Idara nyeti ya usalama wa usafiri wa anga imetia aibu kubwa baada ya kukosa umeme katika jengo lao jipya baada ya kupata hitilafu ya umeme kwa siku nne mfurulizo, tangu ijumaa huku Generator zote mbili zikigoma kuwaka. wakati hali hiyo ikiendelea king'ola cha kuashiria moto kilianza kulia ghafla na kusababisha taharuki kwa wafanyakazi na wateja waliokuwepo ndani wakisubiri huduma ambayo imesimama kutokana na hali hiyo, watu walikuwa wanakimbia hovyo kusalimisha maisha yao, wafanyakazi walilazimika kuondoka mapema kwa kuwa hapakuwa na matumaini yoyote.