TGIF: Aliyeandika habari hii anahitaji kufungwa!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Yaani baada ya kuandika kote wiki hii nzima bado kuna watu wanaamua kuwapotosha Watanzania kwa makusudi. Ninaamini imeandikwa na mtu wa Ikulu au Mambo ya Nje.

JK, Waziri Uingereza wajadili chenji ya rada

Na Mwandishi maalum
2nd July 2011


JK(46).jpg

Rais Jakaya Kikwete

Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Misaada ya Kimataifa ya Maendeleo wa Uingereza, Andrew Mitchel, wamekutana na kuzungumzia kuhusu fedha ambazo Serikali ya Tanzania inadai ilipwe na kampuni ya kuuza silaha ya nchi hiyo ya British Aerospace (BAE).

Katika mazungumzo hayo viongozi hao wawili wamekubaliana kuendelea na jitihada za kuishawishi BAE kuilipa Tanzania fedha hizo ambazo ni chenji iliyotokana na kuuziwa radi kwa sababu ni haki yake.

Tanzania inadai kulipwa fedha zake kiasi cha paundi za Uingereza milioni 29.5 zinazotokana na Tanzania kutozwa kiasi kikubwa zaidi kuliko kile kilichotakiwa kulipwa wakati inanunua rada kutoka BAE.

Ununuzi wa rada hiyo ulisababisha matatizo makubwa yakiwemo madai ya rushwa na hatimaye kampuni hiyo ya BAE ilifikishwa mahakamani kwa madai hayo ya kutoa rushwa katika ununuzi wa rada hiyo.

Hatimaye mahakama iliamua kuwa BAE haikutoa rushwa isipokuwa ilifanya makosa katika vitabu vyake vya mahesabu, lakini kampuni ikaamuliwa pia kulipa kiasi cha Paundi milioni 29.5 kuirudishia Tanzania ambayo ni fedha yake kihalali kwa sababu ilidhulumiwa fedha zake.

Hata hivyo, kampuni hiyo pamoja na kuamuliwa kuilipa Tanzania moja kwa moja, iliamua kutoa fedha hizo kwa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ambayo ingeleta fedha hizo Tanzania kwa njia ya kutoa huduma.

Tanzania imepiga hatua hiyo na majuzi ilitoa taarifa kali bungeni kupinga hatua hiyo ya BEA, Serikali inataka kuziingiza fedha hizo katika kuboresha elimu ikiwa ni pamoja na kununua vitabu kwa ajili ya wanafunzi na kujenga madarasa na nyumba za walimu.


CHANZO: NIPASHE
 
Jitihada zinazofanywa ni kupotosha wananchi kuwa ni chenji, pili kuficha ukweli kwasababu siku zote hadithi inaanzia mahakama ilisema. Hatuambiwi fedha ilitokaje. Jitihada zinazidi kupata nguvu kwa sababu kuna wabunge wameomba suala irudi bungeni na hapo kutazuka 'balaa'.

Pesa za BAE ni takribani bilioni 70 na ushee. Pesa za kagoda ni bilioni 40 yaani nusu ya hizo. Kinachoshangaza kama tunahitaji pesa za BAE kwa nguvu kiasi hicho kwanini hatujui zilipo za Kagoda? Kinachofanyika hapa ni kutaka kuficha ukweli na kuhakikisha pesa zinarudi mifukoni mwao.
 
Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Misaada ya Kimataifa ya Maendeleo wa Uingereza, Andrew Mitchel, wamekutana na kuzungumzia kuhusu fedha ambazo Serikali ya Tanzania inadai ilipwe na kampuni ya kuuza silaha ya nchi hiyo ya British Aerospace (BAE).

Katika mazungumzo hayo viongozi hao wawili wamekubaliana kuendelea na jitihada za kuishawishi BAE kuilipa Tanzania fedha hizo ambazo ni chenji iliyotokana na kuuziwa radi kwa sababu ni haki yake.

Tanzania inadai kulipwa fedha zake kiasi cha paundi za Uingereza milioni 29.5 zinazotokana na Tanzania kutozwa kiasi kikubwa zaidi kuliko kile kilichotakiwa kulipwa wakati inanunua rada kutoka BAE.

Ununuzi wa rada hiyo ulisababisha matatizo makubwa yakiwemo madai ya rushwa na hatimaye kampuni hiyo ya BAE ilifikishwa mahakamani kwa madai hayo ya kutoa rushwa katika ununuzi wa rada hiyo.

Hatimaye mahakama iliamua kuwa BAE haikutoa rushwa isipokuwa ilifanya makosa katika vitabu vyake vya mahesabu, lakini kampuni ikaamuliwa pia kulipa kiasi cha Paundi milioni 29.5 kuirudishia Tanzania ambayo ni fedha yake kihalali kwa sababu ilidhulumiwa fedha zake.

Hata hivyo, kampuni hiyo pamoja na kuamuliwa kuilipa Tanzania moja kwa moja, iliamua kutoa fedha hizo kwa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ambayo ingeleta fedha hizo Tanzania kwa njia ya kutoa huduma.

Tanzania imepiga hatua hiyo na majuzi ilitoa taarifa kali bungeni kupinga hatua hiyo ya BEA, Serikali inataka kuziingiza fedha hizo katika kuboresha elimu ikiwa ni pamoja na kununua vitabu kwa ajili ya wanafunzi na kujenga madarasa na nyumba za walimu.



My Take:

Kuna mtu ana matatizo kweli kichwani jamani; maana hata kasuku hawezi kurudia wimbo wenye makosa namna hii.
 
Mzee Mwanakijiji nilikuomba uliandikie jambo hilo ulipotuwekea jamvini zile nyaraka kuhusiana na Rada, ninawaelewa Viongozi wetu na waandishi wetu-hawatopenda ukweli ujulikane kamwe! Ni upotoshaji tu!Ni lini Watanzania wa vijijini watajua ukweli huo?
 
Tatizo waandishi wenu wananunulika kwa bei nafuu sana, kibaya zaidi wanasahau hata nafasi ya heshima ya taaluma zao.
 
Mkakati unaendelea kwa kusema, mahakama iliamua BAE haikutoa rushwa ila ilifanya makosa ktk vitabu vyake, A. Chenge na Idrissa Rashid waonekane wasafi sana, watu makini wanawasingizia.
 
yani membe keshakuwa chizi juu ya hizi ela, wasiojua wanaona ni stahiki yetu kulipwa kupitia serikali yetu. i say no, A BIG NO! zikipitia serikalini tu, kwisha kazi. itapotea kimiujiza hiyo ela, hatutapata hata pa kuhoji, hatutasikilizwa popote. INANIUMA SANA KUONA UKWELI UNAPOTOSHWA NA WAHUSIKA HAWACHUKULIWI HATUA.
 
Mkakati unaendelea kwa kusema, mahakama iliamua BAE haikutoa rushwa ila ilifanya makosa ktk vitabu vyake, A. Chenge na Idrissa Rashid waonekane wasafi sana, watu makini wanawasingizia.
CHENGE ndiye aliye toa ushauri kuwa account ya BoT "Zifungiwe" na BAE ili kama serikali ikikataa kulipa iwe rahisi kwa BAE kuchukua pesa zao Jamani mbona Chenge hana huruma na sisi Sasa kapeleka ushauri wa kisheria ili kuwalipa DOWAS si angeacha tu washughurike wenyewe " dah I hate this man !!"
 
Pamoja na jitihada zote wanazofanya Rada ni mkuki wa moto wao serikali wajiandae kugumia tu maana haukwepeki
 
Jitihada zinazofanywa ni kupotosha wananchi kuwa ni chenji, pili kuficha ukweli kwasababu siku zote hadithi inaanzia mahakama ilisema. Hatuambiwi fedha ilitokaje. Jitihada zinazidi kupata nguvu kwa sababu kuna wabunge wameomba suala irudi bungeni na hapo kutazuka 'balaa'.

Pesa za BAE ni takribani bilioni 70 na ushee. Pesa za kagoda ni bilioni 40 yaani nusu ya hizo. Kinachoshangaza kama tunahitaji pesa za BAE kwa nguvu kiasi hicho kwanini hatujui zilipo za Kagoda? Kinachofanyika hapa ni kutaka kuficha ukweli na kuhakikisha pesa zinarudi mifukoni mwao.

Hivi hujui CCM walivyo?
 
.........Serikali inataka kuziingiza fedha hizo katika kuboresha elimu ikiwa ni pamoja na kununua vitabu kwa ajili ya wanafunzi na kujenga madarasa na nyumba za walimu.

CHANZO: NIPASHE

Mi siamini serikali haiko serious na elimu na walimu wetu kiasi hiki.

  • Kwa nn kununua vitabu na kujenga nyumba za walimu mpaka pesa a BAE.
Tujiulize kwenye bajeti ya sasa ni kiasi gani kimetengwa kujenga nyumba na walimu na kununua vitabu . Yaaani mpaka pesa iliyokuwa misallocated na wala rushwa imekamatwa ndo wanakuja na sababu tamu.
 
jamani hapa JF ni masikio pa watu wengi. Tunaomba ukweli pamoja na nyaraka zote ziwekwe hapa kama vyombo vya habari vitaendelea kuandika ya wanasiasa wa magamba.

sisi hapa naamini tuko wengi kuliko hizo nakara za magazeti yanayotumika kupotosha ukweli. Tutatumika kama magazeti kuufikisha ukweli utakaowekwa humu.

Mungu tusadie katika haya mapambano ya kutafuta haki na utu mpya wa wanyonge wa kitanzania.
 
Mkuu MM,

Haya masuala ya rada, kagoda, meremeta,deepgreen, IPTL, EPA, Kiwira, Downs (hatimaye Symbion), ukwapuaji wa nyumba za watanzania, safari za nje za raisi, mawaziri kukaa mahotelini kwa gharama kubwa, shule za kata, siasa za udini, kumkashifu BABA WA TAIFA, nk nk kwa ukweli wa Mungu yanaumiza sana. Kwa nini yote haya ? kwa nini angalau hayapungui kama hayawezi kwisha? tatizo hasa ni nini ? Ni CCM, ni watanzania, ni akili zetu finyu au ni kweli kama wengine wanasema tumelogwa ? Au ni mchanganyiko wa mengi ?

Tufanyeje kujinasua na maafa haya ?

Mimi bado naanimi tukipata katiba ya watu italeta mabadiliko na kutuelekeza tunakotaka.

Vile vile katiba ya watu itatuwezesha kuchukua hatua muafaka kwa wahalifu wooote na uhalifu woote huu.

Sijakata tamaa!
 
Mkuu MM,

Haya masuala ya rada, kagoda, meremeta,deepgreen, IPTL, EPA, Kiwira, Downs (hatimaye Symbion), ukwapuaji wa nyumba za watanzania, safari za nje za raisi, mawaziri kukaa mahotelini kwa gharama kubwa, shule za kata, siasa za udini, kumkashifu BABA WA TAIFA, nk nk kwa ukweli wa Mungu yanaumiza sana. Kwa nini yote haya ? kwa nini angalau hayapungui kama hayawezi kwisha? tatizo hasa ni nini ? Ni CCM, ni watanzania, ni akili zetu finyu au ni kweli kama wengine wanasema tumelogwa ? Au ni mchanganyiko wa mengi ?

Tufanyeje kujinasua na maafa haya ?

Mimi bado naanimi tukipata katiba ya watu italeta mabadiliko na kutuelekeza tunakotaka.

Vile vile katiba ya watu itatuwezesha kuchukua hatua muafaka kwa wahalifu wooote na uhalifu woote huu.

Sijakata tamaa!

Kaka usisahau wana mpango wa kuimega mbuga ya Selous karibia hecta Elfu 35 kwa ajili ya kuchimba Uranium then hv majuzi wamekataa kujenga bara bara ya lami inayopita mbugani......bado kufa tu.
 
Chakusikitisha wanadai hela ambazo wao walizitoa sadaka. mm naombea BAE waendelee na msimamo wao,hizo pesa zikija tu wataanza kulipana posho. kweli serikali inafanya mambo ambayo hata mtoto wa drs la 3 hawezi kufanya, wamewakumbatia akina chenge alafu wanajikosha kwetu eti hela hizo ni alali yetu madai yao ni chenji.

Alafu nipashe ni wapotoshaji sana huwa wanaibeba sana serikali hata kwa vitu vya kijinga,badala waeleze ukweli wao waupotosha uma thanx God wtz sasa tumeamka na dr.slaa kasema hatudanganyiki.
 
Ivi viongozi wetu wamerogwa na nani jamani wanatia huruma.malipo ni duniani kila siku ni selikari ndo yenye matatizo,lnabinafsishwa maliasili,madini bado sisi wananchi.kwa iyo mkukuta ni kama series(filamu)ilikuwa moja,sasa 2po pili na ya tatu mwakani...
 
Back
Top Bottom