Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Siku ya jumapili ya tarehe 16 January kwenye kipindi chenu cha matukio yaliyojiri Arusha kati ya wanaharakati wa Chama cha Chadema na polisi kwenye kipindi chenu kwenye TV ya TBC 1 ni uchakachuaji mtupu! kwa mtu yeyote aliyenaakili kilichotokea Arusha ulikua ni uvunjaji wa haki za binadamu kwa polisi kuwapiga raia wasiokua na hatia, watu walishaapewa kibali cha kufanya mkutano na kuandamana bali polisi walitumia nguvu na ubabe kuwatawanya wafuasi wa Chadema kwa kuwapiga mabomu na kutumia risasi za moto pamoja na maji ya kuwasha, lakini katika kile kipindi kilichorushwa na TBC 1 sehemu kubwa ya matukio yote ilionyeshwa kua wafuasi wa Chadema ndio waliokua chanzo cha fujo hakuna sehemu niliona polisi wakiwa wanawapiga wafuasi wale kwa virungu nasema huu pia ulikua ni uchakachuaji kabisa kwakifupi mkanda ule waliufanyia EDITING na kuweka sehemu ya fujo kua ni Chadema tu ndio waliokua wanafanya fujo dhidi ya polisi. Nasema kuwa YOU CAN FULL PEOPLE SOMETIME! BUT YOU CAN NOT FULL PEOPLE ALL THE TIME!