adakiss23
JF-Expert Member
- Jan 23, 2011
- 4,477
- 4,270
Leo TFF wameongeza muda wa usajili hadi 15th Aug ambalo lilitakiwa lifungwe leo 10th Aug saa 6usiku. Wametumia vigezo gani kuongeza muda huo? Je hawana kalenda ya matukio? Au kwa kuwa Yanga hawajakamilisha usajili wa mchezaji wa 5 wa kigeni? Simba washakamilisha usajili wa kigeni cz kuna Twite Mudde Okwi Kanu na Sunzu. Azam washafunga usajili siku nyingi cz wana Blackberry Shikanda Balou n pacha wake Tcheche. Yanga bado m1 na bado mambo hayajaeleweka cz wanahitaji beki na Bin Kleb alikuwa Rwanda Rage akamuwahi akamsajili Twite akatoka akaenda kampala kakosa ikabidi arudi Kigali kurekebisha mambo. Sasa mpaka leo mchana mambo hayasomeki itakuwaje?? Ndo ikatumwa memo kwa prezdaa Tenga arefushe muda 'gumashi' lifanyike. Kwa mtindo huu ligi inaashiria kutakuwa na magumashi ya kutosha. TFF mpaka sasa hawajatoa ratiba ya ligi Kwanini? Wanasubiri nn? Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki soka letu!
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums