Wapinzani `wamechacha` -Tendwa
2009-01-04 12:49:22
Na Simon Mhina
Msajili wa vyama vya siasa, John Tendwa, amesema baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani `wamechacha` hudiriki kumuomba nauli ya daladala ili waweze kurudi majumbani mwao.
Tendwa alitoa madai hayo alipozungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam kuhusu ukaguzi wa mahesabu ya mapato na matumizi ya vyama vya siasa nchini.
Alisema vyama vingi vya siasa vimejitahidi kuleta mahesabu ofisini kwake baada ya kukaguliwa, japokuwa kuna matatizo ya hapa na pale.
Hata hivyo, alisema vyama ambavyo havipati ruzuku ya serikali amevisamehe japokuwa navyo pia sheria inavitaka kukaguliwa na kuwasilisha taarifa ya mapato na matumizi ofisini kwake.
Alipoulizwa ni kwa vipi wao wamesamehewa, msajili huyo alijibu ``Mambo mengine ni kujisumbua tu na kutafuta lawama zisizo na faida, hebu fikiri, kuna wenyeviti wa vyama na makatibu wao wanakuja hapa ofisini, halafu wananiomba nauli, wanasema hawana senti ya kupandia daladala, sasa watu kama hao unawadai mahesabu yepi?``.
Alipoulizwa viongozi hao wakishamuomba nauli hufanyaje, Tendwa alisema hulazimika kuchomoa pochi yake na kuwakatia kitu kidogo.
``Kwa kweli kama kuchacha, kuna viongozi wa vyama vya upinzani wamechacha kwelikweli hadi wananuka, lakini mimi nitafanyaje kwa vile na mimi ni binadamu
SOURCE: Nipashe
2009-01-04 12:49:22
Na Simon Mhina
Msajili wa vyama vya siasa, John Tendwa, amesema baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani `wamechacha` hudiriki kumuomba nauli ya daladala ili waweze kurudi majumbani mwao.
Tendwa alitoa madai hayo alipozungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam kuhusu ukaguzi wa mahesabu ya mapato na matumizi ya vyama vya siasa nchini.
Alisema vyama vingi vya siasa vimejitahidi kuleta mahesabu ofisini kwake baada ya kukaguliwa, japokuwa kuna matatizo ya hapa na pale.
Hata hivyo, alisema vyama ambavyo havipati ruzuku ya serikali amevisamehe japokuwa navyo pia sheria inavitaka kukaguliwa na kuwasilisha taarifa ya mapato na matumizi ofisini kwake.
Alipoulizwa ni kwa vipi wao wamesamehewa, msajili huyo alijibu ``Mambo mengine ni kujisumbua tu na kutafuta lawama zisizo na faida, hebu fikiri, kuna wenyeviti wa vyama na makatibu wao wanakuja hapa ofisini, halafu wananiomba nauli, wanasema hawana senti ya kupandia daladala, sasa watu kama hao unawadai mahesabu yepi?``.
Alipoulizwa viongozi hao wakishamuomba nauli hufanyaje, Tendwa alisema hulazimika kuchomoa pochi yake na kuwakatia kitu kidogo.
``Kwa kweli kama kuchacha, kuna viongozi wa vyama vya upinzani wamechacha kwelikweli hadi wananuka, lakini mimi nitafanyaje kwa vile na mimi ni binadamu
SOURCE: Nipashe