CITYBOY
Member
- Nov 1, 2010
- 42
- 0
Tanzania haina dini bali wananchi ndio wenye dini,hivyo katiba inawaruhusu wote kuabudu pasipo kuvunja sheria.Uislam uko wazi pia hivyo msiojua tuulizeni tuwafundishe.Uongozi katika Uislam unamaadili yake mfano kiongozi lazima awe mtusafi na akubalike kwa tabia njema na awe mwadilifu katika uongozi wake.Kiongozi awapendelee na kuwahurumia raia wake kwa kuwapa huduma yao inayostahili.Sasa anapopewa Muislam kungoza anatakiwa aongoze kwa kivuli cha Uislam na kwakua kama Tanzania haina dini basi Muislam huyu itabidi kwanza awe mnyenyekevu mbele za Mungu na pia atekekeleze sheria za nchi.Kama mtu anajina na hafuati ule mwelekeo wa Uislam kwa kutenda haki basi yuko mbali na Uislam pamoja na Mungu,kwa maana anaifuata na kuiabudu nafsi yake na matamanio yake binafsi.Hivyo MAFISADI na WEZI wahukumiwe kwa dhambi zao na usiandamwe Uislam kama wengi wafanyavyo hapa JF.Anayefanya dhambi hizo uislam hauko naye na tayali wamejitenga wenyewe kwa kuukanusha Uislam.Uislam siotatizo bali tatizo ni wao viongozi.Ingelikua ni sheria ya Uislam kwa kubainika kashfa kiongozi anang'atuliwa.Hivyo kama JK ana matatizo msimuhukumu kwa DINI yake bali muhukumuni yeye kama yeye na si UISLAM na Waislam.