TFDA yatangaza dawa hatari

Baba Mtu

JF-Expert Member
Aug 28, 2008
871
168
MAMLAKA ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imesitisha kwa muda utengenezaji, uingizaji, usambazaji na matumizi ya dawa zenye viwango duni vya ubora, baada ya kubainika kwenye ukaguzi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.

Dawa, matoleo, mtengenezaji na tatizo la dawa hizo kwa mujibu wa taarifa ya TFDA, ni ya sindano ya Gentamycin Sulphate 80mg/2ml Ampules, iliyotengenezwa na Kampuni ya Leshan Sanjiu-Longmarch Pharmaceuticals ya China ambayo maandishi yake kwenye vichupa yanafutika kirahisi.

Nyingine ni tembe za Coldril iliyotengenezwa na Kampuni ya Shelys Pharmaceuticals ya Tanzania toleo la 9041 ambayo tembe hizo zimegandamana; tembe za Pen-V pia za Shelys toleo la 9027 na 9034 ambazo zimebadilika rangi kutoka nyeupe na kuwa njano isiyokoza.

Dawa zingine ni MES Syrup ya ZENUFA Laboratories ya Tanzania toleo LM0021 ambayo inavuja na vifuniko vyake vina kutu; Methyldopa (Dopamet) - 250 iliyotengenezwa na Kampuni ya Medochemie ya Cyprus toleo A3A002 na A3D018 ambayo lebo zake zinabanduka kirahisi na vidonge vyake vimeota kuvu.

Dawa zingine zisizotakiwa ni Phenoxymethylpenicillin Potassium (Medopen) – 250 pia za Medochemie ya Cyprus toleo la P2K049 ambazo zimebadilika rangi nyeupe kuwa ya njano isiyokoza.

Pia tembe za Amoxicillin zilizotengenezwa na Zheijian Holley Nanhu Pharmaceuticals ya China toleo 090901, ambazo ‘blister' ya ndani haina namba ya toleo, siku ya kutengenezwa wala muda wa kwisha matumizi.

Tembe za Doxycyline Hyclate zilizotengenezwa na Zhejiang toleo la 100705 , kasha lake la hifadhi halina siku ya kutengenezwa wala ya kwisha matumizi na huku pakiti yake ikiwa na tarehe zote hizo na dawa nyingine yenye matatizo hayo ni Dyclomax (Diclofenac) iliyotengenezwa na Kampuni ya Medreich ya India toleo namba 460156 ambayo ‘kasha lake pia lina tatizo kama la dawa ya hapo juu.

Kutokana na upungufu huo, wananchi wameonywa wasitumie kabisa dawa hizo huku wenye maduka ya dawa wakitakiwa wazirudishe walikozinunua mara moja na walioziagiza wazitoe mara moja sokoni na kuwasiliana na TFDA wapewe utaratibu wa kuziharibu.

"Pamoja na maelekezo yaliyotolewa, Mamlaka inafanya uchunguzi wa kina kwenye maabara na itachukua hatua zaidi za kisheria baada ya kukamilisha uchunguzi wa dawa hizo," ilisema taarifa iliyotolewa na ofisi ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo.

Mamlaka ilitoa muda wa miezi sita kuanzia Januari mosi kwa wahusika wa utengenezaji, uingizaji na usambazaji wa dawa hizo, kuhakikisha kuwa dawa zao hazina udhaifu kama uliobainika na kuwataka wananchi kutoa taarifa mara moja TFDA wanapogundua upungufu kama huo.

"Taarifa zitolewe ofisi za TFDA barabara ya Mandela, EPI Mabibo External, Dar es Salaam na ofisi za Kanda zilizopo mtaa wa Nkrumah, Mwanza, mtaa wa Sakina – Arusha na jengo la ofisi ya Mifugo Mkoa wa Mbeya.

http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=13428
 
Hii habari njema sana. Swali ni je, TFDA wanampa hii taarifa? Mwananchi (mgonjwa), daktari, mfamasia au wizara ya afya?
 
Hii habari njema sana. Swali ni je, TFDA wanampa hii taarifa? Mwananchi (mgonjwa), daktari, mfamasia au wizara ya afya?

Wote hao kwa ujumla wao ndio wanaopewa taarifa hii
 
Hii habari njema sana. Swali ni je, TFDA wanampa hii taarifa? Mwananchi (mgonjwa), daktari, mfamasia au wizara ya afya?
Kutokana na upungufu huo, wananchi wameonywa wasitumie kabisa dawa hizo huku wenye maduka ya dawa wakitakiwa wazirudishe walikozinunua mara moja na walioziagiza wazitoe mara moja sokoni na kuwasiliana na TFDA wapewe utaratibu wa kuziharibu.
 
swali Je tutazijuaje??? au changa la macho hiloooooooooooooooooooooo,, Inatakiwa kuzikama na kufatilia kwenye hizo Kampuni kama mimi kwenye duka langu nina stock kubwa sana na ndio zinaniweka mjini leo nizirudishe aaaaa NO. Ila Ushauri wananchi tumieni Hospitali za Gov tya Tanzania na sio za Private au maduka ya dawa au uende kwenye Hospital ya Private ya Ukweli sio zile za Street na maduka ya ukweli sio yale ya Street
 
swali Je tutazijuaje??? au changa la macho hiloooooooooooooooooooooo,, Inatakiwa kuzikama na kufatilia kwenye hizo Kampuni kama mimi kwenye duka langu nina stock kubwa sana na ndio zinaniweka mjini leo nizirudishe aaaaa NO. Ila Ushauri wananchi tumieni Hospitali za Gov tya Tanzania na sio za Private au maduka ya dawa au uende kwenye Hospital ya Private ya Ukweli sio zile za Street na maduka ya ukweli sio yale ya Street

Kwa taarifa ni kwamba hizi dawa fake zipo hata Govt. Hospitals!!!!!
 
TFDA fanyeni kazi msilete usanii hapa! Nyie ndio mnaoregister importers wa hizo dawa na mmewekwa kwenye ports kujua nani kaleta nini na batch gani...sasa mnatutangazia sisi ili iweje? wafateni hao watu waziotoe kwenye circulation. Shida yenu mnachumia tumboni tu....mtu akitaka huduma rushwa kwanza...mmeshamaliza kuregister products za ORIFLAME??
Shame on you!

NAOMBA NIWAKUMBUSHE KAZI ZENU /MNAZOLIPWA MSHAHARA...KAMA MMESHINDWA ONDOKENI WENGINE WAJE WAZIFANYE.
HII IMETOKA KWENYE WEBSITE YENU NA MSIENDE KWENYE LUNINGA KUTUAMBIA ETI MIPAKA YA TANZANIA IPO "PORUS". HATUTAKI KUSIKIA UPUUZI.
Functions of TFDA

Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA), is a regulatory body responsible for controlling the quality, safety and effectiveness of food, drugs, herbal drugs, cosmetics and medical devices. It is established under Tanzania Food, Drugs and Cosmetics Act No. 1 of 2003, after repealing the Pharmaceutical and Poisons Act No. 9 of 1978 (which established the Pharmacy Board) and Food {Control of Quality} Act No. 10 of 1978 (which established the National Food Control Commission). TFDA, a semi-autonomous body under the Ministry of Health and Social Welfare, became operational on 1st July 2003.
The Mission of TFDA is to protect the health of consumers against hazards associated with food, drugs, herbal drugs, cosmetics and medical devices. This mission is achieved by performing the following core activities
Product Evaluation and Registration
In Tanzania drugs, prepackaged food, cosmetics, herbal drugs, medical devices and food supplements are evaluated and registered by the Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA) before being approved for distribution and marketing in the country. The objective of the evaluation and registration is to ensure that only safe, quality and efficacious products are approved for use in the country. This section provides information on all aspects of the product evaluation and egistration.
Premises Registration and Licensing
The Directorate of Inspection and Surveillance is responsible with ensuring that all dealings in food, drugs, herbal drugs, cosmetics and medical devices are done after obtaining relevant licenses and permits. This section of the site gives details on the types of licenses and permits issued by TFDA and how to obtain them.
Inspection and Surveillance The Directorate of Inspection and Surveillance is responsible with inspecting manufacturers, wholesalers and retailers and clinical trials sites and at port of entry to ensure that standard requirements for food, drugs, herbal drugs, cosmetics and medical devices are complied to. This section of the site describes the work of the Inspectorate.
Import and Export Control
The TFDA control import and export of food, drugs, herbal drugs, cosmetics and medical devices in order to ensure their safety, quality and effectiveness. This section of the site gives details on the procedures to be followed by importer and exporters.
Post Marketing Product Risk Analysis
TFDA continually monitor safety of food, drugs, herbal drugs, cosmetics and medical devices available on the Tanzania market. This section of the site explains how TFDA conduct Post marketing product risk analysis.
 
Shellys mnatuangusha sana. Kumbe na ninyi mnachezea afya zetu kama wachina na wahindi!
 
Kwa nini tfda hawatangazi dawa hatari za kienyeji zikiwemo matunguli yanayotumika na wachawi kuua watu???
Siku hizi nimesikia hata waganga wa kienyeji wanasajiliwa wizara ya afya lakini zipo dawa zao ambazo ni hatari na zinaua!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom