TCU is a really ****en place

JF2050

JF-Expert Member
Sep 25, 2010
2,085
40
Nilikuwa ofisi za TCU leo zilizopo maeneo ya Mikocheni. Kilichonipeleka ni shida waliopata watoto fulani ambao wapo mkoani wakati wakifanya application kwa ajili ya admission ya vyuo vikuu.

Nilipofika pale mapokezi nikaambiwa chukua form andika tatizo lako. Nikachukua form 2 nikaandika, na baada ya muda akatokea mtu anakusanya hizo form. Baadaye tukaanza kuitwa majina kwa ajili ya kuhudumiwa.

Ikafika zamu yangu nikaingia. Mle ndani kulikuwa na wahudumu wawili (ambao mie nawaita "dogs" utajua kwa nini), mmoja amekaa kwenye kiti ana laptop na pc, mwingine amesimama. Aliyesimama akaniuliza tatizo ni nini? Wakati huo ameshikilia form niliyoijaza ambayo ilikuwa na sehemu ya kuandika kueleza tatizo lililonipeleka. Nikamwambia tatizo limeandikwa hapo halafu nikamwelezea pia.

Baada ya sekunde chache, nikamwambia samahani, nimesubmit form mbili kwa maana sio mimi mwenye tatizo isipokuwa ni watoto fulani wapo mikoani wameniomba niripoti tatizo lao na hii ni mara ya pili nakuja hapa (na ni kweli ilikuwa mara ya pili kuripoti hilo tatizo). Kusema hivyo, jamaa aliyekaa akadakia na kusema hapa hujaja kueleza umekuja mara ngapi! Kwanza wewe ni dalali sisi hatudili na madalali, waambie wanafunzi wenyewe waje!

Nikawaambia jamani hao wanafunzi wako mbali, halafu ukizingatia tatizo ni la system yenu, kwa nini mnataka waingie gharama ya kuja na wakati nimeripoti hili tatizo na hii ni mara ya pili? Basi wakaanza fujo: toka kama hutoki tunakuitia polisi. Nilipatwa na hasira sana nikaamua kutoka.

Nikajiuliza maswali mengi sana mojawapo ni kama hiyo ofisi ni ya mtu binafsi na ana uhuru wa kufanya apendavyo au ni ya serikali?

Sasa naomba kama kuna mtu yeyote anayejua wafanyakazi wa ofisi hiyo ya TCU "computer system administration" anipe majina yao kamili na details zao zingine ili kama tatizo la hao madogo halitashughulikiwa na kupelekea application zao kutoprocessiwa niwashtaki au nideal nao ninavyojua mimi.

Wale wahudumu mie kwa kweli nawaona kama mbwa, kwa tabia yao mbovu achilia mbali uwezo wao mdogo wa kufikiri na kufanya kazi. Isingekuwa ofisini kwao kuna uwezekano mkubwa ningeingia hatia kwa kupiga mtu, maana hii nchi inachosha hata ukilalamika husikilizwi.

TCU siitaki hawana uwezo wa kufanya kazi. Internet-based system yao ya application ni mbovu na hawana utaalamu wamelazimisha tu project ili watengeneze hela hali wakijua hawawezi. Nenda hapo ujionee lundo la watu wanaoripoti matatizo yaleyale kila siku lakini hayatatuliwi.

Mwisho ikitokea watu wanaandamana sasa hivi ili TCU ifutwe mie nitakuwa mmoja wao.

Please nipeni majina na details za hao mbweha.
 
pole sana ofisi zote tanzania zinaohudumia wanafunzi hasa kutoka secondary huwa zinawadharau na kuwafukuza kama majibwa kwa hiyo kama wanataka chuo ni bora uende direct kwenye hicho chuo kuliko kukomaa na hao majibwa kama unavyo waita..
 
hawa wameajiriwa kupitia ndugu zao kwa vimeno unaweza kukuta wamesomea fani znyingine kabisa
 
kweli system yao hawa jamaa inasumbua mbaya kabisa hapa penyewe nilikua namsaidia
jamaa yangu imegoma haitambui vyeti sijui toka wiki mbili zilizopita sasa hawa jamaa kama
wanashindwa hata kauli kwa wateja wo itakuaje???????????????????? mi nachoka nao
 
Ahsanteni kwa comment zenu. Nitajaribu kwa jitihada zangu kudeal nao. Ngoje tu nipate info zao.
 
Dah! Pole sana,yaani mi nimepata hasira utadhani mimi ndo niliyejibiwa hivyo. Sina details za hao jamaa,ila akili zao ni kama vile wapo chooni wamechuchumaa.Ndo hivyohivyo hata ukiwapigia simu,majibu yao ndo kama hayo.
 
Halafu hata ukipiga simu yao all the time busy. Niliwahi kusema hapa kuwa hawajui walifanyalo. Unakusanya hela za watoto wa maskini na bado wanataka kuwadhulumu.
Kila kona Tanzania wizi mtupu!
 
Halafu hata ukipiga simu yao all the time busy. Niliwahi kusema hapa kuwa hawajui walifanyalo. Unakusanya hela za watoto wa maskini na bado wanataka kuwadhulumu.
Kila kona Tanzania wizi mtupu!

Unayosema ni very true!
 
Dah! Pole sana,yaani mi nimepata hasira utadhani mimi ndo niliyejibiwa hivyo. Sina details za hao jamaa,ila akili zao ni kama vile wapo chooni wamechuchumaa.Ndo hivyohivyo hata ukiwapigia simu,majibu yao ndo kama hayo.

Ahsante mkuu
 
Pole Transcend....naelewa frustration yako. Ukipata majina yao wafundishe adabu
 
m*****u yao!!!Wanajifanya wanacope na technology kumbe ubabaishaji tu!Narudia tena m*****u yao!!!
 
m****du yao kabisa, nimepata gadhabu mbaya mno, coz me ni victim wa izo abar, sure wanajifanya database wanaijua, chek xaxa, kilasiku kero...mammbwa kabisa
 
Ukitokea Ubungo Panda Mabasi yanakwenda MWENGE ukifika MWENGE panda mabasi yanakwenda POSTA kupitia SAYANSI ukifika kituo SAYANSI shuka ulizia njia ya ROSE GARDEN BAR ifuate hiyo hiyo njia(au kama una senti kidogo chukua BAJAJ waambie unataka kwenda TCU. kusu uliyetimuliwa TCU pale ulipoondoka ndo uliharibu kaka ungeeng'ang'ania humo humo mpaka kieleweke. Mimi nakumbuka wakati nasoma chuo tulikuwa tunajaza fomu na kuzipitisha kwa Mkuu wa Wilaya nakumbuka nilizipeleka kwa MKUU WA WILAYA TEMEKE(enzi hizo JOHN CHILIGATI secretary wake akawa anatufukuza siku hiyo nikadinda sitoki mpaka nimuone DC) mbona alifyata Mkia na fomu ikasainiwa siku hiyo hiyo. So ACHA WOGA ukiitiwa POLISI kitu gani mbele ya haki yako?kwani umeiba?
 
Ukitokea Ubungo Panda Mabasi yanakwenda MWENGE ukifika MWENGE panda mabasi yanakwenda POSTA kupitia SAYANSI ukifika kituo SAYANSI shuka ulizia njia ya ROSE GARDEN BAR ifuate hiyo hiyo njia(au kama una senti kidogo chukua BAJAJ waambie unataka kwenda TCU. kusu uliyetimuliwa TCU pale ulipoondoka ndo uliharibu kaka ungeeng'ang'ania humo humo mpaka kieleweke. Mimi nakumbuka wakati nasoma chuo tulikuwa tunajaza fomu na kuzipitisha kwa Mkuu wa Wilaya nakumbuka nilizipeleka kwa MKUU WA WILAYA TEMEKE(enzi hizo JOHN CHILIGATI secretary wake akawa anatufukuza siku hiyo nikadinda sitoki mpaka nimuone DC) mbona alifyata Mkia na fomu ikasainiwa siku hiyo hiyo. So ACHA WOGA ukiitiwa POLISI kitu gani mbele ya haki yako?kwani umeiba?

Sure! Alitakiwa kukomaa palepale, au la angeenda kwa next boss. hawa jamaa hawana huruma na watanzania wenzao.Binafsi nina shida na applications,nimewapigia mara kibao simu iko busy, niliwapata siku moja wakanisubilisha kwenye line mpaka ikakatika. Next week nazuka mwenyewe pale kutokea mkoani. Hawana maana hawa!
 
Pole mkuuu....
Mfumo wa CAS ni rahisi ukijua mambo fulani. Kwanza internet ni lazima iwe ya kasi, not modem!!! Natumia broadband internet ya TTCL iko faster, nimesaidia watu kibao, vijana wetu!!! Pia tumia browse ya Google Chrome, kazi ya TCU utamaliza kwa glass ya juisi ukitabasamu....



Hao vinguruwe hapo ofisini TCU nakuomba uende tena, vaa kivingine, ukiwakuta, tegesha simu uwapige picha!!!! Ili tuzianike hapa jamvini.... Ofisi za Umma ni mali ya wananchi!!!!
 
watz wengi hawajali huduma kwa wateja, wanadhani huduma bora kwa wateja ni baa au restaurant peke yake..sasa dawa yao wewe wavalie njuga, nenda tena siku nyingine na fuata taratibu zilezile za kujaza fomu, wakijitia ujuaji komaa nao na ikibidi dai kuonana na bosi wao. Kama bosi wao haeleweki nenda kwa bosi wake, fuata mlolongo huo hadi ikulu kama vipi. Bila hivo hawatajirekebisha kamwe hawa wahuni.
 
Ukitokea Ubungo Panda Mabasi yanakwenda MWENGE ukifika MWENGE panda mabasi yanakwenda POSTA kupitia SAYANSI ukifika kituo SAYANSI shuka ulizia njia ya ROSE GARDEN BAR ifuate hiyo hiyo njia(au kama una senti kidogo chukua BAJAJ waambie unataka kwenda TCU. kusu uliyetimuliwa TCU pale ulipoondoka ndo uliharibu kaka ungeeng'ang'ania humo humo mpaka kieleweke. Mimi nakumbuka wakati nasoma chuo tulikuwa tunajaza fomu na kuzipitisha kwa Mkuu wa Wilaya nakumbuka nilizipeleka kwa MKUU WA WILAYA TEMEKE(enzi hizo JOHN CHILIGATI secretary wake akawa anatufukuza siku hiyo nikadinda sitoki mpaka nimuone DC) mbona alifyata Mkia na fomu ikasainiwa siku hiyo hiyo. So ACHA WOGA ukiitiwa POLISI kitu gani mbele ya haki yako?kwani umeiba?

Kuwa makini na comment zako. Sikuogopa polisi niliondoka baada ya kuwa na hasira sana, na mpaka sasa nimepania kudili nao. Ngoja nisubiri wasishughulikie lile tatizo nililoripoti ndio watajua mie ni nani, watajutia huo uhayawani walioufanya. Nachotafuta ni details kuhusu wao, nikikosa mtu wa kunipa hapa nitazifuata huko2 TCU.
 
Back
Top Bottom