Thank God Slaa is not the president, and that will never be

Waberoya

Platinum Member
Aug 3, 2008
15,169
10,785
Kuna quality za rais wa nchi na kuna quality za usanii!

Kuna busara ya kuwa kiongozi wa nchi na kuna busara ya kuwa kiongozi wa vikao vya harusi!

Bahati mbaya kuna namna ya kulazimisha mtu fulani a-fit sehemu fulani, bahati nzuri kuwa kila anapoweza kufit mtu ndipo anapowekwa kidemokrasia kutokana na akili za waliomweka hapo!

Kwa bahati mbaya mimi sina cha kufuata mkondo, sijawa mbwa mimi wala sina anayenipigia mluzi, ni huru kutoa mawazo pasi kujua au kujali mwingine ataumia vipii

Swala la Arusha, swala la lile sakata la umeya na madiwani, si swala la kuchekewa, damu imemwagika kule!

Ni ufisadi sana kufikiri kuwa yale tunayoyawaza sisi tu ndiyo yako sahihi.

Si busara Slaa kuingilia maamuzi ya madiwani ambao kimamlaka ni wawakilishi wa chama kule kwenye maeneo yao. sidhani kama rais anaweza kuingilia maamuzi ya mkuu wa wilaya kama yale maamuzi yalilenga katika kuleta amani na kusaidia wananchi wa eneo husika

Hii si aibu ya chadema tu, ni aibu ya uongozi wa juu, kutowatumaini wala kuwaamini hawa madiwani, ambao kwayo wanaleta na kusambaza sera za chadema; kibaya risk kubwa iko kuwa madiwani wengi zaidi watatumika kuiweka CCM madarakani kwani ni DHALILISHO LA MADIWANI WOTE....they are kids they can not think what a joke!!si busara hata kidogo na ni ufisadi wa kurubuni watu kuwa chadema ilikuwa haijui kinachoendela huko Arusha,

kila kitu kilikuwa wazi vyombo vilitangaza, na LEO ghafla akina slaa wanashtuka kama vile wamefumaniwa na wake za watu kuwa madiwani hawakuwa sahihi!

Miafaka ipo, haikwepeki inaishi, inakua inatafutwa, ili amani iwepo! HIVI ingekuwaje kama chadema wangekuwa chama tawala kwenye issue hii ya Arusha??Slaa umeishaharibu vitu vingi, ila wale vipofu wako wanaojaribu kwa upofu wao hata kukuona uko sawa na Nyerere! (God Forbid!) ili swal la Arusha limekaa kimaslahi zaidi na siyo ki-nchi zaidi! Nilijua ukimya huu umejengeka kibusara kumbe una kula tuition ya kuwa puppet!watu wako mahali fulani ambao wakilala na kuamka wanaota chadema ishike dola, wako watu mahali fulani wanaona credibility ya wabunge wa chadema, wako wanaoona kwa pandembili......Hivi SLAA ANGEKUWA RAIS ingekuwaje?

Slaa angezuia magazeti yasimchore katuni , SLAA ASINGEKUBALI KUTOKA MADARAKANI KWA NGUVU YA DEMOKRASIA.....Thanks God you are not president!

Swala la Arusha kwa namna nyingine limewaharibia tena.....Lema tunamjua, is just another gang in the house, nguvu za maneno na mob saikoloji havitamfikisha popote......certainly we need change but not changes that alerts us differently!!

MBIO ZA CHADEMA HII zinapeleka kuwa si chama cha demokrasia bali cha kibabe, jeuri, chama ambacho kingekuwa na dola wangekuwa madikteta.

Mbowe hana tatizo, yeye ili mradi biashara zake ziende salama in the name of politics!! bila kujua anamwingiza Slaa chooni, slaa bila kujali hatima yake na mtoto wake mchanga analipuka tu!!! TUTAFANYA UCHAGUZI UPYA WA MADIWANI....TUTAUNDA TUME YA MARANDO ......CCM style....shame on you!!!!!
 
Mkuu umeandika kwa hasira mpaka usomeki!! huwezi pangilia vizuri angalau ukawa na paragraph mbili tatu hivi?
 
sidhani kama rais anaweza kuingilia maamuzi ya mkuu wa wilaya kama yale maamuzi yalilenga katika kuleta amani na kusaidia wananchi wa eneo husika.............................................

Sijakuelewa hapo mkuu ebu fafanua
Una maaana Rais wa nchi gani au rais yupi specifically hawezi kutengua maamuzi ya mkuu wa wilaya ?

Vipi ile wilaya wanayopigaa sana kama mkuu wa wilaya alisema kama kikiruhusiwa kilimo cha bangi hali itakuwa shwari. Je rais akigoma itakuwaje ?
 
Engineer mwenye pumba.

Kama wewe ni injinia wa ukweli,siasa huziwezi. Uko uchi mkuu trust me, hamna kitu hapo. Kama ukiwa honest tutakuonyesha kuwa huna hoja.

Soma soma kidogo ujifunze kama unataka siasa.
 
Kuna quality za rais wa nchi na kuna quality za usanii!

Kuna busara ya kuwa kiongozi wa nchi na kuna busara ya kuwa kiongozi wa vikao vya harusi!

Bahati mbaya kuna namna ya kulazimisha mtu fulani a-fit sehemu fulani, bahati nzuri kuwa kila anapoweza kufit mtu ndipo anapowekwa kidemokrasia kutokana na akili za waliomweka hapo!

Kwa bahati mbaya mimi sina cha kufuata mkondo, sijawa mbwa mimi wala sina anayenipigia mluzi, ni huru kutoa mawazo pasi kujua au kujali mwingine ataumia vipii

Swala la Arusha, swala la lile sakata la umeya na madiwani, si swala la kuchekewa, damu imemwagika kule!

Ni ufisadi sana kufikiri kuwa yale tunayoyawaza sisi tu ndiyo yako sahihi.

Si busara Slaa kuingilia maamuzi ya madiwani ambao kimamlaka ni wawakilishi wa chama kule kwenye maeneo yao. sidhani kama rais anaweza kuingilia maamuzi ya mkuu wa wilaya kama yale maamuzi yalilenga katika kuleta amani na kusaidia wananchi wa eneo husika

Hii si aibu ya chadema tu, ni aibu ya uongozi wa juu, kutowatumaini wala kuwaamini hawa madiwani, ambao kwayo wanaleta na kusambaza sera za chadema; kibaya risk kubwa iko kuwa madiwani wengi zaidi watatumika kuiweka CCM madarakani kwani ni DHALILISHO LA MADIWANI WOTE....they are kids they can not think what a joke!!si busara hata kidogo na ni ufisadi wa kurubuni watu kuwa chadema ilikuwa haijui kinachoendela huko Arusha,

kila kitu kilikuwa wazi vyombo vilitangaza, na LEO ghafla akina slaa wanashtuka kama vile wamefumaniwa na wake za watu kuwa madiwani hawakuwa sahihi!

Miafaka ipo, haikwepeki inaishi, inakua inatafutwa, ili amani iwepo! HIVI ingekuwaje kama chadema wangekuwa chama tawala kwenye issue hii ya Arusha??Slaa umeishaharibu vitu vingi, ila wale vipofu wako wanaojaribu kwa upofu wao hata kukuona uko sawa na Nyerere! (God Forbid!) ili swal la Arusha limekaa kimaslahi zaidi na siyo ki-nchi zaidi! Nilijua ukimya huu umejengeka kibusara kumbe una kula tuition ya kuwa puppet!watu wako mahali fulani ambao wakilala na kuamka wanaota chadema ishike dola, wako watu mahali fulani wanaona credibility ya wabunge wa chadema, wako wanaoona kwa pandembili......Hivi SLAA ANGEKUWA RAIS ingekuwaje?

Slaa angezuia magazeti yasimchore katuni , SLAA ASINGEKUBALI KUTOKA MADARAKANI KWA NGUVU YA DEMOKRASIA.....Thanks God you are not president!

Swala la Arusha kwa namna nyingine limewaharibia tena.....Lema tunamjua, is just another gang in the house, nguvu za maneno na mob saikoloji havitamfikisha popote......certainly we need change but not changes that alerts us differently!!

MBIO ZA CHADEMA HII zinapeleka kuwa si chama cha demokrasia bali cha kibabe, jeuri, chama ambacho kingekuwa na dola wangekuwa madikteta.

Mbowe hana tatizo, yeye ili mradi biashara zake ziende salama in the name of politics!! bila kujua anamwingiza Slaa chooni, slaa bila kujali hatima yake na mtoto wake mchanga analipuka tu!!! TUTAFANYA UCHAGUZI UPYA WA MADIWANI....TUTAUNDA TUME YA MARANDO ......CCM style....shame on you!!!!!

What an argument!? deeply intellectual, emotionaly entertaining, and politically amusing.
 
Slaa anavyoelezea jinsi taratibu zilivyokiukwa huko Arusha ni kama amewahukumu tayari watu walioshiriki katika huo ‘muafaka'. Sasa anaunda tume ya nini tena kama hukumu iko tayari?

Pili: Hii tume kwanza inatumia pesa za nani? Pili je tume ikigundua hukumu aliyoisema Slaa ni tofauti atakuwa tayari kuwaomba msamaha aliowahukumu au kwa kuwa yeye ni katibu mkuu basi wengine wote si kitu.

Tatu: Je hawa madiwani wanawakilisha chama au wanawakilisha wananchi waliowachagua. Je uchaguzi ukirudiwa na wakashinda wale wale, huoni huu utakuwa ni upumbafu wa chama na upotevu wa pesa za wananchi

Eti "Tuko tayari kurudia uchaguzi" kwa gharama za nani? Na je ni busara kwa nchi nzima itishwe mzigo kwa suala ambalo uongozi wa CDM ulijua kabisa nini kinaendelea. Kwani mikutano ya muafaka ilikuwa inafanyika usiku kwa uficho
 
Sijakuelewa hapo mkuu ebu fafanua
Una maaana Rais wa nchi gani au rais yupi specifically hawezi kutengua maamuzi ya mkuu wa wilaya ?

Vipi ile wilaya wanayopigaa sana kama mkuu wa wilaya alisema kama kikiruhusiwa kilimo cha bangi hali itakuwa shwari. Je rais akigoma itakuwaje ?
Ame compare ndizi na chungwa.Ametolea mfano kuhusu madiwani ambao wananchaguliwa na wananchi na kufananisha na wakuu wa wilaya ambao wanateuliwa na rais.Hamna kitu hapo,labda awe ametumwa.Ukitumwa unakuwa na mawazo ya kitumwa tu.Kama angekuwa amejituma,basi pengine angekuwa anaelewa anachoposti humu.Nuttin....Cheki upupu wake hapo chini...
Si busara Slaa kuingilia maamuzi ya madiwani ambao kimamlaka ni wawakilishi wa chama kule kwenye maeneo yao. sidhani kama rais anaweza kuingilia maamuzi ya mkuu wa wilaya kama yale maamuzi yalilenga katika kuleta amani na kusaidia wananchi wa eneo husika
 
Slaa anavyoelezea jinsi taratibu zilivyokiukwa huko Arusha ni kama amewahukumu tayari watu walioshiriki katika huo ‘muafaka'. Sasa anaunda tume ya nini tena kama hukumu iko tayari?

Pili: Hii tume kwanza inatumia pesa za nani? Pili je tume ikigundua hukumu aliyoisema Slaa ni tofauti atakuwa tayari kuwaomba msamaha aliowahukumu au kwa kuwa yeye ni katibu mkuu basi wengine wote si kitu.

Tatu: Je hawa madiwani wanawakilisha chama au wanawakilisha wananchi waliowachagua. Je uchaguzi ukirudiwa na wakashinda wale wale, huoni huu utakuwa ni upumbafu wa chama na upotevu wa pesa za wananchi

Eti "Tuko tayari kurudia uchaguzi" kwa gharama za nani? Na je ni busara kwa nchi nzima itishwe mzigo kwa suala ambalo uongozi wa CDM ulijua kabisa nini kinaendelea. Kwani mikutano ya muafaka ilikuwa inafanyika usiku kwa uficho

Thanks great thinker

You can say it again!
 
Engineer mwenye pumba.Kama wewe ni injinia wa ukweli,siasa huziwezi.Uko uchi mkuu trust me.Hamna kitu hapo.Kama ukiwa honest tutakuonyesha kuwa huna hoja.Soma soma kidogo ujifunze kama unataka siasa.

Injinia gani huyu??
Siasa ataiwezea wapi? Mambo ya mtoto mchanga wa slaa na umeya wa ar wap na wp? Huyu km sikosei atakuwa injinia wa MIPASHO...
 
Slaa anavyoelezea jinsi taratibu zilivyokiukwa huko Arusha ni kama amewahukumu tayari watu walioshiriki katika huo ‘muafaka'. Sasa anaunda tume ya nini tena kama hukumu iko tayari?

Pili: Hii tume kwanza inatumia pesa za nani? Pili je tume ikigundua hukumu aliyoisema Slaa ni tofauti atakuwa tayari kuwaomba msamaha aliowahukumu au kwa kuwa yeye ni katibu mkuu basi wengine wote si kitu.

Tatu: Je hawa madiwani wanawakilisha chama au wanawakilisha wananchi waliowachagua. Je uchaguzi ukirudiwa na wakashinda wale wale, huoni huu utakuwa ni upumbafu wa chama na upotevu wa pesa za wananchi

Eti "Tuko tayari kurudia uchaguzi" kwa gharama za nani? Na je ni busara kwa nchi nzima itishwe mzigo kwa suala ambalo uongozi wa CDM ulijua kabisa nini kinaendelea. Kwani mikutano ya muafaka ilikuwa inafanyika usiku kwa uficho
Pumba yako namba tatu:madiwani waanawawakilisha wananchi kwa kupitia chama.Mnavamia siasa nyie kwasababu mnataka ufisadi.Ni heri muingie kwenye siasa kwasababu mna uchungu na nchi na si kwasababu mnataka maslahi.Hovyoo!
 
umekurupuka mkuu fuatilia mkasa vzr halafu maelezo yako mengi lakini pointi haipo.
 
Ame compare ndizi na chungwa.Ametolea mfano kuhusu madiwani ambao wananchaguliwa na wananchi na kufananisha na wakuu wa wilaya ambao wanateuliwa na rais.Hamna kitu hapo,labda awe ametumwa.Ukitumwa unakuwa na mawazo ya kitumwa tu.Kama angekuwa amejituma,basi pengine angekuwa anaelewa anachoposti humu.Nuttin....Cheki upupu wake hapo chini...

Hapa vipi mkuu umetumwa au umejituma? unakuwa kama JF -kata mushi?

chadema ikiguswa tu hulali! Vipi ng'ombe wa Mbowe umewaingiza zizini?
 
Button ya thanx imeenda wapi? This guy anastahili 1000 thanx! Umefanya analysis ya maana sana! Nakupongeza kwa kuwafumbua watu macho
 
Bukuku umetoka mkuku .Umeadhirika hapa ni JF watu hawakurupuki kama huko CCM hapa tumetulia kama hujui la kusema ni sawa .Wewe huwezi kuwaamlia Chadema na CCM ni watu wa rushwa .Kama mmemwaga hiyo rushwa poa . Watui walikufa pale wananchi wanajua ujinga wa CCM lakini umeingia chooni na kuanza kulia huko tena choo cha shimo.Kweli wewe injinia maana akilli yako duh !!!
 
Mimi pia ni Injinia lakini loo, once is an incidence and twice coincidence, hivo naogopa litakalofuatia. Alianza Eng. Stella Manyanya bungeni na hata wiki haijapita kachombeza Eng. Burton Bukuku hapa JF !

Kama Injinia, ingetosha kabisa kusema Thank God Dr. Slaa is not the President na wengine tungeweza kukuelewa lakini ukiongezea and he will never be, hapo umevua hata hicho kipande cha kaniki kilichokusetiri, umebaki mtupu yaani uchi kabisaaa!

Kwa hali hiyo mimi najiondoa kwenye huu mjadala, sitakubali kushuka that low.
 
Hapa vipi mkuu umetumwa au umejituma? unakuwa kama JF -kata mushi?

chadema ikiguswa tu hulali! Vipi ng'ombe wa Mbowe umewaingiza zizini?
Umenichekesha kweli.Ebu jibu hoja kwanza.Ni kivipi umefafananisha issue ya udiwani na ukuu wa wilaya?Cant you compare apples to apples?Halafu huwa siitetei chadema,umekurupuka mkuu.Kuhusu ng'ombe wa Mbowe hiyo naipotezea Injinia.Kama ulivyo raise issue ya mtoto mchanga na uwezo wake Dr Slaa wa kuwa rais.Pumba to the fullest.
 
umekurupuka mkuu fuatilia mkasa vzr halafu maelezo yako mengi lakini pointi haipo.cdm ni chama makini hakirubuniwi na watu wa aina yako.viva slaa endelea kujenga chama
 
Pumba yako namba tatu:madiwani waanawawakilisha wananchi kwa kupitia chama.Mnavamia siasa nyie kwasababu mnataka ufisadi.Ni heri muingie kwenye siasa kwasababu mna uchungu na nchi na si kwasababu mnataka maslahi.Hovyoo!

Mkuu inaonekana unapenda sana uchafu weye! ulishasema post yako ya kwanza na kuutangazia umma wa JF kuwa nilichoandika ni pumba, naona sasa inapitia pumba moja moja!! LOL!

Unapenda uchafu sana mkuu, umezoea sana kukaa kwenye pumba, angalia mwenzio Mag3 alivyo msafi! amesema hawezi kukaa kwenye hii thread, ameandika ameondoka , japo amegusa kidogo!

Kwanini unazipenda pumba mkuu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom