Tears of Joy..

Wi-Fi

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
2,091
1,378
Hello Chit-chatters..

Napenda ku-share japo kwa kifupi sana siku ya kwanza kulia kwa furaha..
Kitambo nilipokua fomu tuu kuna binti nilimpenda sana na nikawa namtengenezea mazingira takriban mwaka mzima! Siku ikafika nikasema kesho "liwalo Na liwe" napiga saundi (namtokea)..

Jioni ikawa imefika nimeshaandaa nguo nzuri ili kesho nikutane nao huku naendelea kujipanga kimashairi, Ghafla nilipokea barua kupitia Mutual friend..

Nikaipokea na kuisoma: (ndani ya barua) "Tokea nimekuona siku ya kwanza moyo wangu wote ulipata ganzi na kila siku najaribu nitakupataje ili niyaseme yamoyoni mwangu.. Leo nimeshindwa kuvumilia nimeona nikueleza kwamba nashindwa kuvumilia kukupenda" kwa kifupi yule binti alieleza hivyo kwenye barua!! Kijana wa watu namalizia kusoma ile barua nikajikuta nimeloanisha ile karatasi kwa machozi.

Mara ya kwanza kutoa machozi ya furaha ilikua siku iyo.

Please share your experience in brief.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom