AdvocateFi
JF-Expert Member
- Jan 15, 2012
- 11,492
- 5,040
Habari wana JF! Nimechukua fursa hii kutoa mawazo yangu juu ya mchezo mchafu unaofanywa na TBC1 ambayo inajiendesha kupitia kodi zetu, si jambo la ajabu kwa tbc1 kuipendelea CCM na upande wa pili ikiukandamiza upinzani kupitia habari zake, mfano tulishuhudia upotoshaji uliotangazwa na tbc1 kuhusu sakata la CDM na mkuu wa wilaya pale Igunga.
Pia tumeshuhudia tbc1 ikificha kutangaza hata habari muhimu za CDM na upinzani kwa ujumla, pia tumeshuhudia tbc1 ikitumia muda mwingi ktk kutangaza habari zinazohusu chama tawala mfano ktk miaka 35 ya ccm pale mwanza, pia tumeshuhudia TBC1 ikipotosha umma mara nyingi kuhusu sakata la mgomo wa madaktari kwa lengo la kuikingia kifua serkali etc...........
Sasa ni wito kwa viongozi makini wa CDM hasa waziri kivuli wa habari na utamaduni kulishikia bango swala hili ili sisi wananchi tupate tbc1 ambayo haina ubaguzi kwa maslahi ya taifa letu na si kwa maslahi ya magamba pekee.
Pia tumeshuhudia tbc1 ikificha kutangaza hata habari muhimu za CDM na upinzani kwa ujumla, pia tumeshuhudia tbc1 ikitumia muda mwingi ktk kutangaza habari zinazohusu chama tawala mfano ktk miaka 35 ya ccm pale mwanza, pia tumeshuhudia TBC1 ikipotosha umma mara nyingi kuhusu sakata la mgomo wa madaktari kwa lengo la kuikingia kifua serkali etc...........
Sasa ni wito kwa viongozi makini wa CDM hasa waziri kivuli wa habari na utamaduni kulishikia bango swala hili ili sisi wananchi tupate tbc1 ambayo haina ubaguzi kwa maslahi ya taifa letu na si kwa maslahi ya magamba pekee.