TBC1: Selebuka

Injinia

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
849
26
Nimesikia taarifa kuwa TBC1 wanaanzisha kipindi kitakachoitwa "Selebuka"
Kwa uelewa wangu ni kwamba wameiga mfumo wa "Strictly come Dancing" au "Dancing with the Stars" vilivyoanzia Uingereza miaka ya 80 na Marekani baada ya hapo.

Mimi binafsi ni mpenzi sana wa hivi vipindi, haswa Strictly Come Dancing ya BBC1. Ila maswali yananijia:
1. Ni mtindo gani wa dansi watakaoshindanishwa hawa wasanii? Ballroom dancing?
2. Je tuna majaji wa kiwango cha kupima uchezaji wa ballroom dancing Tanzania au ndio wale wale akina Salama Jabir?
3. Ni lazima tuige kutoka nje?
4. Hatuwezi kubuni mashindano yetu wenyewe? Kama ya kucheza ngoma za kienyeji kwa mfano, badala ya kuziacha zife kifo cha mende?
4. Akina Juma nature na wenzake wa Temeke na wengine wa Manzese watafaidika nini na ballroom dancing?

Pendekezo: Tido Mhando, nafahamu una uwezo na pia influence kutoka BBC lakini nashauri uwe "ethnocentric"kidogo. TUSAIDIE KUDUMISHA MILA ZA JAMII ZA KITANZANIA.
 
Nimesikia taarifa kuwa TBC1 wameiga kipindi kitakachoitwa "Strictly come Dancing" au "Dancing with the Stars" aka "Selebuka"
Ni lazima tuige kutoka nje?
Namuquote Mzee wa Uwazi na Ukweli "Watanzania ni wavivu wa kufikiri...." twaiga tu, hatuko innovative maana mpaka mfumo wetu wa utawala tumeiga, bunge proceeding twaiga, maana tujiulize lile RUNGU na JOHO la 6 vinatutatulia vipi matatizo yetu kama WATZ? Tuige tu maana hatutaki kufikiria.
 
Back
Top Bottom