TGIF: Dr. Slaa na Masha ana kwa ana (Picha)

Wanapooneshana vidole hapo juu

Slaa: Ni wewe uliyeniwekea vinasa sauti chini ya godoro
Masha: Si wewe ulianza kunipaka bungeni !
 
Masha: mzee ujue nakuheshimu sana........
Slaa: Na mimi nakuheshimu kijana...
Masha: Naweza kukufanya kitu mbaya sana...kwa kunizushia kashfa zisizokuwa na maana.
Slaa: Dogo, jina langu (Slaa) linajieleza hivyo hunifanyi chochote.
Masha: Mzeeee......Mzeeeee....
Slaa: Dogo..angalia...kidole na jicho....
Masha: Nitakupa kubwaa!!!!!!!!!
Slaa: aaaah wapi! niguse nikuchane chane na viwembe....
Masha: Jitu zima hovyoooo!!!!!!!!
Slaa: Imekuchoma hiyooooo
Slaa: Mimi ndio slaa za maangamizi bwana, nitakula nawe sahani moja hadi ubwage manyanga.
 
Hiyo ndio raha ya watanzania, mnatoana jasho kwa maslahi ya Taifa, na mkikutana mnasalimiana na kuendelea kupeana dozi. Ingekuwa watani wetu Kenya ama wabunge wa Korea Kusini hapo tungeshaona MASUMBWI.
 
Back
Top Bottom