Thanks God for Giving us Kikwete

Professor & Rev Kishoka,
Do you know how the word "hypocricy" came alive; only because the surbodnate want to give favour and those above want to get, and protect each other. Professor you must be on my level, let us be frank: Our mothers are dying our sisters are dying; whom to rescue them? Corruption which want to be protected by this theory which is given by Rev. Pastor Kishoka << REv mind you I gruduated at Kasita those- days>> leave me die alone but not to submit to your rethoric!

A non hypocrite man should not be a farisayo!!
Reverand you did thank this person for this quote.

But i didn't understand it for he quoted me while refering at you and other stuff that i cant understand!

Nitashukuru!
 
Reverand you did thank this person for this quote.

But i didn't understand it for he quoted me while refering at you and other stuff that i cant understand!

Nitashukuru!

Nimetoa shukrani kwa kuchangia mada, pamoja na kuwa vidole vyake vinaonekana vinapingana na mawazo yake!
 
Nimetoa shukrani kwa kuchangia mada, pamoja na kuwa vidole vyake vinaonekana vinapingana na mawazo yake!
Mimi huwa natoa shukrani kwa kukubaliana na point.
Is asante ok regardless of the ambiguity?
Thanks anyways Rev.
 
Mimi huwa natoa shukrani kwa kukubaliana na point.
Is asante ok regardless of the ambiguity?
Thanks anyways Rev.

So goes your definition of Shukrani. If someone has different views wouldn't you acknowledge him/her and say thank you for your views?

Mimi hutoa shukrani hata pale ambapo sikubaliani.

Kwa kuwa nilianzisha mada hii, kwa mtu yeyote kuchukua fursa kusoma na kuchangia, nampa shukrani kwa kitendo hicho. Si lazima tuwe na msimamo mmoja wa mawazo au utata wa majibu.
 
So goes your definition of Shukrani. If someone has different views wouldn't you acknowledge him/her and say thank you for your views?

Mimi hutoa shukrani hata pale ambapo sikubaliani.

Kwa kuwa nilianzisha mada hii, kwa mtu yeyote kuchukua fursa kusoma na kuchangia, nampa shukrani kwa kitendo hicho. Si lazima tuwe na msimamo mmoja wa mawazo au utata wa majibu.
Tatizo sio msimamo ila ni kwamba sijaielewa kabisa ile posting kwasababu kama umeiona ameni quote!

Sasa utasemaje asante kwa kitu kisichoeleweka?

Si ndio maana nikaomba unieleweshe baada ya kuona umetoa asante?

Naomba unieleweshe maana ya posting yake since aliniquote na mimi sikuelewa jibu!
After all that then nitaweza na mimi kumpa shukrani!

Once again Shukran!
 
Mushi,

IO anakuita wewe Profesa na anaongelea kuhusu hypocricy na kuonyesha kuwa kuumina na kutaabikia kwa wananchi, hakuendani na theory zangu kuwa kuwepo kwa Kikwete ndio njia bora ya kuondokana na taabu na mihangaiko.
 
Rev, Kishoka,

Tatizo la Imani yangu pale anaposimama Mungu ni kwamba uchaguzi wa rais MATAKWA yetu, hivyo Mungu hujalia kile tulichokiomba.

kwa hiyo hii habari ya mtaka yote kukosa yote ni matokeo ya mwanadamu ktk tamaa zake hazihusiani na mapendekezo ya Mungu.

hapo ndipo kidogo nilikwama kwa sababu hapa tunaingiza maswala ya imani ya dini na pengine tofauti zilizopo kati ya imani yangu na yako ndiyo yananipa shida kuelewa hata hivyo, nakubaliana na mchango wako kwa kiasi kikubwa kwamba makosa tuliyoyafanya ya kumchagua JK imekuwa rehma kwetu kupata nafasi ya kuyatupia macho maswala ya UFISADI kwani hakuna akti yetu anayeweza kupiga ramri la Uongozi wa Freeman chini ya Chadema...

Yet, pamoja na yote haya ni lazima tukubali tulifanya makosa sisi wenyewe pengine leo hii chini ya Chadema ama CUF tunmgekuwa ktk hatua nyingine kabisa..Mkapa angekuwa akichekea kizimbani, nyumba za serikali zimerudishwa, swala la EPA, Richmond, Buzwagi wala Balali yasingekuwa kweli.
 
Ukweli ni kwamba hatujui ingekuwaje kama tungemchagua Freeman. Huenda sasa tungekuwa pazuri, au huenda nchi ingekuwa imevurugika kiasi cha kutawaliwa na maafande.

Tunachojua ni hiki: JK ameanzisha kampeni ya kutokomeza angalau baadhi ya mafisadi. Kwa sasa amemgeukia Karimagi. Mkataba wa kiwizi wa nyongeza ya muda aliowekeana na mafisadi serikalini unavunjwa.

Asidhani mtu hapa kwamba hawa Wabunge wanathubutu kuwavaa Mkapa na wakuu wengine bila ruhusa ya JK.

Pamoja na kumshukuru JK kwa kazi hii, tunamwomba awafukuze CCM hawa mafisadi.

Mikataba ya Madini huenda itamshinda JK kwani wezi wa nje walihakikisha kunakuweko kipengele cha kusema kwamba kisheria, ni London pekee ndiko wanaweza kuzungumzia mikataba yao. Kilichobak ni JK kuwaambia hawa wezi kwamba wasipokubali mabadiliko yatakayoleta HAKI, basi serikali haitawapa ushirikiano. Wanahitaji huo ushirikiano wa serikali ili kulinda mirija yao.
 
Ukweli ni kwamba hatujui ingekuwaje kama tungemchagua Freeman. Huneda sasa tungekuwa pazuri, au huenda nchi ingekuwa imevurugika kiasi cha kutawaliwa na maafande.

Tunachojua ni hiki: JK ameanzisha kampeni ya kutokomeza angalau baadhi ya mafisadi. Kwa sasa amemgeukia Karimagi. Mkataba wa kiwizi wa nyongeza ya muda aliowekeana na mafisadi serikalini unavunjwa.

Asidhani mtu hapa kwamba hawa Wabunge wanathubutu kuwavaa Mkapa na wakuu wengine bila ruhusa ya JK.

Pamoja na kumshukuru JK kwa kazi hii, tunamwomba awafukuze CCM hawa mafisadi.

Mikataba ya Madini huenda itamshinda JK kwani wezi wa nje walihakikisha kunakuweko kipengele cha kusema kwamba kisheria, ni London pekee ndiko wanaweza kuzungumzia mikataba yao. Kilichobak ni JK kuwaambia hawa wezi kwamba wasipokubali mabadiliko yatakayoleta HAKI, basi serikali haitawapa ushirikiano. Wanahitaji huo ushirikiano wa serikali ili kulinda mirija yao.
Tafadhali be specific kwenye highlighted!
 
Huoni amewatoa mkuku Lowasa, Msabaha, Karimagi, Chenge na Balali? Au ulitaka awaue?

Tunasubiri washtakiwe baadaye, na wafukuzwe CCM
 
Naomba nilinukuu Mwanahalisi na hasa kwenye huo msisitizo. Ukifuatilia pia na mada ya Mwanakijiji ya Illusion of Power, utabaini kuwa Shukrani hii haikuwa na makosa.

KUNA uvumi uliotamalaki kwamba ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), lipo kundi la watu linalojiandaa kumpinga rais wao mwaka 2010.

Kwamba sasa hawautaki ule utaratibu wa CCM ambao haujaandikwa kokote wa kumuacha rais atetee vipindi viwili vya miaka mitano kila kimoja. Sasa wanataka kumpinga katika kipindi cha pili.

Huu ni uvumi ambao umekuwako kwa muda sasa. Hakuna ushahidi wa kuthibitisha haya isipokuwa kwa kuwa ni mambo yanayosemwa si vema kuyapuuzia, yafaa tu kuupa umuhimu uvumi huu.

Katika hali ya kawaida mtu angejiuliza maswali magumu kidogo; kwamba wakati hata Rais Jakaya Kikwete hajamaliza nusu ya muda wake wa miaka mitano ya kwanza amewakosea nini wenzake hadi waanze kufikiria kumpiga?

Swali hili ni gumu kwa sababu kwa rais aliyeshinda kwa wingi wa kura kama za Kikwete, na kwa sifa alizokuwa akimwagiwa wakati wa kampeni, inakuwa ni vigumu kujua kilichotokea hadi wenzake sasa wafikiri kumpinga 2010?

Kubwa zaidi, watu wanajiuliza nini kinapeka mawazo ya watu mwaka 2010 wakati hapa katikati kuna mambo mengi tu ya kimsingi ya kujadili kuhusu maendeleo na mustakabali wa taifa hili? Sina majibu ya maswali haya yote.

Hata hivyo, tafakari ya kina inasogeza mawazo yangu kwamba uvumi huu wa watu wanaoutaka urais ndani ya CCM mwaka 2010 unachochewa na watu ambao hawafurahishwi na mwendeno wa mambo ndani ya serikali ya awamu ya nne.

Watu hawa wasiofurahishwa na mwenendo wa mambo, wanadaiwa kuwa na hasira dhidi ya Kikwete kwa sababu kuu moja.

Kwamba, amekuwa ni rais mlaini mno anayeruhusu watu kuichononoa serikali yake, kuchokonoa mawaziri wake, kuchokonoa maamuzi ya serikali kiasi cha kufanya watu waliozoea kufanya mambo watakavyo kuwa na wakati mgumu.

Watu hawa wanaompinga Kikwete wanaufananisha utawala wake na ule wa mtangulizi wake, Benjamin Mkapa. Wakati wa utawala wake, Mkapa hakuruhusu hata serikali yake kunyooshewa kidole achilia mbali kuwatikisa mawaziri wake.

Watu hawa wenye hasira na Kikwete wanasukumwa na sera mpya za uwazi za Kikwete tofauti na uwazi wa Mkapa ambao kwa hakika ulikuwa uimla na usiri usioelezeka.

Wanaotaka kumpinga Kikwete mwaka 2010 wanasumbuliwa na kitu kimoja tu, kwamba kwa nini serikali ikubali kuchukua hatua kwa kila tuhuma inayotolewa dhidi yake, wakati ingeweza tu kupuuza na kuacha mambo kama yalivyokuwa.

Ni hasira za mwizi anayehoji sababu ya mwenye mali kushtuka kwamba anaibiwa wakati mwizi anaamini ana haki ya kujichukulia tu mali ya watu atakavyo.

Kwa maana hiyo, basi kitendo cha Rais Kikwete kuruhusu Bunge kuunda tume kujadili suala la Richmond ambalo liliishia kuvunjwa kwa Baraza la Mamwaziri; kukubali ukaguzi ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na hatua yake ya kuruhusu uchunguzi wa mikataba ya madini katika migodi mikubwa.

Hatua ya Kikwete kukataa kuwatetea mawaziri wake wenye kashfa na hivyo kulazimika kujiuzulu kama Edward Lowassa, Dk. Ibrahim Msabaha, Nazir Karamagi na hivi karibuni kabisa Andrew Chenge; kwa ujumla ni mambo ambayo hayawafurahishi watu waliozoea kuvuruga mambo na kutetea na Rais wao.


Ndiyo! Tunakumbuka Rais Mkapa akitetea polisi walipoua wananchi kule Pemba, 27 Januari 2001; tunakumbuka Mkapa akitetea mikataba ya ovyo kabisa ambayo viongozi wetu waliitumia kuitumbukiza nchi katika vifungo vya kiuchumi.Kubwa zaidi, wananchi wanakumbuka jinsi Mkapa alivyokuwa na ujasiri wa kutetea maovu na maamuzi ya ovyo kabisa ya utawala wake, bali pia alithubutu kuwatukana wananchi.

Alisema kwamba ni wavivu wa kufikiri na wengine wana wivu wa kijinga pale wanapohoji ukwasi wa kupindukia na wa ghafla wa watawala wetu!

Kwa maana hiyo viongozi waliolelewa na sera na mikakati ya kibabe ya Mkapa, kauli za kuwabeza na kuwakejeli wananchi, matamshi ya kuwadhalilisha wampinzani kuwa ni wachumi na wanasiasa ucharwa; sasa wanajihisi kubanwa katika awamu hii.


Hawaoni raha tena waliyokuwa wanapata chini ya Mkapa. Viongozi hawa ndio wanaojipanga na kueneza uvumi kwamba mwaka 2010 ni lazima Kikwete apingwe.

Wanampinga Kikwete si kwa sababu wana mkakati wa ziada wa kuharakisha maendeleo ya wananchi, ila wanataka kumweka kibaraka wao ambaye atahalalisha uharamia kama ulivyowahi kuhalalishwa huko nyuma.

Hawa ni watu waliochoka, walafi na wanasukumwa na tamaa ya kurejesha Watanzania utumwani. Ingawa watu wanaokusudia kumpinga rais Kikwete mwaka 2010 wanajenga hoja kwamba serikali ya awamu ya nne imepwaya kwa sababu rais wake amekosa umakini (soften) na kwa maana hiyo kumuachia aongoze nchi mapaka 2015 ni sawa na kulitumbukiza taifa kwenye maafa, ukweli wa mambo unabakia kuwa mmoja, hawana jipya wanalokusudia kuleta isipokuwa kuendekeleza ubinafsi wao.

Ebu tufikiri kwa kina zaidi! Ni vigumu kutathmini matatizo ya Tanzania nje ya mfumo mzima wa utawala ulioasisiwa na CCM. CCM ina kila sababu ya kubebeshwa mzingo kuhusu matatizo ya nchi hii. Kama ni rushwa nchini imeletwa na CCM! Kama ni uporaji wa mali ya umma nchi hii umeletwa na CCM kama ni viongozi wazembe nchi hii CCM ni namba moja kwa viongozi wazembe, kuanzia walioko kwenye chama hadi walioko serikalini.

CCM ni muasisi wa matatizo ya taifa hili. Ndiyo maana sisi tunapowatazama watu wanaojitutumua kuutaka urais mwaka 2010 tunawaona kama watu wanaosukumwa na kitu kimoja tu, ubinafsi na tamaa ya kutaka kuendeleza ya kale. Ni watu wasiotaka mabadiliko, ni watu wasiofurahishwa na mwenendo mpya wa uwajibikaji wa kila mmoja kwa makosa yake.

Ndiyo maana wanataka kumwengua Kikwete ili warejeshe &#8216;zimwi likujualo halikuli likakwisha'. Laiti wangelikuwa ni watu wapenda mabadiliko ya kweli, umma ungesimama nyuma yao, lakini kwa historia yao ni watu wanaolililia kurejea ukale wao.

Kwa Wakristo wanafahamu kwamba Musa alipowaongoza wana wa Israel kutoka utumwani Misri kwenda nchi ya ahadi, Kaanani, wapo waliofika njiani na kutamani kurejea utumwani kwa sababu walikumbuka nyama za bure. Wanopanga kumpinga Kikwete 2010 wamekumbuka vya kunyonga, wamekumbuka nguvu zao za kujichukulia kila walichotaka bila kuhojiwa kokote, wamekumbuka utukufu waliojitwalia miaka ya nyuma wanatamani hali hiyo. Hakika nia yao si kuwatumikia wananchi.
 
...kiasi cha kufanya watu waliozoea kufanya mambo watakavyo kuwa na wakati mgumu...

Heeh..So President anawapa watu wakati mgumu....! Na hawa ni wale ambao hawana nia njema ya kuijenga nchi..!!

AND..?

In that case then..He is doing very well!!
 
Jamani mumemuelwewa vibaya,sio kama anamsifie Kikwete,someni upya mutafahamu nini anamaanisha.
Ni tungo tata mno inayohitaji uyakinifu kuipembua,hicho ni kiswhili cha mafumbo.
Mungu wabariki wazaramo.

Ni kweli kabisa,tafadhali muwe na upeo wa kuchanganua mambo,hapo hajasifiwa"positively" bali ni "negatively".Sidhani kama kusifiwa uzembe,kulea ufisadi ni sifa nzuri.
 
Labda niseme kwamba tumshukuru Mungu na tuzidi kumuomba aendelee kumfanya Kikwete azidi kusikia vilio vya watanzania!! Kwani kuna mengi tu bado anayafumbia macho, mfano: kulikuwa na kilio cha wengi kuhusu Chenge na alikuwa pia kwenye list of shames pamoja na Tangold yake lakini Rais alimrudisha kwenye Cabinet!!
Hivyo tumuombe sana Mungu ili macho na masikio ya Kikwete yazidi kuwa wazi aweze kuona na kusikia na mafisadi wake.

LIMBANI, tatizo la JK si kusikia vilio vya watanzania. Naamini JK ni msikilizaji mzuri na anataarifa kamili za vilio vyetu. Tatizo lake kubwa ni kutochukua hatua kwa wakati muafaka! Hii ni kasoro kubwa kwa uongozi kwa kuwa kuchelewesha mno uamuzi kunaweza kuligharimu pakubwa Taifa. Mifano ni mingi: Kumchelewesha DG wa PCCB mfumbia macho Ufisadi, kumpuuza DG wa TIC na kauli zake za kikabila na uongozi wa enzi za mawe, Kuwavumilia Mawaziri wabovu n.k. Yote haya yanagharama. Na si utetezi unaokubalika kila wakati kwa JK kusema eti kwamba anaogopa kumuonea mtu. Yeye Malaika?
 
Shangilieni sana uongozi wa Kikwete, maana 2010 kunaweza kutokea ambayo hayajawahi kutokea.

Get the popcorn, pepsi and smell the coffee!
 
Rev.Kishoka,

..my reading ni kwamba huyo ni Kikwete akitafuta huruma za wapiga kura.

..wakati wa Mkapa kila kashfa[biashara,mashamba,majumba ya kifahari..] alikuwa akisukumiziwa sumaye. kila mtu mwenye ufahamu anajua hizo zilikuwa ni harakati za kikwete na wanamtandao.

..ninachojiuliza mimi ni lini Kikwete ataacha kampeni na kuanza kazi? tumefika mahali nchi inaendeshwa kwa kampeni.

..badala ya mawaziri kutekeleza bajeti, wanasafiri mikoani "kuwaelimisha" wanachi kuhusu kampeni!!
 
Itakuwa kazi kubwa sana kumwangusha Kikwete iwe ndani ya CCM ama nje labda tu Kikwete mwenyewe awe ktk kundi la hao wanaojipanga kumvua Urais. Nikiwa na maana ni mmoja kati ya hao MAFISADI ambao kwa hila zao wanajaribu kuendeleza Utawala wa mkoloni mweusi..

Trust me, Kikwete hawezi kushindwa na mtu yeyote kwa kura ikiwa hawa jamaa watajitenga kwa sababu haya machache aliyoyafanya tayari ni kinga yake kubwa sana ktk uchaguzi ujao hasa akiwa against hao Mafisadi...Jamani hawa jamaa wamechoka ile mbaya kisiasa, hata wengine hali zao sasa hivi inabidi tuwaombee Mungu!.. fedha wanayo lakini macho ya watu ni laana tosha!

Ni kundi moja tu ambalo linaweza kumwangusha Kikwete nalo ni UMOJA wa WAPINZANI kama wataungamna na kuacha kabisa mpango wa wagombea binafsi badala yake wasimamishe wabunge waliofanya vizuri mwaka 2005 hasa wale walioshika nafasi ya pili ktk majimbo. Yote hii inategemea nguvu ya UMOJA wa Wapinzani lakini kama watabakia kuwa hivi walivyo leo basi CCM wanaweza kuchukua tena kwa sababu madai yao yatakuwa wameisha safisha jungu Mafisadi wote wako nje na hawagombei nafasi yoyote!..Kama sahani huwezi kutokula chakula kwa sababu sahani hiyo aliitumia Fisadi.. imesafishwa na hivi sasa safi kabisa!..

Jokakuu,
Tanzania hakuna viongozi kwani kampeni ndio ushindi wa kila kitu kwa kila hawa watawala wetu. Bila kushinda kura huwezi kuwa waziri hivyo shina la Uwaziri ni kampeni ya ushindi na ndio maana kila kiongozi anayo kamati yake ya Ufundi. hakuna kiongozi hata mmoja anayefikiria nini atawafanyia Watanzania kwani kulingana na mfumo huuu tuliochukua viongozi wetu wanafikiria kuwa sasa hivi nchi inajiongoza yenyewe wao wanatawala tu kuhakikisha ufalme wa CCM unawafikia wananchi, yaani kujichana tu na hiyo Free Market Economy ambayo kwetu sisi ina maana moja tu - KILA MTU NA MZIGO WAKE!.
 
Mzee Walioba Alisha Sema Viongozi Wetu Ni Dhaifu,hizo Ni Sifa Za Udhaifu Wa Muungwana Na Mganga Wake Wa Kienyeji Kingunge,hivi Huyu Mzee Wa Nini ?
 
Back
Top Bottom