Hapa umenichanganya kidogo, Mrema ana nyumba Kiboriloni? Na Mengi pia ana nyumba Kiboriloni? Then ya Mrema ni nzuri kuliko ya Mengi? Halafu suala l a dhahabu si ziliwahusu watu wa karibu na mkuu wake enzi hizo? Mkuu nisaidie nisichanganyikiwe zaidi.
yomba Yomba,
Anaitwa Agness, alikuwa mbunge wa TLP wa viti maaalum mrefu hivi na ni mkenge sana, kuna wakati kidogo niupande mkenge kule Dodoma, lakini mshikaji mmoja akanishitua!
Kuna mtu yoyote ana rekodi yake alivyokwua DSO?
nyumba ya mrema ya moshi alijengewa na umoja wa vijana ccm...ni hekalu kweli kweli.....na kiongozi wa pili baada ya myerere kujengewa nyumba na YOUTH LEAGUE!!!
My point mkuu ni kwamba Mrema was never clean, na mara nyingi hata yeye mwenyewe alipohojiwa alikiri hili kwamba "mimi sikuwa malaiaka" kuhusu nyumba samahani kwa kukuchanganya, I meant huko Uchaggani, Mrema ana hekalu zito sana amabalo huwezi kutoka kuwa ofisa usalama kwenda ubunge na uwaziri ukaweza kulijenga kwa mshahara wa halali Mungu Ambariki Anyways, Kiongozi Mrema!
FMES,
On top of hilo hekalu la uchagani, kuna nyumba ilinunuliwa na TLP Dar ili mwenyekiti aweze kuishi humo baada ya Mrema kufanyiwa mizengwe na NHC kwenye nyumba aliyokuwa anaishi. .
Bwana Philemon Michael,
Inawezekana Mrema amewahi kuwa RSO Shinyanga, lakini si kipindi yalipotokea mauaji yaliyomwajibisha mzee Mwinyi. Aliyekuwa RSO pamoja na RPC walikaa miaka kadhaa rumande na baadaye kuhukumiwa kifungo cha miaka saba. Kwa nyumba iliyonuniliwa na TLP, watafute waliokuwa naye karibu. Jinsi alivyojimilikisha sioni tofauti na Mkapa alivyofanya kwenye nyumba ya seaview. Kwa kifupi, tumefikishwa pahali pa kuamini kuwa mbuzi hula kulingana na urefu wa kamba yake and who knows ? Huyu angeukwaa uraisi 1995 haya ya Ben yangekuwa cha mtoto.
Walau tumpime kwa urais wake wa TLP.
Mkuu FMES,
Ni kweli Mrema alikubali kwamba yeye si malaika (ni ukweli kwa binadamu wote), lakini haimaanishi kwamba asiye malaika ni fisadi. Kuna makosa ya kawaida kabisa kwa kila binadamu..awe katika nafasi yoyote. Kuhitimisha kwamba Mrema ni fisadi kwasababu alikiri kwamba yeye si malaika (hata wewe na mimi tunapaswa kukiri hilo) sio sawa!
Kuhusu suala la nyumba (au mahekalu) za Sinza na Kiraracha zote kajengewa na vyama....sasa hapa nashindwa kuona ufisadi wa Mrema.
Mrema aheshimiwe, japo alipaswa kupambana ndani ya sisiem badala ya kuhama. Pia nadhani Mrema si mzuri akiwa top decision maker, rather ni mfuatiaji mzuri.
ALIKUWA RSO SHINYANGA YALIPOTOKEA MAUAJI YA VIKONGWE....NI LILE KUNDI LILILOWAJIBIKA LIKIMUHUSISHA ALIYEKUWA WAZIRI ..ALI HASSAN MWINYI,MKURUGENZI WA USALAMA....NA RSO MREMA....
ALIKAA BENCHI KABLA YA ...AKAENDA KUFUNDISHA MBWENI ..THEN MWAKA 1980 AKATEULIWA MKURUGENZI WA USALAMA CCM....THEN UBUNGE...ETS ETS....
Nyerererist/ism!Mrema tunakushukulu kwa mazuri uliyotufanyia ila kamwe hatutakusahau kwa ubabe, ukabila na uropokaji hata kwenye mambo yanayohitaji hekima kama ulivyowafanyia watu wa Shinyanga wakati ukiwa RSO kama marehem mzee Helman wa pale Kahama...siku zote alikua anasema wewe ni mnyama kuliko viongozi waliowahi kutokea serikalini kwa kumvunjia duka lake bila ya kufuatilia maelezo aliyokua ameyatoa kituo cha polisi...Pumzika kwa amani mzee helman....