The New Dr Shein's Cabinet

Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Vifungu 42 (1) na (2), 43 (1) na (2) na 47 vya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein ameunda Wizara 16 na kuwateua Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi, Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:

1. Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi-
Mhe. Dr. Mwinyihaji Makame

2. Ofisi ya Rais (Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo)

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Fedha, Uchumi, na Mipango ya Maendeleo)
Mhe. Omar Yussuf Mzee

3. Ofisi ya Rais, (Utumishi wa Umma na Utawala Bora)-

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi wa Umma na Utawala Bora)
Mhe. Haji Omar Kheri

4. Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais
Mhe. Fatma Abdulhabib Fereji.

5. Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais-

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais
Mhe. Mohammed Aboud Mohammed

6. Wizara ya Katiba na Sheria

Mhe. Aboubakar Khamis Bakary.

7. Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano

Mhe. Hamad Masoud Hamad

8. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali

Mhe. Ramadhan Abdulla Shaaban

9. Wizara ya Afya

Mhe. Juma Duni Haji

10. Wizara ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Wanawake na Watoto

Mhe. Zainab Omar Mohammed

11. Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo

Mhe. Abdilahi Jihad Hassan

12. Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati-

Mhe. Ali Juma Shamhuna

13. Wizara ya Kilimo na Maliasili

Mhe. Mansoor Yussuf Himid

14. Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko

Mhe. Nassor Ahmed Mazrui

15. Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Mhe. Said Ali Mbarouk

16. Wizara ya Kazi, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika

Mhe. Haroun Ali Suleiman

17. Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum

Mhe. Suleiman Othman Nyanga

18. Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum

Mhe. Haji Faki Shaali

19. Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum

Mhe. Machano Othman Said

Aidha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein ameteua Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:

1. Naibu Waziri, Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano

Mhe. Issa Haji Ussi

2. Naibu Waziri, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali

Mhe. Zahra Ali Hamad

3. Naibu Waziri, Wizara ya Afya

Mhe. Dr. Sira Ubwa Mamboya

4. Naibu Waziri, Wizra ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo,

Mhe. Bihindi Hamad Khamis

5. Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati

Mhe. Haji Mwadini Makame

6. Naibu Waziri, Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko,

Mhe. Thuwaiba Edington Kissasi

Waheshimiwa wote waliotajwa wanatarajiwa kuapishwa hapo kesho jioni katika viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar.
Naomba kuwasilisha.

Kwa hiyo Shamsi Vuai Nahodha Imekula Kwake MAsikini wee ndiyo maana alikua hataki serikali ya umoja wa kitaifa! Kumbeeee!
 
Du! Africa sijui tuna laana? Nchi kenye watu 900,000 mawaziri 25 ???????????????? And yet mambo mengine ya Zenj yanashughulikiwa na mawaziri wa muungano! This is ridiculous, just absurd period.
 
Kwa namna hii bora Shein angeliteua waziri kutoka kila familia moja!! Hahahaha. Halafu anataka kuinuna uchumi wa ZNZ. Kodi yote tutakayokusanya igharimie mawaziri, halafu tuende nje kuomba msaada ili kuwalipa wafanyakazi mishahara yao. Ukweli nimeanza kupoteza imani.
Haijawahi kutokea baraza kubwa kama hili katika historia ya miaka 46 tangu Mapinduzi. Tena tukiambiwa Waafrika tumelaaniwa tunahamaki. Spain yenye watu karibu milioni 45 ina mawaziri 15 - 8 wanaume, 7 wanawake. Hakuna Naibu Waziri, wa nini wakati waziri yupo.
 
Hii serikali ni kubwa sana. Ina wizara 16. Manaibu waziri 6 na mawaziri wasiokua na wizara maalum 3. Jumla 25.
 
Ingelikuwa ni uwezo wangu ningeteua mawaziri sita tu billa ya manaibu hapo Zanzibar ili kuokoa fedha..............
 
Du! Africa sijui tuna laana? Nchi kenye watu 900,000 mawaziri 25 ???????????????? And yet mambo mengine ya Zenj yanashughulikiwa na mawaziri wa muungano! This is ridiculous, just absurd period.
very much amazed, hivyo marekani population ni kiasi gani na masecretary of state ni wangapi?????? Mwenye data tafadhali.
 
kaunda serikali ndogo ya mawaziri 16...

una wazimu

Kuna watu wachache Zanzibar kuliko Mtwara (Milioni 1.1, sensa ya 2002).

Zanzibar kieneo inaingia Newala na Masasi mara kumi!

Nchi ya ki-Wilaya yenye mawaziri 19 si serikali ndogo, ni mtindio wa vichwa!
 
Kinachonichanganya ni kile kile hivi kuna haja gani ya kuwa na manaibu waziri wote hao? Am totally confused!
 
Kenya hivi sasa wamekata mzizi wa fitina na kuhakikisha ya kuwa kwenye katiba yao mpya wameweka ukomo wa idadi ya wizara za serikali ili kumzuia Raisi kutumia madaraka yake vibaya kwa kuwajaza maswahiba wake ili kukidhi mahitaji yake mwenyewe.......sisi huku CCM yasema katiba mpya siyo sera yao........................lakini kututawala wanataka hata kwa kuchakachua matokeo..................
 
Back
Top Bottom