii na wala siyo chama cha siasa.

Mzee Mwanakijiji umenena!
Kwa hali ilivyo hapa nchini kuna haja ya kutathmini role ya Moral institutions katika kujenga jamii staarabu nchini kwetu, hasa kwa kuangalia dini zetu kuu yaani ukristo na uislamu.
Katika ukristo nchi hii ina madhehebu makubwa mawili, wakatoliki na walutheri, kwa kifupi madhehebu haya yameshindwa vibaya ktk kuandaa watu wzr kwa jumuia zetu, wote wanaotuhumiwa kwa wizi na matumizi mabaya ya madaraka ni wakatoliki na walutheri, ni aibu kwa makanisa haya!!!! ndio maana wengine wanaona heri kusimama kuwatetea, inakuwaje muumini wenu anakuwa mwizi wa mali ya umma tena akiwa kiongozi??????
Kwa upande wa waislamu kwa kweli wanashika kile wanachokiamin vzr, ndio maana si rahis kukuta viongozi toka zanzibar wanatuhumiwa kwa wizi!!! ni watu wanyenyekevu wasio na tamaa, waangalie kina dk Shein, Salmin, marehemu dk. omar ali juma nk
Yapo madhehebu mengine ya kilokole (Pentecostals) hawa ni wazuri pia.pengine ipo haja ya kuwauliza walutheri na wakatoliki kuwa kwa nini wanaendelea kukumbatia watu wanaotuhumiwa kwa wizi makanisani kwao???
Labda wakifanya kama wpentecoste wanaowatenga waumini pale anapotuhumiwa kwa kosa lolote inaweza kusaidia kuwa na watu wema ktk jamii yetu, hasa viongozi!!
 
nilikuwa najiuliza tu,hivi kizazi hiki chote kitakuja kutoweka? halafu tutaacha wengine nyuma? nao watakuwa hivihivi? basi hii biashara kichaa kabisa. Ukianza biashara ukaproject hasara, kuna sababu ya kufanya hiyo biashara? labda kama mtaji ni wa EPA, kwa hiyo unazuga tu. Mimi sijui tunavumiliana saaaana mpaka lini? Chenge na mwenzake wameiba? sasa tatizo nini? mahakama kumbe ni kwa ajili yetu sisi tu, na jela je? Sijui kizazi kijacho kitarithi nini, kama kabla ya kufa ni lazima tuiharibu kabisa Tanzania ili watakaokuja wasiikute, Mungu atusamehe.. labda hatujui tutendalo? sote tuone aibuuuuuuuu, kama hatufanyi lolote, shame, shame on us all, kwani jk ni nani, na huyu Lowasa ndio nani? kwani wao ni watz kuliko sisi wengine wote, kwa kuwa wanamimvi kichwani? tusibabaishane bwana,wote ni watanzania, ila wametuona sisi wadanganyika eeh, wakija tunawekenulia meno kama vile hakuna kilichotokea tuone aibuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu.
 
nilikuwa najiuliza tu,hivi kizazi hiki chote kitakuja kutoweka? halafu tutaacha wengine nyuma? nao watakuwa hivihivi? basi hii biashara kichaa kabisa.

- Sawa sawa, hapa tupo pamoja sana, hili nalo ni swali la msingi sana tutaacha nini nyuma yetu? Eti watoto wetu watakuwa tofauti na sisi?

- Wasomi na wanadini, ni wakati muafaka sasa wakatafakari na kutuelimisha ni wapi tulikose akwenye hili, kwa sababu tabia zote nzuri za Mwalimu tunazo, kuanzia umasikini jeuri mpaka elimu za kubobea,

Sasa hizi tabia tabia tumeziota wapi mbona Mwalimu hakuwa nazo?


?
 
Kama kuna vikundi ambavyo vinatuangusha kwenye hii vita - ni vikundi vya dini. Inakatisha tamaa viongozi fulani fulani wa dini wanapojitokeza mbele ya hadhara na bila aibu kuyakumbatia na kuyatetea haya majizi - eti mradi wanachangia mifuko yao ya ulaji.

Sasa ni wakati muafaka tuanze kwa kuwaelekezea vidole na bila kumun'gunya maneno kuwaambia waache mara moja kutumia dini kama sabuni ya kuyafulia haya majambazi. Hii vita lazima ipigwe kwa kutumia zana na mbinu zote kama tunataka kufanikiwa.

Kamwe tusikubali hawa wezi watumie makanisa ama misikiti kama viwanda vya kusafisha (launder) pesa zao chafu. Tumeshuhudia wengi wakienda kutafuta hifadhi huko baada ya umma kuamua kuwazomea na kuwatenga. This has to stop now.
 
Back
Top Bottom