Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Imefika wakati sasa kwa mamlaka zinazohusika kusikiliza malalamiko ya wananchi ili ufumbuzi upatikane. Sasa hivi mitaani, kwenye mitandao ya jamii watu wanapiga kelele kuhusu wizi wa kampuni hii ya simu inayoitwa TIGO. Siamini kama mamlaka husika mfano TCRA hawalijui hili, kwani bila shaka miongoni mwao wapo wanaotumia mtandao huu. Wabunge wetu najua nao miongoni mwao wapo wanaotumia mtandao huu. Hata uongozi wa juu wa kampuni hiyo siamini kama hawajui kinachofanyika katika kampuni yao. Huduma zao zimekuwa mbovu na gharama kubwa. Sioni sababu ya kukata pesa mtu unapiga simu, unayempigia kama simu yake haipatikani, ukichelewa kidogo kuondoka hewani. Wanakata salio. Mbaya zaidi kama una tatizo ukitaka kuwasiliana na mshauri au huduma kwa wateja. Simu yao unalipia hata kama tatizo lililokupata limesababishwa na wao wenyewe. Kibaya zaidi simu yao ukipiga haipokelewi kamwe. Hebu kwa uchunguzi wa awali kama kuna muhusika kutoka TCRA hapa jamvini apige namba hii ya huduma kwa wateja TIGO aone kama itapokelewa: 0713800800. Tunaomba serikali na mamlaka zinazohusika zitusaidie wananchi. Ufumbuzi si kuhama kampuni, ni kutatua tatizo.