Nakubaliana na wewe Mwanakijiji, tatizo lipo kwa wapangaji wetu wa Magogoni. Ukitembelea nchi zilizoendelea utakuta viwanja kama vya watu wanaishi mabondeni ni bei ghali mno. Kwanza kipo karibu na mto, pili kuna kama mlima. Nchi zilizoendelea hizo sehemu ni bei ghali kama viwanja vilivyo karibu na Bahari.
Tatizo liliopo hapa kwetu ni kwamba serikali haijali wananchi, haitengenezi miundombinu ya kupitishia maji machafu na safi na mazingira mazuri ya kuwafanya watu wanoishi (mabondeni kama wanavyosema) kupata hizo huduma, ingawa kupata hizo huduma hapa Tanzania ni ndoto kama tukiendelea na wajinga hawa waliotufikisha hapa tulipo kwa upuuzi wa watu wachache, uvivu wao wa kufikiria umefika kikomo zaidi ya kukwapua kodi za Watanzania na kuzitumia kwa matumizi yao binafsi bila ya kuwajali walipa kodi wenyewe.
Hebu angalieni Nyumba zilizo sehemu kama hizo za Mabondeni na hakuna mafuriko, tusiwalaumu wakazi wa sehemu hizo wakati tatizo lipo kwa wapangaji wetu wa magogoni wliofikia kikomo cha kufikiria na Wavivu ndani ya vichwa vyao
View attachment 43929
View attachment 43930
Nafikiri, lazima tukubaliane na hali halisi ya mazingira husika na si kujaribu kulinganisha kila kitu. Mfano ulaya, mito yao ni mitulivu sana utafikiri madibwi na ndio maana wanaweza kuitumia kwa usafiri.
Pili mvua ya ulaya ni manyunyu ya afrika sijawahi kuona mvua ulaya zaidi ya manyunyu na ili kutokee mafuriko lazima haya manyunyu ya ulaya yaneyeshe kwa zaidi ya miezi hivyo kwao inakuwa rahisi kupredict maana wanakuwa wanapima mito maji yalnavyongezeka na kuona ya kwamba baada ya siku fulani maji haya yatakuwa yamefika mita kadhaa na kumwagika.
Hii ni tofauti na hali ya afrika, mito inafujo uko km 20 kutoka mto ulipo unasikia mto unaunguruma, wakati ulaya upo sentimenta 1 kutoka kwa mto wala huusikii kama una unaunguruma.
Mvua za afrika hasa Tanzania zinanyesha kwa fujo, inaweza nyesha dakika 10 na ikasababisha mafuriko, tofauti na ulaya ambapo inanyesha miezi kadhaa.
Kwa hiyo kukabiliana na majanga hasa ya afrika, kitu namba moja ni kuhama mabondeni, tukihama mabondeni itawapa fursa jwtz kuwasili na boat yao moja kabla maji hayajafika nyanda za juu.