Kuna jamaa yangu kaniambia kwamba kuna hiyo association inaitwa TEDET (Tanzania Eco-Development Trust), kwamba inakusanya hela za wanachama kiingilio sh. laki 5 (500.000) ambayo inajumuisha kiingilio ada ya uanachama na shamba la ukubwa wa hekari 5 huko bonde la mto RUFIJI. Kasema makubaliano ni kwamba mwanachama anapewa hilo shamba heka 5, ila anakuwa analimiwa hilo shamba heka 4 mazao ya biashara na heka moja mazao ya chakula.
Mazao ya chakula atakuwa akipewa magunia 20 ya mahindi /mpunga kwa msimu yaani misimu miwili kwa mwaka, wakati mazao ya biashara yatakuwa yakiuzwa kwa pamoja masoko ya nje na kila heka ikikadiliwa kutoa mazao ya wastani wa thamani ya milioni 1.5, lakini mkulima atakuwa akikatwa laki 2 kila heka kama garama ya uendeshaji.
Kasema hiyo Tedeti inashirikiana na KIMUDEA umoja wa wakulima wilaya ya Kinondoni, na wakazi wa Rufiji chini ya umoja wao wa RUDIDEA na kwamba wanachama wanapelekwa kuonyeshwa mashamba huko Rufiji.
Nilipo search goggle nikakuta kweli hiyo kitu ilikuwepo toka mwaka 2006, na mwenyekiti wake ni Dr. Mugishagwe. Na kuna pesa mamilioni mengi, toka kwa wafadhili zimekuwa zikiingia huko TEDET, taarifa zipo ukigoogle za upokeaji wa pesa hizo. Hakuna taarifa zaidi kuhusu huu umoja, kilimo hata hizo ada za uanachama.. Kasema ofisi zao zipo MASASI HOUSE KARIAKOO?
Kweli nikaona maelezo yake ni mazuri, lakini nikapata hofu kwamba je hii haiwezi kuwa DECI ama PUFDEA nyingine? Manake hii kusanya ya kiingilio cha laki 5 kila mwanachama, na kasema wanatakiwa wanachama elfu 10,000. Na kasema wengi sana wamejiunga. Na ahadi ni kwamba wanaanza kilimo mwaka huu.
Ndipo nikaona pengine niimwage hapa kwenye Jamvi nene labda kuna wenye datas za uhakika nisije ingia mkenge wa DECI no.2
Na kama kweli si DECI, basi wanajamvi tuchangamkie uanachama kwani maelezo yake ni mazuri.
Asante wakuu.
Mod. tafadhali iacheni kwa muda hapa tupate datas
Mazao ya chakula atakuwa akipewa magunia 20 ya mahindi /mpunga kwa msimu yaani misimu miwili kwa mwaka, wakati mazao ya biashara yatakuwa yakiuzwa kwa pamoja masoko ya nje na kila heka ikikadiliwa kutoa mazao ya wastani wa thamani ya milioni 1.5, lakini mkulima atakuwa akikatwa laki 2 kila heka kama garama ya uendeshaji.
Kasema hiyo Tedeti inashirikiana na KIMUDEA umoja wa wakulima wilaya ya Kinondoni, na wakazi wa Rufiji chini ya umoja wao wa RUDIDEA na kwamba wanachama wanapelekwa kuonyeshwa mashamba huko Rufiji.
Nilipo search goggle nikakuta kweli hiyo kitu ilikuwepo toka mwaka 2006, na mwenyekiti wake ni Dr. Mugishagwe. Na kuna pesa mamilioni mengi, toka kwa wafadhili zimekuwa zikiingia huko TEDET, taarifa zipo ukigoogle za upokeaji wa pesa hizo. Hakuna taarifa zaidi kuhusu huu umoja, kilimo hata hizo ada za uanachama.. Kasema ofisi zao zipo MASASI HOUSE KARIAKOO?
Kweli nikaona maelezo yake ni mazuri, lakini nikapata hofu kwamba je hii haiwezi kuwa DECI ama PUFDEA nyingine? Manake hii kusanya ya kiingilio cha laki 5 kila mwanachama, na kasema wanatakiwa wanachama elfu 10,000. Na kasema wengi sana wamejiunga. Na ahadi ni kwamba wanaanza kilimo mwaka huu.
Ndipo nikaona pengine niimwage hapa kwenye Jamvi nene labda kuna wenye datas za uhakika nisije ingia mkenge wa DECI no.2
Na kama kweli si DECI, basi wanajamvi tuchangamkie uanachama kwani maelezo yake ni mazuri.
Asante wakuu.
Mod. tafadhali iacheni kwa muda hapa tupate datas