MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,640
- 33,421
Mkuu wangu mimi pia Mkatoliki lakini nakiri hakuna justification juu ya hili! Tuache kupotosha kwa kutumia maneno Matakatifu ili kujiridhisha.pale Lowasa hakuitwa kuinjilisha! Hata Alhaji Mzee Mwinyi alikuwepo! EL amealikwa na Kanisa kutoa mchango (huku wakijua wananchi wako gizani juu ya tuhuma zake!).Huwezi kumuhukumu mtu kwani mwamuzi ni mwenyezi Mungu lakini kinachoshangaza na kutia wasiwasi ni kauli ya Askofu wa Mwanza na EL kuruhusiwa kutumia madhabahu kujisafisha! Kanisa letu limetughafilisha sana tunaofikiri nje ya box! Ingekuwa wanatangaza kama mkutano wa injili then yeyote anakwenda(akiwemo EL) ingekuwa sawa tu lakini huku wanatoa kauli hatujamwalika huku kahudhuria! kweli Kanisa limefikia hapo? EL ni Mtanzania mwenzetu,kiongozi wetu lakini Kanisa kwa hili HALIELEWEKI!Geza,
Lisilowezekana kwa mwanadamu, kwa Mungu linawezekana!.
Mwana wa Adamu Alikuja kwa ajili ya waliopotea na sio kwa ajili ya watakatifu!.
Tena akahimiza "wote wenye mizigo waje kwangu nitawapumzisha!"
Wakuu wa kanisa wanapaswa kutenda kama mkuu wao kuwakumbatia wasio wakamilifu ili kuwatakasa!.
Na mwisho nasisitiza, " JIWE WALILOLIKATAA WAASHI LITAFANYWA KUWA JIWE KUU LA PEMBENI!".