Tbc1 watoa hali ya kutisha mfumuko wa bei ya vyakula

BONGOLALA

JF-Expert Member
Sep 14, 2009
16,507
11,883
Kipindi cha mwaka 2005-2010 mfumuko wa bei ya vyakula ni ya kutisha nchini TZ kufikia na kuzidi 200%.Jamani hayo ndiyo maisha bora?au kipimo ni magorofa machache ya watu wachache yanayochomoza kila kukicha dar, arusha na mwanza peke yake? WANAUCHUMI TUSAIDIENI KWA TAFSIRI YA UCHUMI KUKUA
 
na bado, CCM wako tayari kuchakachua na wakifanikiwa huo mfumuko utafika 1000% na tutakuwa sawa na Zimbabwe
 
Bora enzi zile za Mkapa na waziri wake wa fedha (Mramba). Walikuwa angalau wanajua wanachofanya
 
UKISHANGAA TU VYA MUSA, UKIONA VYA FIRAUNI (PHARAOH) JE?

TAZAMA FULL NOTE JUNSI UCHUMI ULIVYOUWAWA NA HUYU JK...BILA HATA AIBU!!


KIONGOZI BEN WILLIAM MKAPA Vs J KIKWETE...(MZEE WA KUDONDOKA)

MWAKA 2000 -2004 Vs 2005-2009 - CHEKI MFUMUKO...WA BEI!

Unga 460 Vs 1000 = 217%
Mchele 600 Vs 1200 = 200%
Sukari 760/kg Vs 1600/kg = 210%
Mkate 250 Vs 700 = 280%
Maharagwe 360/kg Vs 1000/kg = 277%
Mafuta ya taa 450/lt Vs 1050 = 233%
Mafuta ya uto 178/lt Vs 720/lt = 404%
Nazi 100 Vs 550 = 550%
Mchicha/tembele 50 Vs 150 = 300%
 
Huumfumuko huu kamwe hutakaa uuone katika utawala mpya, utawala wa wenye maono na umakini...hadi waana na wajukuu wetu...na dr slaa atapoingia ikulu, n forever...ccm watang'atana memo hadi watoto na wajukuu wao, jumba jeupe watalisikia ktk bomba tu!
 
Nchi imepata maendeleo kwa kuwa na ongezeko la mabango yenye picha za JK kwa wingi na kwa ukubwa. Khanga, vitenge na kofia za CCM zimeongezeka sana mwaka huu. Na pia safari hii masuala ya kijamii yamezingatiwa kwa kuwashirikisha wanawake na watoto katika kampeni yaani Mama Salma, Ridhiwani na Miraji.

Tumeweza kuendelea sana kwa kununua vifaa bora kabisa vya kijeshi ili kuvunja shingo za wapiga kura wasipotaka kutuchagua, maana itabidi tuhakikishe kama Serikali CCM inalazimika kurudi madarakani. Tunajivunia sana Silaha za kisasa ambazo zitatumika vema baada ya uchaguzi huu.

Suala la mfumuko wa bei sio tatizo kwa CCM kwa sababu halimuhusu Ridhiwani, Miraji wala Halfani. Maisha bora kwa kila mtanzania maana yake ni kuwa hata bei zingeongezeka kwa 20 billion % bado watanzania hawawezi kudhani kuwa uongozi mbovu unasababisha hayo.

Japo suala la bei linatuhusu watanzania wote lakini ukilizungumzia na hasa kulalamikia juu ya mfumuko huo holela wa bei unaonekana wewe CHADEEEEEEMA. Yaani wabongo sie hata kwenye hili ambalo ni la wazi kabisa bado CCM inadai ni propaganda za upinzani, yaani kweli hatuoni hata vinavyotoka mifukoni mwetu??????

Kumbe kutetea haki yako ni kuwa CHADEMA!!!! Hata mfumuko wa bei hamuuoni. WHAT DO YOU DO WITH YOUR MONEY WHEN IT HAS BEEN DEPRIVED OF ITS PURCHASING POWER??????.....CHAMBIA!!!
 
AWAKATI WA MKAPA Vs KIKWETE!!

Unga 460 Vs 1000 = 217%
Mchele 600 Vs 1200 = 200%
Sukari 760/kg Vs 1600/kg = 210%
Mkate 250 Vs 700 = 280%
Maharagwe 360/kg Vs 1000/kg = 277%
Mafuta ya taa 450/lt Vs 1050 = 233%
Mafuta ya uto 178/lt Vs 720/lt = 404%
Nazi 100 Vs 550 = 550%
Mchicha/tembele 50 Vs 150 = 300%

unalipwa 100,000/-kwa mwezi kwa jedwali la hapo juu kila siku lazima
ununue unga robo 400, mchele nusu 300, uto kibaba 125, mafta taa
kipimo 300, sabuni nusu kipande 50, sukari robo 400, maharagwe robo
250, mkaa nusu kisado 300, nauli go & return 500, maji ya kunywa 500,
hapo ni bachalor kwa siku ni 3,125 mara 30 = 93,750 kwa mwezi. Okay
kodi kwa mwezi 20,000/- umeme 6000 kwa mwezi =total kwa mwezi ni
120,000/- je hiyo 20,000/- ziada katoa wapi????? ndo hizo mwisho wa
siku zina wapeleka jela au kuwanaachishwa kazi. Je maisha bora hapo
atoe wapi? Na je angekuwa na mtoto wa shule au watoto wawili? hapo
hajaumwa, hajatembelewa na mgeni akamnunulia soda, hajanunua nguo
nyingine!!!! Huyu mnaempigia kura hayajui hayo na hatambui kama una
familia kijijini pia. wao wanatibiwa na serikali, mafuta ya magari
kwao ni sawa na kumuuliza bibi akupigie story ya sungura. wenzie
wakitaka ongezo la mshahara wanajadiliwa in 2Hrs jibu tayari ila
waalimu na wenzao.........! 3 years.
 
I now remember maswali ya mtu mmoja mwema in 2005! Hivi mnajua vizuri JK? Huyu bwana sio kiongozi.
 
Dira hakuna na jamaa hapati picha...mbele haoni, nyuma haoni...anabaki ktk taarab na mipasho! Hata kagame kamuacha kilometers kibao mbali na taaba za interahamwe, na mambo na kimbari...uchumi wa rwanda unapaaa....!!
Huyu jamaa akapumzike tu ngurdoto kwa rafiki yake awaachie wanaojua kuongoza taifa hili tajiri, awe anaangalia ktk tv, ajute sawasawa...amepewa mkate wa siagi ka-shea na majibwa (mafisadi), kuwakemea hawezi, naye kageuka mwenzi wao...
 
Nazi shilingi 550? Mimi nishanunua nazi shilingi 50 si zamani sana, Hela yetu haina maana.
 
UKISHANGAA TU VYA MUSA, UKIONA VYA FIRAUNI (PHARAOH) JE?

TAZAMA FULL NOTE JUNSI UCHUMI ULIVYOUWAWA NA HUYU JK...BILA HATA AIBU!!


KIONGOZI BEN WILLIAM MKAPA Vs J KIKWETE...(MZEE WA KUDONDOKA)

MWAKA 2000 -2004 Vs 2005-2009 - CHEKI MFUMUKO...WA BEI!

Unga 460 Vs 1000 = 217%
Mchele 600 Vs 1200 = 200%
Sukari 760/kg Vs 1600/kg = 210%
Mkate 250 Vs 700 = 280%
Maharagwe 360/kg Vs 1000/kg = 277%
Mafuta ya taa 450/lt Vs 1050 = 233%
Mafuta ya uto 178/lt Vs 720/lt = 404%
Nazi 100 Vs 550 = 550%
Mchicha/tembele 50 Vs 150 = 300%

Duh! Halafu kuna Mitanzania huko inavaa njano na kijani na kushangilia utafikiri simba na yanga hii! Kweli upstairs hamnazo kabisa!
 
Kipindi cha mwaka 2005-2010 mfumuko wa bei ya vyakula ni ya kutisha nchini TZ kufikia na kuzidi 200%.Jamani hayo ndiyo maisha bora?au kipimo ni magorofa machache ya watu wachache yanayochomoza kila kukicha dar, arusha na mwanza peke yake? WANAUCHUMI TUSAIDIENI KWA TAFSIRI YA UCHUMI KUKUA

Tungepata data alizoleta mwenzetu, tungeweza kupata picha nzuri zaidi. Lakini posti zinaonyesha ni Mismanagemet of Kikwete Administration. Ingawa ni moja ya sababu halali. Hata Mkapa ni kama hivo tu. na mwinyi pia. Sidhani kua ccm uongozi wa sisiem unaridhika kwa sabubu wamekua kazini tangu Feb 1977. Upandaji wa bei kiholela kama hivo unasabishwa na sabubu za kua na hela nyingi lakini bidhaa chache. Au speculation investment, ambayo imeangusha uchumi wa nchi nyingi ikiwemo Greece hivi karibuni. Kwa mfano, Hela zote za (so called misaada) naona zimekaa Dar. Arusha, Mazoo. Karibia viwanda vyote vikubwa viko Dar, Arusha, Mwanza.bu tuzungumzeni mawili mawili kwanza,. Hii kasumba ni ya sisiem au ya wakubwa wanazotoka hizo sehem kufikiria manufaa ya ndugu zao kabla ya manufaa ya nchi. Hii ni problem ya nyerere ambaye alikua na sababu nzuri tu ya kurecycled bad apples (for the timebeing), well kulikua hakuna wataalam wakutosha. Wakuu ni wakati wakuvuna huu. yeye alitarajia ile mambo ya kuharibu kazi Tanesco kagera unahamishiwa Tanesco Kigoma au Tanga mpaka leo inaendelea. I think we have a culture issue, unless we admit it even Slaa is not gonna be successful, if he wins the election.

Hela nyingi Dareslam mpaka ATM runs out of money and they (managemnt) think they can control flow of cash into the public by limiting ATM transaction (thats how I look at it). Walipewa milioni 29 dola za kupunguza umasikini, unadhani hela ziko wapi? hapo hapo dar, arusha, mwanza nadhani. haya, karibia 80% ya micro loans wanapata watu Dar, Arusha, Mwanza. you are concentrate resources a three tiny locations. Only govenment and Banks can fix this. Hao watoa misaada wenyewe kazi yao kutoa misaada, lakini hapendi kugundua ile misaada ilifika inakwokwenda? Hamna namna watadanganywa wakose kujua, nadhani hujifanya wajinga. kwa sababu hivo sivo wanavyofanya wanaposaidia nchini mwao. Inawezekana wafanya kazi wao au mameneja hufanya Fraud. Hivi tunataka misaada ya nini? Ndio mana watu hawapendi kuondoka madarakani. na huenda hata uyu slaa au lipumba wakawa kama ccm.

Kupanda kwa bei za vitu ni Banki Kuu na Raisi ndio wanauwezo wa kulaumiwa. its a monetary and fiscal policy phenomenon. Na mtu ukitaka kusaidia kuchunguza haya mambo nibora kuanzia wakati wa nyerere baada ya vita ya uganda mpake leo. Solution is probable.

Wakuu huyu swali lake akaulize jamaa zetu wanaojaaliwa kupata kazi kule wizara ya uchumi na mambo ya fedha. tena watakupa mrundo wa data.
 
Naomba nikukosoe kidogo bwana Mziba, aina ya uchumi wa nchin yetu ni free, inamaanisha kwamba serikali haihusiki na upangaji wa bei za bidhaa.sababu ya huu mfumuko wa ajabu wa bei ni nyingi ila nita point moja tu ambayo mama ya sababu zote, POOR MANEGEMENT.

Haya matatizo yote yanasababishwa na wafanyabiashara wetu, wamejaa uroho mpaka basi, wao ndo wanajipangia bei tu bila ya sababu zozote, halafu serikali inakaa tu imefumba macho, kwa mfano angalia bei ya nazi, kutoka 100 hadi 500 sasa muulize muzaji kwa nini? atakwambia eti usafirishaji, haya muulize dereva mafuta shilingi ngapi?, haya pio muulize BP kwanini unauza mafuta bei ghali hivi? atasema soko la kimataifa bei imepanda. nenda soko la kimataifa ukaangalie,mafuta mwaka huu bei zimekua very stable.

tatizo ni kwamba wafanyabiashara wanajua kwamba watanzania wengi ni mambumbumbu, na badala ya serikali kuwalinda, yenyewe inawachekea tu wafanyabiashara, matokeo yake ona wafanyabiashara wanavyo kuwa matajiri na jinsi wafanyakazi wanavyozidi kuwa masikini.
 
AWAKATI WA MKAPA Vs KIKWETE!!

Unga 460 Vs 1000 = 217%
Mchele 600 Vs 1200 = 200%
Sukari 760/kg Vs 1600/kg = 210%
Mkate 250 Vs 700 = 280%
Maharagwe 360/kg Vs 1000/kg = 277%
Mafuta ya taa 450/lt Vs 1050 = 233%
Mafuta ya uto 178/lt Vs 720/lt = 404%
Nazi 100 Vs 550 = 550%
Mchicha/tembele 50 Vs 150 = 300%

unalipwa 100,000/-kwa mwezi kwa jedwali la hapo juu kila siku lazima
ununue unga robo 400, mchele nusu 300, uto kibaba 125, mafta taa
kipimo 300, sabuni nusu kipande 50, sukari robo 400, maharagwe robo
250, mkaa nusu kisado 300, nauli go & return 500, maji ya kunywa 500,
hapo ni bachalor kwa siku ni 3,125 mara 30 = 93,750 kwa mwezi. Okay
kodi kwa mwezi 20,000/- umeme 6000 kwa mwezi =total kwa mwezi ni
120,000/- je hiyo 20,000/- ziada katoa wapi????? ndo hizo mwisho wa
siku zina wapeleka jela au kuwanaachishwa kazi. Je maisha bora hapo
atoe wapi? Na je angekuwa na mtoto wa shule au watoto wawili? hapo
hajaumwa, hajatembelewa na mgeni akamnunulia soda, hajanunua nguo
nyingine!!!! Huyu mnaempigia kura hayajui hayo na hatambui kama una
familia kijijini pia. wao wanatibiwa na serikali, mafuta ya magari
kwao ni sawa na kumuuliza bibi akupigie story ya sungura. wenzie
wakitaka ongezo la mshahara wanajadiliwa in 2Hrs jibu tayari ila
waalimu na wenzao.........! 3 years.

ili mtanzania huyu asiibe/asikope/asidhulumu/asiombe rushwa inabidi mshara wake wa sasa hivi uwe na ongezeko la asilimia 297 toka kipindi cha mkapa hadi kikwete.
kw hiyo aliyekuwa akilipwa laki 1,angepasaw kulipwa laki 3 hivi.sasa kwa aina hiyo ya hyper inflation,ni wananchi machizi tu ndio wanaweza kumrudhisha kiongozi wa aina hii madarakani.
I am watching october 31st to see how far have we gone down the insane line.
imagine obama turns out just 100% inflation rates 2012..,even BUSH was better than this junk we have.
 
ili mtanzania huyu asiibe/asikope/asidhulumu/asiombe rushwa inabidi mshara wake wa sasa hivi uwe na ongezeko la asilimia 297 toka kipindi cha mkapa hadi kikwete.
kw hiyo aliyekuwa akilipwa laki 1,angepasaw kulipwa laki 3 hivi.sasa kwa aina hiyo ya hyper inflation,ni wananchi machizi tu ndio wanaweza kumrudhisha kiongozi wa aina hii madarakani.
I am watching october 31st to see how far have we gone down the insane line.
imagine obama turns out just 100% inflation rates 2012..,even BUSH was better than this junk we have.[/QUOTE

Mimi huwa najiuliza sana maswali: Ni nani huwa anaipigia kura CCM hadi ishinde kwa kishindo wakati karibia kila mtu ninayezungumza naye anaiponda CCM then at the end kwenye uchaguzi eti CCM inashinda? Au sisi tunaojifanya tunajua ubaya na uzuri wa CCM (inawezekana ni kweli tunajua) huwa hatupigi kura? Au tunadanganyana tu tunapokuwa tunaongea then mtu kimya kimya anapmigia kura kiongozi wa CCM hata kama hawezi kuongoza kwa sababu unakuta mpiga kura huyo ana link na wazee (vigogo wa CCM)? Au watu ambao kwao vyombo vya habari pekee ni simu za mkononi (ambao hata redio kwao ni msamiati, TV na magazeti nd'o usiseme) nd'o wapiga kura wengi nini? Kwa maana naona hao nd'o wanaozikimbilia hizo kofia na T-shirts za njano/kijani.

Kuna kata moja Wilaya ya Liwale inaitwa Mirui nilikuwepo huko wiki mbili zilizopita katika kuongea ongea mambo ya uchaguzi nikajikuta naongea na mpiga kura mmoja akasema: ''Mgombea ubunge wa huku ametuahidi atatuletea mnara wa simu''. Duh! Yaani pesa ambazo wanazipata kwa shida wazimalizie kwenye kununua voucher za simu ili wafanyeje? Wawapigie simu wamiliki wa ndege waje wawabebee mazao yao? (kwa maana miundo mbinu haifai). Hata huo mnara yeye nd'o anamiliki kampuni ya simu - wamiliki wa kampuni ya simu watapeleka mnara wa simu kwa sababu mbunge amesema?! Hii nchi jamani?! Unaweza kukuta amesikia wana mpango wa kupeleka mnara wa simu halafu yeye kawadanganya wananchi kuwa atawapelekea mnara wa simu! Mmmmh! Bora
mtu akunyime pesa/ mali kuliko kukunyima elimu.
 
Naomba nikukosoe kidogo bwana Mziba, aina ya uchumi wa nchin yetu ni free, inamaanisha kwamba serikali haihusiki na upangaji wa bei za bidhaa.sababu ya huu mfumuko wa ajabu wa bei ni nyingi ila nita point moja tu ambayo mama ya sababu zote, POOR MANEGEMENT.

Haya matatizo yote yanasababishwa na wafanyabiashara wetu, wamejaa uroho mpaka basi, wao ndo wanajipangia bei tu bila ya sababu zozote, halafu serikali inakaa tu imefumba macho, kwa mfano angalia bei ya nazi, kutoka 100 hadi 500 sasa muulize muzaji kwa nini? atakwambia eti usafirishaji, haya muulize dereva mafuta shilingi ngapi?, haya pio muulize BP kwanini unauza mafuta bei ghali hivi? atasema soko la kimataifa bei imepanda. nenda soko la kimataifa ukaangalie,mafuta mwaka huu bei zimekua very stable.

tatizo ni kwamba wafanyabiashara wanajua kwamba watanzania wengi ni mambumbumbu, na badala ya serikali kuwalinda, yenyewe inawachekea tu wafanyabiashara, matokeo yake ona wafanyabiashara wanavyo kuwa matajiri na jinsi wafanyakazi wanavyozidi kuwa masikini.

Ahasante Smiling Panda kwa kukosoa na asante kwa kupoint mama wa sababu Poor management, indeed. Hii mambo ya BP (kwanza kama ni hivo ni kuwafukuza au kama si umeona marekani ilivowafanya) ni matokeo ya poor management. Serikali yetu ni ya ubepari. Tufanyeni kama mabepari wenyewe au bora zaidi.
 
TBC wamejuta kurusha kipindi kama hichi.

Kuna tetesi mwandaaji wa kipindi amelimwa barua ya kujieleza kwanini asifukuzwa kazi.
 
Back
Top Bottom