GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
TBS amkeni Magari USED ya Japan nayo Balaa si Samaki wa TFDA pekee
Asubuhi ya leo nimefuatilia mahojiano kati ya Mkurugenzi wa TFDA Ramadhan Msuya na Idhaa ya Kiswahili ya BBC inayotangaza kutoka Nairobi akiwatahadharisha umma wa Watanzania kujiepusha na sehemu ya shehena ya samaki wa kusindika waliosambaa kwa wauzaji wa rejareja kutoka Nchini Japan.
Samaki hawa hasa wanaotoka katika Miji ya Kobe na eneo jirani na ufuo wa kinu cha Nyuklia cha fukushima wanadaiwa kuwa na vinasaba vya mionzi ya Nyuklia ambayo ni hatari kwa afya ya Binadamu.
Sehemu kubwa ya shehena hii imezuiliwa katika maghala na TFDA huku sehemu ya shehena hii tayari inavinjari katika Mini-market zilizochipuka kama uyoga katika viunga vya miji mbalimbali ya Tanzania.
Ashkum si matusi, jana kidogo nami niingie mkenge kwa kutaka kunasa mkebe mmoja wa samaki wa Kopo wakati nafanya manunuzi Super Market, kwa bahati nzuri waziri wa mambo ya Ndani akanitolea nje vibaya…Haya hilo limepita salama
Swali langu na hofu ya watanzania wengine Ilikuwaje sehemu ya shehena hiyo ikapenya katika mamlaka husika hadi TFDA nao waanze kuisaka katika masoko? Wahusika wanayo majibu sahihi.
Katika mahojiano hayo Msuya alilikwepa swali la mwandishi aliyetaka kujua inakuwaje Tanzania Nchi yenye fuo nyingi na maeneo mengi ya kuwezesha uvunaji wa Samaki kuendelea kuagiza samaki kutoka Japan, alikwepa swali hilo kwa kusema kuwa '' tupeni nafsi TFDA tushughulike na majukumu yetu na kuwa hili jingine ni nje ya uwezo wa TFDA''
Kinachogomba hapa ni kusambaa kwa mionzi hii kutokana na kuvuja kwa kwa kinu cha fukushima kufuatia tetemeko la Ardhi na Tsunami katika ukanda huo wa miji ya KOBE Nchini Japan.
Miji ya KOBE inasifika sana kwa maarufu kwa kuwa na utitiri wa YARD za magari yaliyokwishatumika yanayouzwa katika nchi nyingi za Dunia ya tatu na Tanzania ikiwa ni soko mahiri sana kwa wafanyabishara wa Kijapan ambao sasa wamefungua matawi mengi katika jiji la Dar na Mwanza kwa kuwatumia mawakala wao.
Kwa mtaji huo haishii tu kwa kuwatolea macho samaki hao na tukayafumbia macho magari haya ambayo Yard nyingi ni biashara za watumishi wenye mamlaka.
My TAKE:
Vipi imekugusa hii Mdau, Chukua tahadhari wakati TBS bado wapo katika usingizi mzito.
ADIOS
Asubuhi ya leo nimefuatilia mahojiano kati ya Mkurugenzi wa TFDA Ramadhan Msuya na Idhaa ya Kiswahili ya BBC inayotangaza kutoka Nairobi akiwatahadharisha umma wa Watanzania kujiepusha na sehemu ya shehena ya samaki wa kusindika waliosambaa kwa wauzaji wa rejareja kutoka Nchini Japan.
Samaki hawa hasa wanaotoka katika Miji ya Kobe na eneo jirani na ufuo wa kinu cha Nyuklia cha fukushima wanadaiwa kuwa na vinasaba vya mionzi ya Nyuklia ambayo ni hatari kwa afya ya Binadamu.
Sehemu kubwa ya shehena hii imezuiliwa katika maghala na TFDA huku sehemu ya shehena hii tayari inavinjari katika Mini-market zilizochipuka kama uyoga katika viunga vya miji mbalimbali ya Tanzania.
Ashkum si matusi, jana kidogo nami niingie mkenge kwa kutaka kunasa mkebe mmoja wa samaki wa Kopo wakati nafanya manunuzi Super Market, kwa bahati nzuri waziri wa mambo ya Ndani akanitolea nje vibaya…Haya hilo limepita salama
Swali langu na hofu ya watanzania wengine Ilikuwaje sehemu ya shehena hiyo ikapenya katika mamlaka husika hadi TFDA nao waanze kuisaka katika masoko? Wahusika wanayo majibu sahihi.
Katika mahojiano hayo Msuya alilikwepa swali la mwandishi aliyetaka kujua inakuwaje Tanzania Nchi yenye fuo nyingi na maeneo mengi ya kuwezesha uvunaji wa Samaki kuendelea kuagiza samaki kutoka Japan, alikwepa swali hilo kwa kusema kuwa '' tupeni nafsi TFDA tushughulike na majukumu yetu na kuwa hili jingine ni nje ya uwezo wa TFDA''
Kinachogomba hapa ni kusambaa kwa mionzi hii kutokana na kuvuja kwa kwa kinu cha fukushima kufuatia tetemeko la Ardhi na Tsunami katika ukanda huo wa miji ya KOBE Nchini Japan.
Miji ya KOBE inasifika sana kwa maarufu kwa kuwa na utitiri wa YARD za magari yaliyokwishatumika yanayouzwa katika nchi nyingi za Dunia ya tatu na Tanzania ikiwa ni soko mahiri sana kwa wafanyabishara wa Kijapan ambao sasa wamefungua matawi mengi katika jiji la Dar na Mwanza kwa kuwatumia mawakala wao.
Kwa mtaji huo haishii tu kwa kuwatolea macho samaki hao na tukayafumbia macho magari haya ambayo Yard nyingi ni biashara za watumishi wenye mamlaka.
My TAKE:
- Tusiishie tu kupigia kelele minofu ya samaki, magari ni moja ya nyenzo muhimu inayoweza kutunza mionzi isiyokufa kwa zaidi ya miaka 100, utafiti wa kisayansi unathibitisha hili.
- Kenya wameanza jitihada hizi magari yote kutoka Japan yatakuwa yanapimwa Bandarini kabla ya kukanyaga ardhi ya kubaini kiwango cha mionzi kufuatia malalamiko mengi ya matatizo ya kiafya kwa watumiaji wa magari kutoka Japan kufuatia kadhia la fukushima. Endapo yatabainika kuwa contaminated yataharibiwa ama kurudishwa Japan.
- Japan pia kupitia The Japan Export Vehicle Inspection Centre (JEVIC) wamethibitisha kupokea malalamiko hayo na kuwa watafanya uchunguzi huo kupitia International Maritime Dangerous Goods Code and International Atomic Energy Agency's safety standards.
- JEVIC tayar wameingia mkataba na TBS ya Kenya ijulikanayo kama Kenya Bureau of Standards (Kebs) lakini hapa kwetu TBS kimya mpaka tufe tuishe na magari haya ya bei chee. Uchunguzi Nchini Kenya umeanza toka mwezi Mei na unayahusisha pia magari yanayoingia Nchini humo kutokea Dubai.
- JEVIC imethibitisha kuwa uchunguzi wa haraka umebaini magari 10 kati ya 5000 yamebainika kuwa yamebeba mionzi hii baada ya kuvuja kutoka kinu cha Fukushima.
Vipi imekugusa hii Mdau, Chukua tahadhari wakati TBS bado wapo katika usingizi mzito.
ADIOS