JACADUOGO2.
JF-Expert Member
- Dec 13, 2010
- 930
- 217
Ndugu wana JF napenda kuuliza kuwa TBC1 ni shirika la umma wa watanzania au ni shirika la CCM? Tukiangalia mwenendo wa TBC1 kwa kweli inatukatisha tamaa sisi kama wananchi wa Tanzania tunakuwa na wasiwasi mkubwa dhidi ya TBC1. Kwa mfano ukifuatilia taarifa ya habari ya TBC1 kila siku lazima watoa habari za CCM hata habari zisizokuwa na msingi wowote kwa maendeleo ya taifa letu. Ukifuatilia mambo makubwa na makongamano na hata maandamano ya CHADEMA hayatangazwi wala hayazungumziwi TBC na watu wanaoalikwa kwenye kipindi cha jambo cha asubuhi TBC1 ni wale wale wa CCM kila siku! Je, watanzania tutafika?