Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Wakiondoa sababu nyingine zozote vi "nzi" vinaripoti kwa uhakika mkubwa kuwa Msajili wa Vyama vya siasa nchini Bw. John Tendwa na Waziri anayeshughulikia mambo ya siasa Bunge Bw. Phillip Marmo wameamua kuhakikisha kuwa chama kipya cha siasa nchini ambayo kinakuja na fikra mpya za kulirudisha taifa mikononi mwa wananchi CCJ hakipati usajili wa kudumu.
Akizungumza mapema leo na vyombo vya habari Bw. Tendwa amezungumza kwa kejeli kuwa ofisi yake haina fedha za kwenda kufanya uhakiki wa wanachama mikoani kama sheria inavyotaka akidai kuwa kutokana na shughuli mbalimbali za uchaguzi haitowezekana kufanya hivyo kwa sasa.
Hata hivyo, vi'nzi" hivyo vinadokeza kuwa msimamo huo wa Tendwa unatokana na maelekezo ya ushauri kutoka kwa Marmo ambaye kutokana na nafasi yake anatishiwa na mwanasiasa mmoja huko Mbulu ambaye ameonesha nia ya kutaka kugombea jimbo la MBulu kwa kupitia CCJ na ambaye tayari anaonekana kukubalika na hivyo, usajili wa CCJ utatishia moja kwa moja nafasi ya Bw. Marmo.
Pamoja na hilo uongozi wa CCJ uliofanya mashauri masaa machache yaliyopita umeendelea kusisitiza kuwa hakuna jambo lolote ambalo serikali ya CCM itafanya litakalozuia CCJ kupata usajili wa kudumu kwani haki za maelfu ya Watanzania ambao wameamua kujiunganisha chini ya chama hiki kipya ni lazima zilindwe na hata ikibidi kuzuia uchaguzi mkuu kufanyika hadi CCJ nayo ipate usajili wa kudumu.
Wakati huo huo CCJ inajipanga siku chache zijazo kutoa majibu kwa wazee wa Jiji la Dar kuhusu hotuba ya Rais Kikwete mbele ya wazee "wengine"; taarifa zaidi ya mkutano huo zitakuja mbeleni.
Akizungumza mapema leo na vyombo vya habari Bw. Tendwa amezungumza kwa kejeli kuwa ofisi yake haina fedha za kwenda kufanya uhakiki wa wanachama mikoani kama sheria inavyotaka akidai kuwa kutokana na shughuli mbalimbali za uchaguzi haitowezekana kufanya hivyo kwa sasa.
Hata hivyo, vi'nzi" hivyo vinadokeza kuwa msimamo huo wa Tendwa unatokana na maelekezo ya ushauri kutoka kwa Marmo ambaye kutokana na nafasi yake anatishiwa na mwanasiasa mmoja huko Mbulu ambaye ameonesha nia ya kutaka kugombea jimbo la MBulu kwa kupitia CCJ na ambaye tayari anaonekana kukubalika na hivyo, usajili wa CCJ utatishia moja kwa moja nafasi ya Bw. Marmo.
Pamoja na hilo uongozi wa CCJ uliofanya mashauri masaa machache yaliyopita umeendelea kusisitiza kuwa hakuna jambo lolote ambalo serikali ya CCM itafanya litakalozuia CCJ kupata usajili wa kudumu kwani haki za maelfu ya Watanzania ambao wameamua kujiunganisha chini ya chama hiki kipya ni lazima zilindwe na hata ikibidi kuzuia uchaguzi mkuu kufanyika hadi CCJ nayo ipate usajili wa kudumu.
Wakati huo huo CCJ inajipanga siku chache zijazo kutoa majibu kwa wazee wa Jiji la Dar kuhusu hotuba ya Rais Kikwete mbele ya wazee "wengine"; taarifa zaidi ya mkutano huo zitakuja mbeleni.