TFF na Uamuzi wa Busara Usio na Busara

Baba Kiki

JF-Expert Member
May 31, 2012
1,544
940
Jinsi sakata la mchezaji wa zamani wa Simba Hassan Ramadhan Kessy kujiunga na Yanga lilivyoshughulikiwa na inayoitwa Kamati ya Sheria na Haki za wachezaji inaonyesha ni namna gani safari ya Tanzania kuondoa ubabaishaji michezoni ilivyo ngumu na hivyo kutishia mustakabali wa maendeleo ya mchezo kwa ujumla. Hata watu wataalamu na wabobezi katika sheria na uongozi wanaotazamiwa kusaidia kuondoa migogoro na ujanja ujanja kwenye michezo, bado wao wanakuwa sehemu ya tatizo.

Suala la Kessy kwa mfano badala ya kumalizwa limeachwa tena pending bila sababu za msingi. Huu ni mlango wa mgogoro na kelele wakati ligi inaendelea. Sehemu ya taarifa ya Kamati inanukuliwa ikisema eti;

"TFF inafuatilia na kuangalia haki ya Simba namna ya kupata haki yake baada ya kuwasilisha madai kuhusu kuvunja mkataba na mwajiri wake wa zamani.
Kanuni hazimzuii mchezaji kuendelea kucheza kwa hoja ya madai badala yake suala hilo linaweza kumalizwa wakati mashindano yanaendelea
"

Badala ya watu kufuatilia matokeo na ufundi wa timu ktk ligi, bado kuna nafasi ya kuendelea kufuatilia issue ya Kessy, kwamba leo hivi, kesho vile. Haya ndio mambo ambayo hayana maana sana kwenye mpira. Kamati ilipaswa kufanya yafuatayo tu na kufunga mjadala kabisa;

1. Kujiridhisha kama Kessy alisajiliwa na Yanga huku akiwa bado na mkataba na Simba au la
2. Kama jibu ni ndiyo sheria na kanuni zinasemaje? Alipaswa kulipa fidia? Kiwango cha fidia
wanayodai Simba ni sahihi. Kama sivyo, kipi ni kiwango sahihi?
3. Kuamua kuwa kama madai ya Simba ni kweli, Kessy na mwajiri wake wanapewa muda gani
kulipa kiwango hiki?
4. Kama sivyo, kutupilia mbali madai ya Simba na kumwidhinisha Yanga bila sharti lolote.

Hii ya kuachia vitu nusu-nusu, inatafsirika kama ni kupima upepo, kuona hukumu itapokelewaje. Kama nilisema hapo juu, ni mlango wa kutengeneza zengwe lisilo na sababu wala tija yoyote.
Tujifunze kuongoza vitu kwa utaratibu na kutoa hukumu stahili badala ya kutengeneza mazingira ya kuridhisha kila upande ktk shauri.
 
Kuendelea kumzua Kessy ni kuua kiwango cha mchezaji na hilo ndilo linaua kiwango cha wachezaji wetu, kiufupi timu ziache ubabaishaji, Kessy akizuiliwa kucheza Simba itafaidika na nini???
 
kwa hiyo ulitaka kessy asicheze mpira forever?
Na nyie mnao mtumia mavugo huku bado akiwa na mkataba halali na timu yake,
Soccer siyo mchezo wa kukomoana kama nyie wamatopeni mnavyo fikiri,
 
Kuendelea kumzua Kessy ni kuua kiwango cha mchezaji na hilo ndilo linaua kiwango cha wachezaji wetu, kiufupi timu ziache ubabaishaji, Kessy akizuiliwa kucheza Simba itafaidika na nini???

Suala halipo kwa Kessy kucheza au kutokucheza ili kulinda kiwango chake. Issue ni kumaliza issue yake bila kumung'unya maneno kwa sababu iko wazi. Kuliacha hili jambo liendelee kwa kile kinachodaiwa eti ''namna Simba itakavyopata haki yake'' ndio palipo na tatizo. Kama Simba ina haki, Kamati ingeamua tu moja kwa moja kuwa Kessy anapaswa kuilipa Simba Kiasi fulani na amepewa siku kadhaa awe amelipa..... na kamati imeamruhusu aendelee kucheza kulinda kiwango chake. Kama sivyo madai ya Simba yangetupiliwa mbali kwa kusema Kamati imejiridhisha kuwa Kessy aliingia mkataba na Yanga baada ya kumaliza mkataba wake na Simba. Full stop. Ndivyo wenzetu wanavyofanya, ni ama nyeupe au nyeusi.

Lakini kuacha tu vitu nusu nusu kama 'kuangalia namna Simba itakavyopata haki yake' ni dalili ya kutumia busara isyo na busara..
 
kwa hiyo ulitaka kessy asicheze mpira forever?
Na nyie mnao mtumia mavugo huku bado akiwa na mkataba halali na timu yake,
Soccer siyo mchezo wa kukomoana kama nyie wamatopeni mnavyo fikiri,


Fikiria vizuri. Soma kwa akili, punguza mzuka wa kishabiki. Kuwa na mapenzi na timu fulani hakukuzuii kutumia akili au kuwa mwenye mtazamo mpana.
 
Jamal Malinzi ana ajenda mbaya na soka laTanzania. Hana nia njema na ndio maana maamuzi yake yamekuwa ya ajabuajabu. Anajua anachokifanya na katika hili yaonekana kuna mtu au watu wanamkingia kifua. Huyu Bwana tuliambiwa TAKUKURU wanachunguza maamuzi yake kuhusu Upangaji wa Matokeo. Hadi leo TAKUKURU wapo kimyaa. Na hili la chombo adhimu cha kupiga vita rushwa kukaa kimya linayufanya tuanze kuzua tafsiri potofu.
Juzi wakati JPM alipokuwa Mwanza alimkaribisha Diwani wa Nyamagana. Diwani alimshukuru JPM kwa kupigania uwanja wa Nyamagana usigeuzwe kuwa Hoteli. Yule Diwani pia aliongelea hela za Halmashauri zilizoliwa na watu wa TFF kwa ajili ya nyasi bandia. Naona kama lilipotezewa kiaina na wala hakukuwa na maagizo yoyote yale. Nimekuwa najiuliza sana kuhusu huyu Bwana Jamal Malinzi, je ana mtu anamkingia kifua? Hivi kwa nini anaendelea kufumbiwa macho na vyombo vya dola?
Hapa tunaona maajabu mengine ya kutaka kuvuruga soka kwa makusudi. Mimi naomba tuweke kando mahaba yetu ya kisoka ili kanuni na taratibu zifuatwe. Hili suala la Kessy lisifanye watu wakiuke kanuni na taratibu za soka. Kama Kessy ni haki yake kuchezea Yanga na amefuta taratibu kwa nini vikao vya maamuzi vicheleweshe hayo maamuzi?
 
Kuendelea kumzua Kessy ni kuua kiwango cha mchezaji na hilo ndilo linaua kiwango cha wachezaji wetu, kiufupi timu ziache ubabaishaji, Kessy akizuiliwa kucheza Simba itafaidika na nini???
Hans Pope ndio anataka kumkomoa Kessy, sidhani kama Simba wana haki kwenye hiyo issue.
 
Tff mi sina hamu nao kabisa. Naiona FAT inakuja. Bongo hatutafika mbali kisoka kabisa. Kama baba ndani ya nyumba akiwa mwoga wa maamzi hiyo nyumba itabomoka tu
 
Fikiria vizuri. Soma kwa akili, punguza mzuka wa kishabiki. Kuwa na mapenzi na timu fulani hakukuzuii kutumia akili au kuwa mwenye mtazamo mpana.

linapokuja suala la mchezaji wa simba anataka kuhamia yanga viongozi wa simba lazima waanzishe figisu pasipo sababu za msingi, deo njohole, mogela, gaga, kizota, chuji, ngasa etc tena hawa ni baadhi, wote walionja machungu na figisu figisu za simba
Kwanza kessy mlimpiga na kumfukuza mapema kabisa hata kabla ligi haijaisha, baada ya kusikia kasaini yanga figisu likaanza
 
Hizo fedha wanamdai Kessy sio club ya Yanga. Lakini wanasahau kwamba hata wao hawakutimiza kumhusu Kessy.
Hay yataenda lakini yataisha au kufa natural death!
Mtu kama Hans Poppe anapenda kujenga picha kwamba suala lipo upande wao kisheria wakati sio kweli.
Miaka nenda rudi Simba wanapigwa chinI mambo ya uhamisho
 
Hizo fedha wanamdai Kessy sio club ya Yanga. Lakini wanasahau kwamba hata wao hawakutimiza kumhusu Kessy.
Hay yataenda lakini yataisha au kufa natural death!
Mtu kama Hans Poppe anapenda kujenga picha kwamba suala lipo upande wao kisheria wakati sio kweli.
Miaka nenda rudi Simba wanapigwa chinI mambo ya uhamisho

Enhe, hapo sasa ndio kwenye tatizo. Uamuzi unatakiwa ukamilike sio kuacha mambo yafe yenyewe.
 
Natamani wadau wajue kinachojadiliwa hapa ni aina ya hukumu ambayo haijakamilika bila sababu zozote za msingi. Huu ni mlango wa mizengwe. Hatujadili haki ilistahili kwenda wapi na kwa nani, maana TFF hawajatupa msingi wa maamuzi yao kama Kessy aliingia Yanga akiwa na mkataba au la. Hadi sasa mimi sijui, kamati ya TFF imeshindwa kutujulisha hili.
 
Enhe, hapo sasa ndio kwenye tatizo. Uamuzi unatakiwa ukamilike sio kuacha mambo yafe yenyewe.
Kwa upande was TFF wamefanya ya kwao! Hayo madai ndiyo yatakufa natural death maana hayana mashiko hata kidogo. Simba wanadai na Kessy anadai
 
Kwa upande was TFF wamefanya ya kwao! Hayo madai ndiyo yatakufa natural death maana hayana mashiko hata kidogo. Simba wanadai na Kessy anadai

Natamani kusikia unazungumzia nini kuhusu "utabiri" wako wa jambo hili kufa natural death? Wapenzi wa mpira tupunguze ushabiki kwenye vitu vya kutumia kanuni na miongozo iliyowekwa. Kwa jambo hili TFF wanathibitisha kuwa kuna watu ndani yake wanafanya kazi kwa niaba ya Yanga. Simba wameprove madai yao, tena baada ya kukomaa watu jambo liko wazi kabisa. Ni aibu kwa mamlaka za soka
 
Natamani kusikia unazungumzia nini kuhusu "utabiri" wako wa jambo hili kufa natural death? Wapenzi wa mpira tupunguze ushabiki kwenye vitu vya kutumia kanuni na miongozo iliyowekwa. Kwa jambo hili TFF wanathibitisha kuwa kuna watu ndani yake wanafanya kazi kwa niaba ya Yanga. Simba wameprove madai yao, tena baada ya kukomaa watu jambo liko wazi kabisa. Ni aibu kwa mamlaka za soka
Hili ndilo soka letu lilivyo. Ukizubaa unaliwa!!!
 
Mkuu Baba Kiki unafikiri watarudi kutetea utabiri wao.Wamekuja na mpya sasa kwamba ni pesa ndogo sana. Mkataba ulibakiza siku 5 umetozwa milioni 10 kila siku unadai ni pesa ndogo. Wangeaandika barua tu kama kuidhinishiwa kama kanuni zinavyodai
hayo yote yasingetokea. Kiburi na tabia ya kubebwa imewaponza. Hongera kwa kukomaa mpaka haki imepatikana. Although justice delayed is justice denied.
 
Natamani kusikia unazungumzia nini kuhusu "utabiri" wako wa jambo hili kufa natural death? Wapenzi wa mpira tupunguze ushabiki kwenye vitu vya kutumia kanuni na miongozo iliyowekwa. Kwa jambo hili TFF wanathibitisha kuwa kuna watu ndani yake wanafanya kazi kwa niaba ya Yanga. Simba wameprove madai yao, tena baada ya kukomaa watu jambo liko wazi kabisa. Ni aibu kwa mamlaka za soka
Hahaha hiyo natural death yenyewe. Kutoka billion hadi million 50?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom