Elections 2010 Tendwa kuweka historia?

Pax

JF-Expert Member
May 3, 2009
268
87
Wachambuzi wa mambo ya kisiasa hapa Tanzania wanasubiri kuona kama Tendwa ataamua kujiwekea historia katika siasa za Tanzania kutokana na maamuzi atakayoyafanya kuhusu pingamizi alilowekewa Kikwete. Je ataweka kando itikadi na kuamua kufuata haki na uadilifu kwa kutimiza malengo na matakwa ya sheria ya uchaguzi?

Hebu tuangalie shtaka analoshitakiwa nalo Kikwete, la kutoa mishahara mipya kama njia ya kushawishi wafanyakazi wampe kura, Je linastahili kuitwa Rushwa? Nianze kwa kuangalia mifano ya nyuma ya nyongeza za mishahara, mojamoja kwa moja natazama nyongeza waliyoongezewa madaktari wakati walipogoma miaka michache iliyopita. Serikali kwa kusukumwa na athari za mgomo wa madaktari iliongeza mishahara nahisi bila kibali cha bunge, na hapa wanasiasa hawakuinuka kudai amevunja sheria. Tendwa anaweza kutumia mfano huu katika kufanya maamuzi, hata hivyo akifanya hivyo atakuwa amecheza karata vibaya. Ameongeza mishahara ya wafanyakazi pasipo kuwa na any emergency kwani wafanyakazi walishakubali kuwa serikali imegoma kuongeza mishahara. Zaidi ni kuwa serikali ilikuwa na muda mwingi tu wa ama kuwabembeleza wafanyakazi kama ambavyo Kikwete anafanya au hata kutoa nyongeza. Hii ina maana moja tu, Kikwete kaongeza mishahara ili kuwashawishi wafanyakazi wampe kura, There is no any other explanation. Hamna emergecy iliyokuwepo, hakuna mgomo wa wafanyakazi, kwa nini unaongeza mshahara wakati ulishakataa?

Tendwa anayo nafasi ya kujiweka katika historia kwa kuamua kuandika historia kama akiamua.

MUNGU IBARIKI TANZANIA,
 
Macho na masikio yetu yote kwake. Lakini kwa vile hapa kwetu watu wenye taaluma zao wamekuwa wakizizika ili kuyatetea maslahi binafsi, usishangae tunashindwa kushangaa kuwa kinachoamuliwa kinakuwa kiini macho!
 
Mnategemea nini wakati ameshasema chama kitakachoona hakijaridhika na maamuzi basi kiende mahakamani. Na mnajua mahaka ilivyochakachuliwa utasikia, "hili ni la kisiasa zaidi, liende bungeni"!!!! JIBU la tendwa linaonyesha wazi kuwa tayari solution anayo kabla hata pingamizi halijawasilishwa. Kinachofanyika sasa ni, wananchi waridhishwe vipi ili angalau waonekane wanafanya kazi!!!
 
I can bet my last shilling Tendwa hawezi kukubali pingamizi hili.
 
Mhhh,

Hapa ni kesi ya Nyani kapelekewa Ngedere. Anyaway wamefanya wakijua kuwa Tendwa can do nothing on this, na wala hana huo mshipa wa kuweza kufanya hicho. Ila wamepeleka ili haya mambo yaingie kwenye vitabu tu, records ziwepo kuwa walilalamikia hili. Hapa I understand.

Kuhusu kusema kuwa Tendwa anaweza kutumia mfano wa madaktari, naona hapa hakuna mshiko wowote. Madaktari walipogoma kipindi kile hakikuwa kipindi cha uchaguzi, na sheria ya matumizi ya fedha madaraka kwenye uchaguzi inatumika kipindi hicho tu na si kingine. Lakini Kikwete anakampeni kama raisi wazi wazi na anatumia advantage yake ya urais wazi wazi bila hata kujificha au ku-mask. Tatizo la Tanzania si kuwepo kwa sheria; ni enforcement ya sheria hizo! Inafanyika selectively pale watawala wanapotaka, full stop.

Umewasikia wakazi wa Mwanza wakilalamikia ujenzi holela wa Ma-Night clubs katika maeneo ya makazi ya raia?? Wakazi wenyewe hawajui kuwa shetani wao ni halmashauri yao ya jiji la Mwanza na madiwani wao. Hawajui kuwa tiba sahihi ni kuwaondoa madiwani wote, ili wapate meya mpya ambaye watamwambia aondoe tatizo hilo. Hipa ndipo tulipo.

Tendwa hawezi kufanya maamuzi yoyote magumu, kwani akijaribu zigo litamwangukia yeye peke yake!! Njia pekee ni watanzania wote kubeba jukumu la mabadiliko kwa kuwaondoa wale walioko madarakani, ili wale wapya watakaoingia tuwaambie kuwa hiki na kile hatukitaki. Hawa waliopo madarakani wameshakuwa NUNDA. Hatutaweza kuwabadili asilani, njia pekee ni kuwaondoa. simple!!
 
Itifaki kuzingatiwa, toka lini mtoto akasema baba kajamba? Funika kombe mwanaharamu apite
 
Not in Tanzania my friend. Ni sawa na kumshughulikia baba yako wakati unaishi kwake na anakuhudumia kila kitu na unajua ukimwasi huna pa kukimbilia. "The boss (JK) is always right".
 
Hawezi kufanya maamuzi yanayoweza kuiathiri CCM kwa kuwa yeye na hao waliokoCCM ni pete na kidole. Kabla hajateuliwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, alikuwa katika moja ya Mahakama Kuu, akavuruga kibarua kule akapigwa benchi.

Ilitoa Takrima ya Whisky kibao kumpelekea Mhe Bakari Mwapachu nyumbani na ofisina wakati huo Waziri wa Wizara ya Sheria kubembeleza apatiwe kibarua upya. Ndipo kutokana na takrima hizo kateuliwa kushika wadhifa wa Msajili wa Vyama vya Siasa baada ya Ndg Liundi kustaafu.

Alipoteuliwa akakuta Mafisadi ndani ya CCM wana mapango wa kugawana nyumba za Serikali, nasikia akahama kutoka nyumba yake binafsi huko Kimara alikokuwa akiisha na kuhamia Oysterebay ili naye aweze kuwa eligible kumilikishwa moja nyumba ya Serikali, mali ya watanzania wote.

Baada ya kufisadi moja ya nyumba za watanzania wote, nasikia amerudi huko kijijini kwao Kimara, na kuipangisha hiyo nyumba ya wananchi na yeye kujipatia madola ya Kimarekani kibao kila mwezi.

Kwa msingi huo hawezi kuchukua hatua yoyote tengible. Tusubiri tuone kama Fisadi anaweza kuwaumbua Mafisadi wenzake
.
 
Haya mambo yanawezekana, kama Tendwa asipotenda haki! nahisi mikakati ipo tayari, imeshaundwa, hakuna kurudi nyuma! litakuwa kombora lenye vikombora ndani vingi ambavyo vikifumka hakuna cha Tendwa wala JK.

Litawafanya Chadema wazidi kuwa juu zaidi na ndio yanayotafutwa hapa.

Hesabu zilishapigwa, Tendwa akijiengua kwenye lawama, kuna stage tayari ipo kwenye mikakati. Watu hawalali wanachanga karata hapo. Mimi nauhakika hapa lazima mtu atoke nje ya ulingo (akae pembeni, JK).
 
Not in Tanzania my friend. Ni sawa na kumshughulikia baba yako wakati unaishi kwake na anakuhudumia kila kitu na unajua ukimwasi huna pa kukimbilia. "The boss (JK) is always right".

Wazungu wanasema "you do not bite the hand that feeds you" kwahiyo its unrealistic kufikiri kuwa Tendwa atafanya chochote kuhusiana na hilo anasema analishughulikia ili tu aonekane kama vile he is going to do something but in reality decision ilishafanyika anavita time tu...
 
Ni ngumu kwa Tendwa kufanya agaist the system. Wait and see...

Hizi siku tano ni za kutafuta wanasheria guru wa katika na mambo yanayohusiana na hayo watengue faulty ua Mbayuwayu. Kumbuka hata hao wanasheria watakaoitwa watengue huu mtego pia wako compromise na wameshahu taaluma yao, watajikomba kwa Mbayuwayu ili wasisahauliwe kwenye ufalme wa Mbayuwayu pindi akipita!!

Mimi kwa upnda wangu sioni jipya hapa!! Yale yale tu...
 
Mbona alishatoa maamuzi Alhamisi iliyopita kwenye kipindi cha "Tuambie"- TBC, kuwa hiyo si rushwa ni ahadi?
 
Akitenda haki Tendwa, utakuwa muujiza wa kwanza mwaka huu, mingine mingi itafuata. Namwomba Mungu muujiza huu utokeeee.
 
Tendwa akifuata sheria na kumtosa ata loss nini kwani JK atakuwa rais tena rais si atakuwa Slaa .Go Tendwa onyesha busara fuata sheria si ulikuwa Judge ww weka historia
 
Back
Top Bottom