wadau napata shaka kuelewa kwanini TBC1 hawaku cover habari ya Riz1 kujijitetea, juzi wala jana hawajaonyesha habari hiyo, je wana ajenda gani?station zote na magazeti walicover kwanini wao?
Si Mkurugenzi mpya pale TBC1 ni Mshana bana au ulichanganya kidogo Ma-Desa ukdhania kwamba kile kichwa kutoka BBC bado yupo ndani ya nyumba???
Sasa jiweke sawa kwamba TBC-RTD kamwe haiwezi kujiruhusu kuruka vihunzi ambavyo vilikua vikirukwa sana tu na TBC-BBC kwa maana ya kulinda ueledi kwa gharama yoyote hata kama maana yake ni kuondolewa kwenye ajira yenyewe.
Tangu sasa kwenda mbele pale TBC watu tujiweke utayari wa kupelekwa ki-ujima ujima mpaka habari gani iende hewani hadi waziri wa habari akatoe kwanza kimemo baada ya kushauriwa kwenye vikao RASMI.
Viewers wa TBC tulianza ku-feel pengo la Tido mara alipoondoka. Hata baadhi ya vipindi alivyoviasisi kama Usiku wa Habari havipo tena. Mechi muhimu hatuzioni tena TBC1. Hii ndio Tz.
Mkuu nakubaliana nawe haswaa! Ever since Tido aondoshwe pale professionally wanarudi nyuma in all wise, ikiwa ni pamoja na Programming na quality ya programs na signals. Jamani ni swala la kukosekana leadership yenye weledi.
TBC1 ni kichwa kuuma utawaona hata watangazaji hawajiamini kile wanachosome kwenye taarifa wameshakwisha tulihama ITV tukawaaminia kwenye taarifa tuemsharudi sasa bora uangalie ITV taarifa zao angalau
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.