Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,314
- 33,108
MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa amesema hatashangaa siku moja vyama vya upinzani vikishinda uchaguzi na kushika madaraka.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma kuhusu maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini, Tendwa alisema "kushika dola ndilo lengo la kila chama cha siasa".
Alisema yeye akiwa mlezi wa vyama vya saisa nchini angefurahi kuona vyama hivyo vinakua na kutimiza lengo la kutwaa dola au nafasi za uongozi katika mamlaka mbalimbali za nchi.
"Hili haliwezi kuwa ni jambo la kushangaza, sheria iko wazi kabisa kwamba lengo la kila chama cha siasa ni kushika dola au kuongoza mamlaka nyingine za kiserikali kwa mujibu wa sheria za nchi, na mimi nikiwa mlezi wa vyama vya siasa kama mlivyosema ningefurahi wapambane washinde ili wasifanye fujo,"alisema Tendwa.
Kuhusu miaka 20 ya demokrasia ya vyama vingi nchini, Msajili huyo wa Vyama vya Siasa alisema maadhimisho hayo yataanza Julai 1, mwaka huu na kwamba yatatumika kufanya tathmini ya zama na matukio mbalimbali yaliyotokea katika kipindi hicho pia mchango wa vyama vingi katika demokrasia ya nchi.
Tendwa alisema katika uzoefu wake akiwa msajili wa vyama vya siasa amebaini kuwapo kwa umuhimu wa sheria ya vyama kufanyiwa marekebisho makubwa ili kuongeza tija ya uwapo wa ofisi yake na vyama hivyo kwa ujumla wake.
Alisema katika mchakato wa uandishi wa Katiba Mpya, watapendekeza Msajili wa Vyama vya Siasa na naibu wake baada ya kuteuliwa waidhinishwe na mamlaka nyingine kama Bunge ili kuwapa nguvu ya kiutendaji na uwajibikaji.
"Hili litaondoa lawama za mara anafanya hili au lile ili kumridhisha fulani kwani aliteuliwa na Fulani, kwahiyo sisi tunadhani mtu akiidhinishwa na chombo kingine basi anakuwa na uhuru wa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kwa ufanisi zaidi," alisema.
Kuhusu vyama vya siasa, Tendwa alisema lazima uwapo utaratibu wa vyama visivyo na tija ‘kushuka daraja' kila baada ya uchaguzi kufanyika na kwamba hatua hiyo itavilazimisha vyama vyete kufanya shughuli za kisiasa.
CHANZO: Tendwa: Sitashangaa siku wapinzani wakichukua nchi
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma kuhusu maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini, Tendwa alisema "kushika dola ndilo lengo la kila chama cha siasa".
Alisema yeye akiwa mlezi wa vyama vya saisa nchini angefurahi kuona vyama hivyo vinakua na kutimiza lengo la kutwaa dola au nafasi za uongozi katika mamlaka mbalimbali za nchi.
"Hili haliwezi kuwa ni jambo la kushangaza, sheria iko wazi kabisa kwamba lengo la kila chama cha siasa ni kushika dola au kuongoza mamlaka nyingine za kiserikali kwa mujibu wa sheria za nchi, na mimi nikiwa mlezi wa vyama vya siasa kama mlivyosema ningefurahi wapambane washinde ili wasifanye fujo,"alisema Tendwa.
Kuhusu miaka 20 ya demokrasia ya vyama vingi nchini, Msajili huyo wa Vyama vya Siasa alisema maadhimisho hayo yataanza Julai 1, mwaka huu na kwamba yatatumika kufanya tathmini ya zama na matukio mbalimbali yaliyotokea katika kipindi hicho pia mchango wa vyama vingi katika demokrasia ya nchi.
Tendwa alisema katika uzoefu wake akiwa msajili wa vyama vya siasa amebaini kuwapo kwa umuhimu wa sheria ya vyama kufanyiwa marekebisho makubwa ili kuongeza tija ya uwapo wa ofisi yake na vyama hivyo kwa ujumla wake.
Alisema katika mchakato wa uandishi wa Katiba Mpya, watapendekeza Msajili wa Vyama vya Siasa na naibu wake baada ya kuteuliwa waidhinishwe na mamlaka nyingine kama Bunge ili kuwapa nguvu ya kiutendaji na uwajibikaji.
"Hili litaondoa lawama za mara anafanya hili au lile ili kumridhisha fulani kwani aliteuliwa na Fulani, kwahiyo sisi tunadhani mtu akiidhinishwa na chombo kingine basi anakuwa na uhuru wa kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kwa ufanisi zaidi," alisema.
Kuhusu vyama vya siasa, Tendwa alisema lazima uwapo utaratibu wa vyama visivyo na tija ‘kushuka daraja' kila baada ya uchaguzi kufanyika na kwamba hatua hiyo itavilazimisha vyama vyete kufanya shughuli za kisiasa.
CHANZO: Tendwa: Sitashangaa siku wapinzani wakichukua nchi