TzPride
JF-Expert Member
- Nov 2, 2006
- 2,616
- 1,167
Jana jioni niliangalia taarifa ya habari ya TBC1 nakuona jinsi hii TV ya uma ilivyo chafu! Walitoa habari ya ukosefu wa maji katika mjini wa Karatu. Ni aibu sana TV ya uma inayoongozwa na mtu aliyepata "exposure" ya jinsi vyombo vya uma vya wenzetu vinavyoendeshwa, yeye anafanya kinyume!
Hii habari ilikuwa ni kumchafua Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla. Hivi jamani ukosefu wa maji katika nchi hii ni habari kweli? haya ni maisha ya kila siku. Dar ni sehemu ngapi maji yanatoka muda wote, watu wasichote kwa madumu kutoka mbali? Kwa nini iwe habari kwa Karatu?
Ushauri wangu mafisadi wa nchi hii, mwisho wenu hauko mbali. Tumieni tu ulafi wa akina Tido Mhando na wengineo kwa maslahi yenu, lakini mjue wazalendo inatuuma na ipo siku tutaikomboa nchi yetu. Wakuu wa vyombo vya uma na wote wale wenye dhamana kama hizo, muogopeni Mungu----watanzania wamedhulumiwa sana kwa kitendo cha ninyi kuabudu mafisadi na kutumia dhamana hizo kwa maslahi yenu binafsi.
Nalaani kitendo hicho kiovu cha TBC1, kodi zetu mnatumia kwa manufaa ya mafisadi!
Hii habari ilikuwa ni kumchafua Dr. Slaa na Chadema kwa ujumla. Hivi jamani ukosefu wa maji katika nchi hii ni habari kweli? haya ni maisha ya kila siku. Dar ni sehemu ngapi maji yanatoka muda wote, watu wasichote kwa madumu kutoka mbali? Kwa nini iwe habari kwa Karatu?
Ushauri wangu mafisadi wa nchi hii, mwisho wenu hauko mbali. Tumieni tu ulafi wa akina Tido Mhando na wengineo kwa maslahi yenu, lakini mjue wazalendo inatuuma na ipo siku tutaikomboa nchi yetu. Wakuu wa vyombo vya uma na wote wale wenye dhamana kama hizo, muogopeni Mungu----watanzania wamedhulumiwa sana kwa kitendo cha ninyi kuabudu mafisadi na kutumia dhamana hizo kwa maslahi yenu binafsi.
Nalaani kitendo hicho kiovu cha TBC1, kodi zetu mnatumia kwa manufaa ya mafisadi!