Najaribu kutumia tembocard mastercard online lakini haiwi recognized, ambaye anatumia au aliyewahi kutumia anielekeze
duh? Ngoja nitaenda later benki nikaone wananihelp vipi, mi naona ni rahisi kushop online kama kuhost au kununua softwares kuliko kununua kibongo bongo.
Watakuibia hao wanaweza kuuzia kitu dola 100 ukaona rahisi then shipping mpaka bongo ikakukost dola mia zengine
Mi binafsi nahitaji huduma ya VISA tu with my TEMBO/MASTERCard lakini sasa sijaelewaga shida ni nini, maana tangu niwe na hiyo Card sijaweza kabisa ku'draw pesa kwenye ATM ya Bank nyingine zaidi ya CRDB, au ndo tuseme huduma ya VISA haipo nini kwenye TEMBO/ MASTER Card?
Inategemea na ATM za bank husika. Kama bank haitumii hizo VISA cards au Master Cards usitegemee ATM zake zitakubali mtu wa bank nyingine mwenye VISA card achomoe pesa kirahisi kwani hizi transactions ziko centralized sehemu, its like a Power Pool. Kwa hiyo unapotaka kudraw pesa kwenye ATM ya bank nyingine, inabidi uangalie hiyo ATM inakubali VISA cards au la. Otherwise, zinakubali bila matatizo with some little charges different from the normal one.
Nashukuru mkuu, lakini nimekuwa nikijaribu kutumia ATM za Bank kama NBC, BARCLAYS & STANCHART, ambazo bila shaka zote hizo zina'support huduma ya VISA [kama ambavo nimekuwa nikizitumia bila ya matatizo yoyote kwa kutumia TEMBOcard VISA yangu ambayo ilikwisha muda wake ndipo nika'process hii TEMBOcard MASTERcard nikidhani ingekuwa na more advanced features maybe, sasa cha ajabu kila nikijaribu kuitumia for VISA kutoa pesa kwenye ATM napata ujumbe like "YOUR TRANSACTION HAS BEEN DECLINED BY YOUR ISSUERER ...[or something like that], sasa sijui hii maana yake huwa ni nini hasa, hebu watu wa CRDB waliopo jamvini watatusaidie labda.
Watakuibia hao wanaweza kuuzia kitu dola 100 ukaona rahisi then shipping mpaka bongo ikakukost dola mia zengine