Mkuu, hawana lolote. Wanaangalia sana hasa kipindi cha original komedy na bungecdm mlilisusia kutazama tbc
"Mtazamaji wa TBC1,hatutaweza kuwaletea matangazo ya bunge kutoka dodoma kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu mpaka hapo tutakapowataarifu tena, tunaomba radhi kwa usumbufu" hivyo ndivyo tangazo linavyosomeka hapa tbc1
Sasa ni lazima wananchi wote tuchachamae na kuihoji TBC, ni kwa nini chombo hicho kinaendeshwa kwa kodi zetu sote, wanachama wa CDM, wa CCM, na wa vyama vingine,lakini wao wanakiendesha kwa maelekezo ya ofisi ya Lumumba?!
Haihitaji mtu uwe na degree,ujue sababu ya kusitisha matangazo ya bunge leo,ni kuwa hivi leo ni siku ya maswali ya papo kwa papo,na kutokana na matukio mfululizo yaliyotokea nchini,kama vile matokeo ya kidato cha nne kufutwa, suala la Mwigulu na wenzake wa usalama wa Taifa kuwabambikia viongozi wa CDM,makosa ya ugaidi na tukio la kulipuiiwa kwa bomu, kwa kanisa la Arusha,ni dhahiri maswali ya kiongozi wa upinzani bungeni,Mbowe na makamanda wengine wa CDM,ni dhahiri leo bungeni kungrkuwa na shinikizo kubwa la vigogo wa CCM,kuachia ngazi,jambo ambalo Pinda,angeshindwa kulihimili,badala yake angebakia kutoa machozi kama ilivyo kawaida yake!!
Sasa kwa kuwa TBC,siku zote inafanya shughuli zake kwa kulinda maslahi ya CCM na viongozi wake, wameonelea wasitishe matangazo hayo,ili kumuepusha mzee wetu Pinda,kuonekana kwenye luninga akimwaga machozi ya kufa mtu!!!
TBC kwasasa wana mkurugenzi msikivu. Na lazima ajifunza yaliyomtokea Tido Muhando, haiwezekani kabisa Viongozi wanakuambia achana na Midaharo weka Ze commedy wananchi wafurahie wewe unang'ang'ania Midaharo tu.
hiki chombo kwa kweli akina nguvu ata kidogo TBC ina matatizo mengi sana kiuchumi kati mashirika ya serikali yalitelekezwa na kupewa watendaji vibaraka ni TBC hali yake ni mbaya sana kile kipindi cha kusoma taarifa ya habari kwa kutumia kibatari pale RTD (TBC TAIFA) NYERERE ROAD. inarudi akika.
"NI BORA KUPIGANA NA MTU ANAESIKIA KULIKO KUPIGANA NA KIZIWI KWANI ATA KAMA AMEKUZIDI NGUVU HAWEZI KUKUACHA HADI DAMU IKUTOKE"
Kuna kipindi watajikuta wanashindwa kutangaza chochote kwa kuhisi sasa kila kitu kiko against CCM. Manake mambo yanazidi kuongezeka kila siku. Bora waanze kuachane na matangazo yote tu kuanzia sasa, wapige taarabu manake mitaa ya pwani ina washabiki wengi.
Wanaficha uozo wa ccm wakati kila mtanzania anaujua mahakama imewaumbua baada ya kutenda haki!!! sioni maana ya tbc bora wazipe channel nyingene ridhaa ya kurusha live vipindi vya bunge, watu leo tulitaka kuckia kutoka serekalini kuhusu tuhuma za ugaidi dhidi ya chadema lakini ccm wametunyima haki yetu ya kupata habari!!! ccm + tbc ni wakuchingia baharini
Au inawezekana Lissu ameanza kuongea, maana yake hawa jamaa . . . .Wanaficha kitu
Hivi leo ni wizara gani? Watajidai tatizo la mitambo
Wanabodi:
Mimi na wewe kama walipa kodi wa nchi hii ambayo kwa njia moja ama nyingine ndiyo inasaidia kuendesha television ya taifa TBC,sasa naona ni bora ikaondolewa ruzuku hiyo kwa kutotimiza wajibu.Kuna mtu kanidokeza kuwa TBC si chombo cha Umma bali ni chombo cha Seriakali(kuna tofauti kubwa kati ya mali ya Umma na Serikali).
TBC imeshindwa kukidhi mahitaji au matarajio ya wananchi kwa maana ya wamiliki wa hiki kituo.
tazama hoja zenye maslahi ya jamii wao wanafanya ya kwao,urushaji matangazo ya moja kwa moja matatizo,ukitazama website yao hakuna habri mpya nk.
wana kipindi kinaitwa ZE COMEDY ambacho licha ya kuchekeza hivi sasa wanarusha matangazo ya biashara tu,huku wakitoa matangazo mpaka ya aibu kabisa katika TV ya taifa ,hata kama ni vichekezio.huwezi kutoa kichekezo kuwa 'chachandu ya chakula kwa wanandoa ni CONDOM' tena bila kuonesha kuwa ni uongozo,watoto wetu wanatazama huu upuuzi.
Tazama website yao leo katika kitengo cha video.
Video
na tazama website ya KBC (Kenya) na UBC (Uganda)
Kenya Broadcasting Corporation
UBC.ug - Uganda Broadcasting Corporation - UBC TV
Nina mengi ,nitarejea