Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 975
- 47
na Edward Kinabo
MSAJILI wa vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, anakusudia kukichukulia hatua Chama cha DP, iwapo itabainika madai aliyotoa Mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila, kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, yalilenga kukichafua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka mjini Dodoma, Tendwa alisema kama msajili na mlezi wa vyama vya siasa nchini, ana jukumu la kulinda kanuni za maadili ya vyama vya siasa ambazo haziruhusu siasa za kuchafuana baina ya vyama na vyama.
Alisema, ofisi yake itapitia madai ya Mtikila na iwapo itabainika kuwa yalipata baraka za DP na yalikuwa na lengo la kuichafua au kuiathiri CHADEMA kisiasa, hatasita kuchukulia hatua zinazostahili.
Nimesoma kwenye vyombo vya habari kwamba Mtikila amewatuhumu Mbowe na Mengi kuwa walifadhili mpango wa mauaji ya Wangwe. Sasa Mengi ni mtu tu si chama cha siasa na Mbowe naye ni mtu, si chama cha siasa.
Sasa kama alituhumu watu, basi ni jukumu la watu hao wanaodai kukashifiwa kwenda kumshitaki maana ni hivi karibuni Mtikila huyu huyu alifutiwa kesi ya kumkashifu rais aliyepita, Mkapa. Kwa hiyo kama wamekashifiwa nao wanaweza kwenda kumshitaki.
Lakini kama shutuma za Mtikila ziliigusa CHADEMA kama chama, hapo ofisi yangu itachukua hatua zinazostahili dhidi ya DP. Tutalitazama suala hili na kuchukua hatua, alisema.
Wiki iliyopita, Mchungaji Mtikila, alielezea kile alichokiita mpango kamili wa kumuua Wangwe, akidai kuwa aliuawa na watu kutoka Kenya ambao walikodiwa kwa kazi hiyo.
Katika madai yake hayo, alimtaja Mbowe kuwa mmoja wa watu waliofadhili mpango huo na mfanyabiashara, Reginald Mengi, ambaye hata hivyo hajazungumzia lolote kuhusu madai hayo.
Juzi akihutubia mkutano kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Mbugani jijini Mwanza, katika maadhimisho ya mwaka mmoja tangu CHADEMA itangaze orodha ya mafisadi 11, Mbowe alisema CCM inatumia wapinzani kutoka vyama visivyo makini, ili kukitumia kifo cha Wangwe kuendesha propaganda za kukidhohofisha chama chake.
Source: Tanzania Daima
MSAJILI wa vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, anakusudia kukichukulia hatua Chama cha DP, iwapo itabainika madai aliyotoa Mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila, kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, yalilenga kukichafua Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka mjini Dodoma, Tendwa alisema kama msajili na mlezi wa vyama vya siasa nchini, ana jukumu la kulinda kanuni za maadili ya vyama vya siasa ambazo haziruhusu siasa za kuchafuana baina ya vyama na vyama.
Alisema, ofisi yake itapitia madai ya Mtikila na iwapo itabainika kuwa yalipata baraka za DP na yalikuwa na lengo la kuichafua au kuiathiri CHADEMA kisiasa, hatasita kuchukulia hatua zinazostahili.
Nimesoma kwenye vyombo vya habari kwamba Mtikila amewatuhumu Mbowe na Mengi kuwa walifadhili mpango wa mauaji ya Wangwe. Sasa Mengi ni mtu tu si chama cha siasa na Mbowe naye ni mtu, si chama cha siasa.
Sasa kama alituhumu watu, basi ni jukumu la watu hao wanaodai kukashifiwa kwenda kumshitaki maana ni hivi karibuni Mtikila huyu huyu alifutiwa kesi ya kumkashifu rais aliyepita, Mkapa. Kwa hiyo kama wamekashifiwa nao wanaweza kwenda kumshitaki.
Lakini kama shutuma za Mtikila ziliigusa CHADEMA kama chama, hapo ofisi yangu itachukua hatua zinazostahili dhidi ya DP. Tutalitazama suala hili na kuchukua hatua, alisema.
Wiki iliyopita, Mchungaji Mtikila, alielezea kile alichokiita mpango kamili wa kumuua Wangwe, akidai kuwa aliuawa na watu kutoka Kenya ambao walikodiwa kwa kazi hiyo.
Katika madai yake hayo, alimtaja Mbowe kuwa mmoja wa watu waliofadhili mpango huo na mfanyabiashara, Reginald Mengi, ambaye hata hivyo hajazungumzia lolote kuhusu madai hayo.
Juzi akihutubia mkutano kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Mbugani jijini Mwanza, katika maadhimisho ya mwaka mmoja tangu CHADEMA itangaze orodha ya mafisadi 11, Mbowe alisema CCM inatumia wapinzani kutoka vyama visivyo makini, ili kukitumia kifo cha Wangwe kuendesha propaganda za kukidhohofisha chama chake.
Source: Tanzania Daima